BlessedHope
JF-Expert Member
- Jan 29, 2016
- 7,988
- 32,649
ZABURI 1131.Haleluya,Enyi watumishi wa BWANA ,Sifuni,lisifuni jina la BWANA.
2.Jina la BWANA lihimidiwe,Tangu leo na hata milele.
3.Toka mawio ya jua hata machweo yake Jina la BWANA husifiwa
4.BWANA ni mkuu juu ya mataifa yote,Na utukufu wake ni juu ya mbingu.
5.Ni nani aliye mfano wa BWANA ,Mungu wetu aketiye juu
6.Anyenyekeaye kutazama Mbinguni na diniani?
7.Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
8.Amketishe pamojs na wakuu,Pamoja na wakuu wa watu wake.
9.Huweka nyumbani Mwanamke aliye tasa,Awe mama ya watoto wenye furaha
TUOMBE
Mwenyezi Mungu Baba wa Mbinguni asante kwa kutuamsha salama.
Tunaomba utubariki siku ya leo tukinge na hatari mbalimbali na ajali mbalimbali za mwili na roho
Ponya wagonjwa,fariji wafiwa,wajane ,yatima watie moyo waliopondeka mioyo.
Bariki kazi za mikono yetu,tukumbuke tupate riziki halali.
Uwe kinga yetu siku ya leo tuweze kutenda yanayokupendeza,vinywa vyetu,mawazo yetu,yabariki wengine na kuponya
Leo ni siku ya wamama duniani,watie moyo wamama wote wawe wamama wenye kukupendeza sana na kubariki,wathamini familia na jamii na kutenda mambo ya kukupendeza Mungu wetu.
Asante kwa kuwa utatenda sawa na mapenzi yako Amen
MBARIKIWE SIKU NJEMA
