Makapuku Forum

Makapuku Forum

Bunge laomba uchunguzi wa matunzo ya Faru Fausta
a9d26e5b21107ac9ada557dd9073b30d.jpg


BUNGE limeitaka serikali kutathimini gharama za matunzo zinazotumika kumtunza faru Fausta aliyepo katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro baada ya kubainika kuwa matunzo hayo yanagharimu Sh milioni 768 kwa mwaka.

Spika Ndugai aliiomba serikali kufanya tathimini hiyo wakati akijibu mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakanjoka (Chadema) aliyetaka kujua msimamo wa Spika kuhusu ukubwa wa gharama za malezi ya faru huyo.

Mwakanjoka aliomba mwongozo huo baada ya awali Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe kueleza sababu za msingi za serikali kuendelea kumtunza faru huyo pamoja na matunzo hayo kugharimu fedha nyingi.

Profesa Maghembe alilazimika kutoa majibu hayo katika swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul (Chadema) aliyehoji sababu za serikali kutumia Sh milioni 64 kila mwezi kumtunza faru Fausta.

Waziri akijibu alisema; “Ni kweli yupo faru Fausta katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro. Faru huyu amezeeka kweli na amekuwa akisumbuliwa na maradhi mbalimbali.”

“Hata hivyo, tumekuwa tunalazimika kuendelea kumtunza kwa vile zipo tafiti mbalimbali zinaendelea kufanywa kwake ili kusaidia katika kujua namna sahihi za maisha ya wanyama hawa ambao wamekuwa adimu sana duniani.

“Ni muhimu kupata takwimu za wanyama hawa ili tujue namna nzuri ya kuwatunza, ingawa ni kweli kuwa matunzo ya faru Fausta yana gharama kubwa ambazo kimsingi ndio gharama zenyewe za uhifadhi,” alifafanua Profesa Maghembe.

Alisema serikali inafanya hivyo kwa nia njema kwa vile gharama hizo zina thamani halisi za maisha ya wanyama hao adimu duniani.

Majibu hayo ndiyo yaliyomfanya Mwakanjoka kuomba mwongozo huo wa Spika ili kujua kama zipo sababu kwa serikali kuendelea kutumia kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa faru huyo mzee badala ya kuzielekeza kwenye matatizo ya wananchi.

NOTE: Faru Fausta ana miaka 54 alitimiza tarehe 29/1/2017 pia ni kipofu. Inasadikika ndiye Faru mzee kuliko wote duniani.
 
Bunge laomba uchunguzi wa matunzo ya Faru Fausta
a9d26e5b21107ac9ada557dd9073b30d.jpg


BUNGE limeitaka serikali kutathimini gharama za matunzo zinazotumika kumtunza faru Fausta aliyepo katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro baada ya kubainika kuwa matunzo hayo yanagharimu Sh milioni 768 kwa mwaka.

Spika Ndugai aliiomba serikali kufanya tathimini hiyo wakati akijibu mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakanjoka (Chadema) aliyetaka kujua msimamo wa Spika kuhusu ukubwa wa gharama za malezi ya faru huyo.

Mwakanjoka aliomba mwongozo huo baada ya awali Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe kueleza sababu za msingi za serikali kuendelea kumtunza faru huyo pamoja na matunzo hayo kugharimu fedha nyingi.

Profesa Maghembe alilazimika kutoa majibu hayo katika swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul (Chadema) aliyehoji sababu za serikali kutumia Sh milioni 64 kila mwezi kumtunza faru Fausta.

Waziri akijibu alisema; “Ni kweli yupo faru Fausta katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro. Faru huyu amezeeka kweli na amekuwa akisumbuliwa na maradhi mbalimbali.”

“Hata hivyo, tumekuwa tunalazimika kuendelea kumtunza kwa vile zipo tafiti mbalimbali zinaendelea kufanywa kwake ili kusaidia katika kujua namna sahihi za maisha ya wanyama hawa ambao wamekuwa adimu sana duniani.

“Ni muhimu kupata takwimu za wanyama hawa ili tujue namna nzuri ya kuwatunza, ingawa ni kweli kuwa matunzo ya faru Fausta yana gharama kubwa ambazo kimsingi ndio gharama zenyewe za uhifadhi,” alifafanua Profesa Maghembe.

Alisema serikali inafanya hivyo kwa nia njema kwa vile gharama hizo zina thamani halisi za maisha ya wanyama hao adimu duniani.

Majibu hayo ndiyo yaliyomfanya Mwakanjoka kuomba mwongozo huo wa Spika ili kujua kama zipo sababu kwa serikali kuendelea kutumia kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa faru huyo mzee badala ya kuzielekeza kwenye matatizo ya wananchi.

NOTE: Faru Fausta ana miaka 54 alitimiza tarehe 29/1/2017 pia ni kipofu. Inasadikika ndiye Faru mzee kuliko wote duniani.
kumbe hajafikia umri hata alio fikia bibi kidude!?!?

Let it go !!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom