Makapuku Forum

Makapuku Forum

Unaelewa jinsi upelelezi unavyofanyika? Siyo rahisi kama unavyodhani unless kama huyo Roma walikuwa wanajua aliko.

Kuhusu kauli kutofautiana serikali hii haina coordination na ni kila mtu na lwake. Ndiyo maana unakuta waziri anasema hichi, Mkuu kabisa anasema hichi, Bashite naye akiibuka anasema hichi ali mradi vurugu tupu.
Mzee wa serikali umekuja mbio km kawaida yako
Ni kweli sijui kitu!
Swali...walioongozana na Bashite Clouds ni akina nani?
Maana mwenzetu inaonekana una akili
.....
 
Una uhakika kuwa Roma amechukuliwa na watawala? Siamini kama watawala ni wajinga kiasi cha kufanya jambo la kijinga namna hii kwa mtu ambaye wala siyo hatarishi katika jamii.

Siasa ni mchezo wa kucheza na akili za watu. Sitashangaa kama mambo haya yanafanywa na kikundi fulani cha watu ambacho wala hakifungamani na watawala ili kuigombanisha na watawaliwa. Binafsi sikufurahishwa jinsi suala la Ben Saanane lilivyoshughulikiwa na mabosi wake huko chamani. Yaani ilikuwa kama vile kondoo kapotea na siyo mtumishi mtiifu mwenhe cheo cha Mwenyekiti wa Sera na Utafiti wa chama.

Yote kwa yote hata kama watawala hawahusiki, hawawezi kukwepa lawama kwa sababu ni wajibu wao kulinda raia na mali zao. Na siamini kama kweli TISS na vyombo vingine vya dola wameshindwa kujua walipo watu hawa. Ndiyo maana ni haki watu kuamini kuwa pengine watawala wanahusika.

Na kinachonishangaza zaidi ni jinsi serikali hii isivyojali. Haina hata ile dhana muhimu ya "political capital" - kutumia matukio kujiimarisha kisiasa na kufahamu kuwa tukio dogo tu linaweza kuwa na madhara makubwa sana kisiasa. Inashangaza sana!
Mzee wa kolomije uko deep sana well done
 
Bila shaka umeanza kunielewa kuwa serikali iko nyuma ya utekaji wa Roma, ninaposema serikali simaanishi ni rais bali waliopewa dhamana na kuaminiwa naye na wanayatumia madaraka na imani waliyopewa vibaya.
Bashite ni sehemu ya hiyo serikali, kauli yake ni kauli ya serikali ktkt eneo lake la utendaji ni rais wa darisalama
Huyu jamaa anafikiri humu wote ni pipo with low IQ kwavile tunapigaga stori hivyo hatujaelimika wala hatujui siasa chafu au nini na nini

Akisikia tunaikosoa serikali ya msukuma mwenzie basi atakuja rundo la maneno kudefend
Nimeishamzoea

........
 
597f2236688db5545612fdee88316f42.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom