BlessedHope
JF-Expert Member
- Jan 29, 2016
- 7,988
- 32,649
Morning Be BlessedMorning friends
Morning Be BlessedMorning friends
1986 - Mapinduzi ya umma dhidi ya Serikali ya Philippines yaanza nchini humo kwa siku tatu na kufanikiwa kumuondoa Rais Ferdinand Marcos.
Mapinduzi hayo yalijulikana kama People Power Revolution. Pia hujulikana kama Philippines Revolution of 1986.
Poleeeeee ubarikiwe kwa kila unalofanya ufanikiweNipo, busy sana
AmenMorning Be Blessed
Naomba uirudishe ile avata yako ya mwanzoRudi juu kuna link ingia usome post nzima
1994 - Wakala wa CIA, Aldrich Ames na Mkewe wanashtakiwa na Serikali ya Marekani kwa kosa la kukubali kuuza siri za Nchi hiyo na kufanya kazi shirika la Ujasusi la Urusi KGB.
Aldrich Ames baada ya miaka 31 ya utumishi wake ndani ya CIA alijikuta akiwa " Double Agent " wa KGB jambo ambalo ni kosa la jinai.
Kwasasa anatumikia kifungo cha Maisha katika gereza lenye ulinzi mkali la Allenwood.
2002 - Kiongozi wa waasi nchini Angola, Jonas Savimbi anauwawa.
Aliuwawa baada ya mapambano makali kati yake na majeshi ya Serikali ambapo Savimbi alipigwa risasi 15 kichwani na kifuani hali iliyopelekea kupoteza maisha papo hapo.
1921 - Jean Bedel Bokassa anazaliwa.
Kiongozi wa zamani wa Afrika ya kati ambapo alikuwa ni Rais wa Pili wa Nchi hiyo.
Alikuwa ni dikteta aliyejitangazia Urais wa Maisha katika Nchi hiyo.
Alipinduliwa mwaka 1979 kwa msaada wa Majeshi ya Ufaransa.
Alifariki mwaka 1996.
1969 - Brian Laudrup anazaliwa.
Mchezaji wa zamani wa Ac Milan, Bayern Munich, Chelsea, Ajax na timu ya taifa ya Denmark.
Alikuwa ni straika, winga aliyeshinda ubingwa wa ulaya mwaka 1992 akiwa na timu ya taifa ya Denmark.
Pia alitwaa ubingwa huo kwa ngazi ya vilabu akiwa na Ac Milan mwaka 1994.
Pia kaka yake Michael Laudrup alikuwa ni mchezaji waliecheza nae pamoja.
1984 - Branslav Ivanovic anazaliwa.
Mchezaji wa zamani wa Chelsea ambaye anakipiga klabu ya Zenit St Petersburg .
Ametwaa Uefa champions league, Europa League, EPL, FA Cup akiwa na klabu ya Chelsea.