Ama kweli ubabe umepungua mtaani, hakuna muziki munene kwa magari kama ilivyozoeleka kwa vijana wa town, uchumi wa MTU mmoja mmoja umeleta utata
Magufuli shikamoo..
Bank nako hakuna foleni, tulizoea kuona foleni ndefu kuanzia kuweka hadi kuchukua pesa kwa ATM lakini hazipo tena, sasa ukienda bank unanyoosha kaunta,
Nasema tena shikamooo.
Ubabe wa matajiri na wenye Nazo nao umepungua, sasa tunaheshimiana.
Ninakuamkia..shikamooo.
Ofisi za umma Nazo zilikuwa na miungu watu, sasa no watumishi wa umma na sio miungu watu tena, baba Jesca shikamooo.
Umetumbua majipu bila ganzi na usaha umetudondokea mifukoni,
Mkuu shikamooo.
Wewe ni kiboko
Nasema shikamooo umeleta heshima MUJINI