2006 - Mtandao wa Kijamii wa Twitter waanzishwa rasmi huko San Fransisco, Jijini California nchini Marekani.
Ni moja kati ya mitandao yenye habari za haraka na watumiaji wengi.
Pamoja na kutimiza miaka 11 bado watu wengi wanashindwa kutumia mtandao huo.
1961 - Lothar Matthaus anazaliwa.
Kiungo wa zamani wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani.
Alikuwa kepteni wakati Ujerumani inatwaa ubingwa wa Kombe la Dunia mwaka 1990 pale Italia kwa kuifunga Argentina ya Diego Armando Maradona.
Ndio Mjerumani pekee mpaka sasa kushinda tuzo ya Mchezaji bora wa Dunia.
Ndio mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi kwenye timu ya taifa ya Nchi hiyo.
Ata mimi naona ngumu kweli kutumia...![]()
Hata mm situmii![]()
....
1963 - Ronald Koeman anazaliwa.
Beki wa zamani wa PSV, Ajax, Barcelona na timu ya taifa ya Uholanzi.
Pia amewahi kuwa kocha wa Ajax, PSV, Southampton na sasa Everton.
Moja kati ya mabeki bora wa kati wa muda wote, ambaye akiwa Barcelona aliifungia timu hiyo magoli 90 mengi yakiwa ni Freekick na penati.
Yeye ndio anaongoza kwa kufunga penati 46 kwa timu ya Barcelona katika La Liga mpaka sasa.
Pia anashika nafasi ya pili nyuma ya Leo Messi kwa kufunga goli nyingi za Freekick pale Barcelona.
Alitwaa ubingwa wa Euro mwaka 1988 akiwa na Uholanzi chini ya staa Marco Van Basten.
Kwasasa anapigiwa chapuo kwenda kurithi mikoba ya kocja wa sasa wa Barcelona, Luis Enrique.
1980 - Ronaldinho Gaucho anazaliwa.
Jina lake halisi ni Ronaldo De Assis Moreira.
Kiungo mshambuliaji wa zamani wa PSG, Ac Milan, Barcelona na timu ya taifa ya Brazil.
Anatajwa kama mmoja wa wachezaji bora wa wakati wote kuwahi kutokea katika ulimwengu wa soka.
Ameshinda kila kitu katika soka, Kuanzia Copa America mwaka 1999, Kombe la Dunia mwaka 2002, Uefa Champions League mwaka 2006, ubingwa wa La Liga mara mbili.
Pia ameshinda Ballon D'or mara mbili.
Alisifika kwa chenga zake za madaha, uwezo wa kukokota mpra na hata magoli adimu.
Mpinzani wake mkuu wakati anacheza alikuwa Zinedine Zidane wa Ufaransa, mpaka leo hakuna jibu sahihi kati ya Zidane na Ronaldinho nani alikuwa zaidi?
ata mm pia imenishinda nilishakua na acc yake![]()
Hata mm situmii![]()
....
shukran mussolin na kwako piaLEO KATIKA HISTORIA:
Sina la ziada niwatakie siku njema.
1986 - Michu anazaliwa.
Straika wa zamani wa Swansea kutoka Hispania