Aisee siku mbili tu10/Sultan Khalid Bin Bargash
Huyu alikuwa Sultani wa Zanzibar mnamo mwaka 1869 baada ya kifo cha binamu yake lakini akaonja madaraka kwa siku mbili tu
Waingereza baada ya kusikia Bargash kawa kiongozi wa Zanzibar walimpa masaa 24 aachie madaraka kwa hiyari yake lakini akawagomea na kupelekea baada ya siku moja kupita Waingereza watume meli zao za kivita na wanajeshi
Hapo ndo ikazaliwa vita iliyojulikana kama Anglo Zanzibar War ambayo ilidumu kwa muda wa dk 38 pekee iliyoisha August 27 1869 na kuwa miongoni mwa vita fupi zaidi kupiganwa duniani
Wakati wa vita hiyo Wazanzibar waliokufa na kujeruhiwa ni 500 wakati Mwingereza aliyeumia ni mmoja pekee, boti mbili zilizama
Hivyo jamaa alitawala kwa siku 2 tu
.........
Khaaa9/Diasdado CabelloHuyu bwana alionja Urais wa Venezuela kwa muda wa siku moja pekee baada ya Rais kujiuzulu kufuatiia kuonekana anasapoti ubepari
Hivyo Cabello akachukua madaraka kisha akamchagua Hugo Chavez kuwa Makamu wake halafu yeye mwenyewe akajiuzulu na Chavez kuwa Rais...mchezo ndo ulivyochezwa
Yaani kautumikia urais kwa muda wa siku moja pekee
..........
Usishangae yupo hadi wa dk 30Aisee siku mbili tu
hahahhh7/Roger LaFontant
Huyu alikuwa kiongozi wa kijeshi huko Haiti ambapo mwaka 1991 alikuwa Rais kwa masaa 24 tu
Rais alijiuzulu hivyo Katiba ya nchi hiyo kumpa madaraka Jaji Mkuu Estha Pascal Trouillot ambaye aliitisha Uchaguzi wa kidemokrasia lakini Fountant akatumia fursa hiyo kufanya mapinduzi na kujitangazia Urais lakini ghafla bin vuuuu wajanja zaidi yake wajampindua ndani ya masaa 24 tu yaani wakati anaamka tu huko Ikulu hata swimming pool hakugusa!!
...........
Aisee8/Ratu Tevita Momoedomu
Huyu jamaa alikuwa Waziri mkuu wa Fiji katika muhula/vipindi viwili vifupifupi kama stuli za Manzese..
Mwaka 2000 alikaa madarakani kwa masaa mawili pekee wakati mwaka 2001 alikaa madarakani kwa siku mbili
Mwaka 2000 yalitokea mapinduzi/maasi ambapo yeye pekee akajikuta ndo amebaki kwenye jengo la serikali hivyo kuwa kiongozi kama ngekewa vile halafu mwaka 2001 akachaguliwa tena baada ya kuachia madaraka ili kukidhi matakwa ta kikatiba
............
hahaha...h ata sura yake ipo kama aliyekurupuka5/Boris Yeltsin
Huyu mzee alijiteua mwenyewe kuwa Waziri mkuu wa Urusi mwaka 1998
Hii ilikuwa wakati yeye akiwa Rais na mgogoro wa kisiasa ukiwa umepamba moto hivyo akaamua kumpunguzia majukumu Waziri Mkuu kwa kujiteua yeye mwenyewe
Baada ya kukosolewa vikali na wananchi wake na wapinzani akaamua fasta kuachia huo Uwaziri na kumteua mtu mwingine
Yaani ndani ya masaa manne tu...kukurupuka ni kubaya!!!
.........
mmmh jamn mambo yakoMmeshindaje wapendwa
hahahaha aisee hatar thana6/Joseph GoebbelsHuyu alikuwa Kansela wa Ujerumani kwa muda wa masaa 5 pekee mwaka 1945 May 1
Wakati Vita Kuu ya Pili ikiendelea na Adolf Hitler kuonekana kuzidiwa akaamua kumteua swahiba wake Goebbels kuwa Kansela akiamini ni Waziri wa Propaganda ndo pekee anayeweza kumuokoa lakini hata kabla hawajaanza propaganda zao wakagundua wamezingirwa hivyo kuamua kujiua
Jamaa kaonja ukansela masaa yasiyozidi Matano pekee
........
Aisee6/Joseph GoebbelsHuyu alikuwa Kansela wa Ujerumani kwa muda wa masaa 5 pekee mwaka 1945 May 1
Wakati Vita Kuu ya Pili ikiendelea na Adolf Hitler kuonekana kuzidiwa akaamua kumteua swahiba wake Goebbels kuwa Kansela akiamini ni Waziri wa Propaganda ndo pekee anayeweza kumuokoa lakini hata kabla hawajaanza propaganda zao wakagundua wamezingirwa hivyo kuamua kujiua
Jamaa kaonja ukansela masaa yasiyozidi Matano pekee
........
Salama za wwhabar wanafamilia
tumeshinda salama sijui kwakoMmeshindaje wapendwa