
ZABURI 55
16.Nami nitamwita Bwana naye ataniokoa
17.Jioni ,Asubuhi,na adhuhuri nitalalama na kuugua,Naye atasikia sauti yangu.
TUOMBE
Baba Mungu wa Mbinguni
Asante kwa ulinzi wako mchana kutwa,tunaomba toba kwavyote tuliyokosa kwa mawazo,maneno na matendo uturehemu.
Usiku huu Baba ,nyoosha mkono wako tufunike Baba kama kuku afunikavyo vifaranga
Naenda kinyume na pepo wa chafu,nguvu za giza uchawi usiwe na nafasi katika malango yetu usiku wa leo.
Tunamuombea SHIMBA YA BUYENZE BABA mponye jino Baba wa mbinguni,mtoe katika maumivu makali aliyonayo ukamtulize mwili na roho.
Baba wafariji wafiwa,wajane yatima ponya wagonjwa wote.
Tuna malaika wako watakatifu wazunguke vitanda vyetu na waweke vituo majumbani mwetu,Baba linda nyumba zetu damu Takatifu ikaponye nyumba zetu kwa hatari zote za kimwili na kiroho maana imeandikwa "...BWANA asipoulinda mji yeye aulindaye akesha bure..." ZABURI 127:1b Kesha nasi BWANA
Tunaombea ndoa,familia ,watoto na wote katika familia zetu ziwe familia takatifu kama ile ya Yesu,Maria na Yoseph
Mungu Baba tunakuomba utuamshe salama tukiwa na nguvu za kukutumikia,Roho Mtakatifu shuka utuongoze katika safari yetu ya mbinguni.
Tunaomba yote katika jina la Yesu mpatanishi na mwokozi wetu.
Amen
Tunawaombea marehemu wote wapumzike kwa amani
USIKU MWEMA WAPENDWA