Camilo Cienfuegos
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 19,228
- 68,246
1904 - Shirikisho la Soka la Kimataifa ( FIFA ) laanzishwa huko Paris, Ufaransa.
ujinga mtupu, kwani askari wa kike hajapata mafunzo
Mimi niliambiwa nitumie Chibuku muulize Bibi Vipi Ataiweza????![]()
Shikamoo Makapuku
Nategemea hapo ulipo haujambo
Huku nyumbani bibi khajambo lakini aliniambia nikujulishe kuhusu ile kitu yake ya siku zote kama imepanda bei
Zamani aliipate kwa anko deby kwa tsh 100 lakini tokea waseme no viroba imepanda kweli
Nimejitahidi kuzunguka mitaa ya kina shemera nako tabu nimekosa
Nimejaribu kumpigia anty Shinune kasema eti nae kaokoka hakika kama jinsi ujuavyo bila kupatikaña hiyo kitu sidhani kama bibi kesho ataamka
Bibi kasema ni kueleze wewe anko Kapuku kwa kuwa anakuaminia hasa zile styre zako zakuchomekea suruali yenye viraka huku ukitembea kwa madaha mfano wa ile band ya Tarumbeta anaamini kama utakasa hakika huwezi kikosa kabisa....
Basi kama utapata usije kuleta hadharani nakuomba ufunge vilivyo ili watoto wasije kungamua kilicho chonde chonde usiache sory....
Wako Akupendae
Anko Zoba...

MorningMorning mkuu
NdioKumbe alikuwa na hisa hapo CRDB
Pamoja sana mkuu ChaplinShukrani mkuu shululu kwa magazeti
Aisee, RIP Rajiv1991 - Waziri Mkuu wa zamani wa India, Rajiv Gandhi anauwawa katika shambulizi la kujitoa muhanga lililofanywa na mwanamke mmoja huko Madras.
Hii ajali ilikuwa kubwa sana, pia mamlaka zetu hazijui kuzuia abiria kujazana kwenye vyombo vya usafiri1996 - Meli ya Mv Bukoba yazama katika Ziwa Viktoria na kuua watu zaidi ya 700.
Ilikuwa ikitoka Bukoba kwenda Mwanza, ilizama karibu na pwani ya Bwiru.
Rais wa kipindi hiko, Benjamin Mkapa alitangaza siku tatu za maombolezo na bendera kupepea nusu mlingoti.
Makaburi ya wahanga wa tukio hilo yapo Igoma, Mwanza ambapo walioshindwa kutambuliwa na ndugu zao walizikwa hapo.
HBD Mr T1952 - Mr. T anazaliwa.
Ni msanii wa Movie na mwanamieleka wa zamani kutoka Marekani.