Mungu Baba Mwenyezi asante sana kwa kutuamsha tukiwa salama,tunakuomba utubariki siku ya leo ikawe njema ya kukupendeza,tunawaombea wagonjwa,wafiwa,wanaouguza,wenye changamoto yoyote Baba ukawape wepesi,tunawaombea wasafiri Mungu ukawalinde vyombo vyote vya usafiri majini,nchi kavu,angani viwe salama,Bariki kazi za mikono yetu Baba ili kila mmoja apate riziki halali,tunaombea ndoa zote,uchumba na mahusiano yawe ya amani.Baba tunakushukuru kwa kuwa utafanya sawa na mapenzi yako tunaomba na kushukuru katika jina la Yesu Mpatanishi na Mwokozi wetu Amen