Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki Kuelekea Ijumaa

Habari za muda Makapuku waaminifu, yeah, waaminifu maana kila siku tunatia timu humu na hatujawahi kulalamika kuwa kuna kitu tunakosa. Zaidi ni ukweli kwamba ambao hawako humu wanakosa mengi mazuri na hata tukiwapelekea tunafaidika nayo humu (kuanzisha thread kutokana na yaliyojiri humu) bado wa mwanzo ni wa mwanzo tu.

Kuna anayebisha? Huku tunauliza majibu maswali yanapoteza muda.

Tunakutana tena usiku huu huku tukiwa na muda mchache tu kuikaribia 'furahidei'. Kwa makusudi kabisa nakuwish happy almost furahiday Kapuku mwenzangu.

Well, ni wakati wa ka-kipengele ka buruduni ya gitaa katika muziki. Leo tunaangalia muziki wa band, yeah yaani kama mfano wa tancut Almasi enzi zile, bana Beta na nyingine nyingine, sema nini ujue, hii iko wapwa zake malkia LizzyII yaani US of A.
Tunamwangalia mwanadada Samantha Fish na band inaitwa Samantha Fish Band, hawa wanapiga Blues la kisasa sio lile la Chicago la kina Buddy Guy and co. Hapa gitaa na ngoma za umeme zinakung'utwa sawasawa kiasi kwamba inahitaji milo saba na si miatu kama tuliyozoea.

Muziki na upigaji wake wa gitaa umekuwa ukifanana sana na SRV (Nitamleta hapa huyu nguli, na kama unakumbuka wakati nimempandisha BB King alikuwa BB, Buddy, na Stivie Ray Vaughan).

Keshashinda tuzo katika muziki wa Blues huko USA na nyimbo zake kukamata chati kadhaa

Asante kwa Mondray aliyetoa darasa la kulink sasa nina link hii clip ya YouTube umuone mwanadada Samantha Fish akitumbuiza

SN: Nyie ni watu bora kabisa kutumia muda pamoja. LLL


00f2a6a11192dc6deac7bd1f63606ba9.jpg
bdbf3a5e0bacfd13af3a10795412f5b5.jpg
Nchi zilizoendekea ukizaliwa na kipaji ni tiketi ya utajiri
Bongoland njaa tupu
.........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom