Makapuku Forum

Makapuku Forum

Babe anatakiwa kuwa mshamba kidogo... Siyo unadate binti anajua mpaka Lukaku alifunga mabao mangapi msimu uliopita??...
Demu unakaa naye anamjua Boro Yanki, Van Dame, Bill Branks.... Anakuadithia "anodi ya jini mwanzo mwisho"...
Yaani huna hata kipya cha kumfundisha...
Binti anatakiwa ukimuuliza "Bebi unamjua Rooney?? " anakujibu "Namsikia tuu.. Hivi ameimba wimbo gani?? "
Babe anatakiwa kuwa mshamba kidogo... Yaani eti babe anampenda Undertaker na Marehemu Umaga...
Binti anangaalia Movie ya Wrong Turn hata hajifichi amekodoa mimacho kuanzia mwanzo mpaka list ya majina inapita...
Babe anatakiwa ukiangalia naye Final Destination muda wote kafumba macho... Kila Mara anaongea na waigizaji... "Jamani wewe usiende utakufa huko" Mara unasikia "babe toa hii nitaota"...
Siyo Bae anakaza mdomo kabisa kwa hasira mtu akikoswakoswa kufa unamsikia kudadeki afe tu huyo anakihelehele..
BAE anatakiwa kuwa mashamba kidogo.
#BaeUshambaNiSexy.




 
1470336172774.jpg
 
Niliwahi kusikia hivi;
Ulaya mteja anaitwa mfalme,
Japani mteja anaitwa mungu
Afrika hasa tz mteja ni shetani.
Kauli hii ya mteja ni shetani nimejaribu kuifanyia utafiti sana.
Mfano unaingia duka la nguo unamkuta dada mrembooo mwenye simu kali na anachati...unajaribu kuchagua nguo, then unaamua kuanza kuuliza bei..lkn unakuta dada anachukua ka dkk 5 kukujibu halafu anaendelea kuchat, ukiuliza zaidi ya x3, anakujibu kwa karaha ..hivi wew ni mteja au unasumbua tu!
Kauli hii inaashiria jinsi muuzaji hajali mteja
Amwona kinyaaa au mdumbufu flani
Tubadilike mteja ni wa muhimu na anakupa jeuri
Ya kwenda msalani
....kachunguze, huyo dada sio mwenye biashara!!!....either ni mfanyakazi au mdogo/ndugu yake mwenye biashara....
 
Kisa cha kweli mtaani kwangu.
Kuna mzee mmoja alipitia duka flani kama mara mbili na akipitia hupenda kuuliza bei na kuonfoka na muuzaji ni bidada flani hivi.
Majuzi kati alikuja tena kama kawaida, wakati anakaribia dukani kabisa, yule dada muuzaji aliongea kwa sauti but aliongea kilugha....akimwambia shoga yake kuwa huyu mzee anakuwaga msumbufu sana...huuliza tuuuu bei bila kununua, so mimi naondoka wewe umsikilize.
Yule mzee kumbe alikuwa kabila moja na yule dada hivyo aliskia asemavyo
Mdada.
Mzee kusikia hivyo...alimjibu yule dada kilugha, binti udiondoke leo ninanunua...unisamehe mwanangu sikujua kuwa huwa ninakuudhi.
Nilikuwa naulizia ili nije kununua mwanangu.
Yule binti aliona aibu sana na alimwomba msamaha yule baba.
Mpendwa, usimdharau mtu na pia mjali mteja, ukimjibu vyema leo hata kama hajanunua, ipo siku atakuungisha
....aibu nimeona mimi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom