Makapuku Forum

Makapuku Forum

2001 - Yanatokea mashambulizi ya Kigaidi huko katika miji ya New York, ambapo ndege zilizoongozwa na Magaidi wa Al Qaeda wanashambulia jengo la Biashara la Kimataifa.

Katika tukio hilo maarufu kama " September 11 " pia walishambulia makao makuu ya Jeshi la Marekani " The Pentagon " na kusababisha watu takribani 3000 kupoteza maisha.

Baada ya hapo Marekani ikaanzisha vita dhidi ya Ugaidi, ili kuwasaka wale wote waliohusika ambao ni Al Qaeda chini ya Osama bin Laden.
 
1945 - Franz Beckenbauer anazaliwa.
Ni maarufu kama " The Kaiser "

Ni mchezaji na kocha wa zamani wa Bayern Munich na Ujerumani.

Anachukuliwa kama mchezaji bora wa Ujerumani wa muda wote japo alicheza nafasi ya Beki.

Ameshinda Kombe la Dunia akiwa Mchezaji mwaka 1974 na pia ameshinda kombe la Dunia kama kocha mwaka 1990 alipoiongoza Ujerumani kushinda dhidi ya Argentina ya Diego Maradona.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom