Makapuku Forum

Mtumishi. Majaribio ya aina hii ni unethical kwa sababu implications zake ni hatari mno. Cross-breeding, DNA crossing/splicing na uhamishaji huu wa seli za ubongo hautakiwi kuachiwa tu ufanyike kiholela. Kuna siku atatokea rogue scientist huko North Korea achanganye DNA ya simba na binadamu kwenye lab ili kuzalisha wanajeshi wasioogopa halafu atuletee matatizo. Kama binadamu hatupaswi kuingilia uumbaji wa Mungu na kuanza kuhamisha DNA hovyo hovyo lakini huko ndiko tunakoelekea kwa sababu tiba za magonjwa mengi inaonekana zimejificha katika DNA na kwa kadri siku zinavyokwenda wanasayansi wanadai itafikia mahali wataweza kuzalisha binadamu asiyeugua wala kuzeeka.

Kama leo tunaweka brain cells za binadamu kwenye ubongo wa panya, vipi tukiweka kwenye ubongo wa simba, tiger au hata nyumbu? Tunacheza na moto!
 
Hatari sana, wataalamu wa DNA wanasema sisi binadamu tunatumia 4%tu ya DNA zetu, je 96% ziko wapi na zinatumikaje?
 
Kweli ,kuna clip nimeiona simba anamshambulia binadamu nimeogopa sana kweli wakizalishwa askari simba kumi tu korea hatarii
 
Unaendeleaje lakini?pole Ubarikiwe
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…