Makapuku Forum


Hii ni nadra sana
Watu wanashindwa waadhimishe ipi kati ya birthday na deathday
.....
 
Hadi leo nafikiri rekodi haijavunjwa
Ila Waafrika wa sasa ni mabingwa wa kudanganya umri/kupunguza miaka
......
Rekodi bado ipo imesimama haijavunjwa.

Kikosi kile cha Cameroon mwaka 1990 kilimfanya marehemu Pepe Kalle kutunga nyimbo mahsusi kwa Roger Milla na kikosi kizima cha Simba Wasiofugika ( Indomitable Lions ).

Ikumbukwe mechi ya ufunguzi wa Kombe la Dunia mwaka 1990 pale Italy, ilkuwa ni Argentina ( Mabingwa watetezi ) dhidi ya Cameroon.

Mechi iliisha kwa Cameroon kuifunga Argentina 1-0 , huku Diego Armando Maradona akibanwa vilivyo kabisa ( Man marking ) na Emanuel Kunde na matokeo hayo kuishangaza Dunia.

Cameroon ikaenda hadi robo fainali alitolewa na England. Hivyo kuwa timu ya kwanza ya Afrija kufika robo fainali ya WC.
 

Yaleyale ya Senegal 2002 pale Japan na Korea Kusini
Mechi ya kwanza walimtabdika bingwa mtetezi kwa nao 1 lililofingwa na Papa Bouba Diop
Ikafika hadi robo fainali
.......
 
Yaleyale ya Senegal 2002 pale Japan na Korea Kusini
Mechi ya kwanza walimtabdika bingwa mtetezi kwa nao 1 lililofingwa na Pape Diop
Ikafika hadi robo fainali
.......
Kweli matukio yanafanana sana.

Kikosi kile cha Marehemu kocha Bruno Metsu hakika kiliushtua Ulimwengu wa soka.

Wachezaji mahiri kama Tony Silva, Omar Daf, Khalilu Fadiga, Nahodha Aloiu Cisse ( kocha wa sasa ), Ferdinand Colly, Papa Bouba Diop, Hussein Diouf, Henry Camara na wengineo hakika kilikuwa ni kikosi cha dhahabu.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…