Asante mkuu kwa updates mubashara ...ongera Samatta' team Europa yenu ...
Na Arsenal naona anajitahidi awezavyo kumfuata rafiki yake kipenzi man u ila yote tisa kumi Alexis Sanchez akitaka mshahara mnono ni haki yake ..... Ila pia akitaka kuondoka kwenda kutafuta mikono juu ni halali yake pia.... Mesut Ozil akitaka kuondoka ni halali kwake, ila pia akigoma kusaini kandarasi mpya ni haki yake pia..... Mzee Wenger akiomba mkataba mpya ni halali yake, ila pia akibebewa mabango ni haki yake pia. Watu wanataka mataji, wachezaji wanataka mataji ila mabosi wanamtaka mzee Wenger.
Kuna wakati akili zetu zinajidanganya kweli ila ukweli ni kwamba Arsenal ni Arsen wewe kubali wewe kataa. Mabosi wameshakubali Arsenal iwe halali yake na mashabiki hawamtaki wakiamini Arsen sio haki ya Arsenal.....
Endelea kujiuliza kwanini wazungu wamemjumuisha Alexis katika PFA player of the year list..... Alafu unalala wakati unajua uhalisia na ugumu wa michezo ya jumatatu.....
Vita ya top four sio mchezo.... Wacha tulaumiane maana huu Msimu ni wa lawama tu.
Tukutane kijiweni kwetu wakuu