Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ebhaneeeee, upo mitaa hiyo mdau. Hapo jirani na usalama nakuwepo sana. Nitakuibukia one time, tugonge vinywaji vya punguzo
Mkuu Obe , sijakuona hapa Masasi ingawa nilikuwepo hapa kwa siku mbili tatu, muda wa kuwa kwenye mji huu umeisha.
Shukrani za dhati kwa wadau wa Mkuti, Nyasa, Stendi, Rest, Namajani, Namalembo Chiungutwa, Lukuledi na hapa Mkomaindo.🙏🙏🙏

Wadau mliopo Tunduru tukutane weekend hì na mliopo Namabengo mnisubiri naja
 
Uzuri wa jukwaa hili, Makapuku, kuwe kumechangamka au kumepoa, bado unapoingia unapata utulivu fulani hivi wenye kumaanisha utakuwa na wiki njema. Na ndicho ninachotaka kukutakia wakati huu, wiki njema, na tayari tushaigawa kati Mei.
 
Well, jana kulikuwa na tukio ambalo si maarufu sana kwako wewe ambaye si mpenzi sana wa muziki wa country. Tukio lenyewe lajulikana kama 2026 Academy of Country Music na lilikuwa na MC mpya kabisa mwaka huu, huyu tunamjua wengi, maana enzi hizo wakongwe tupo shule za upili, nani ambaye hakuijua nyimbo yake 'You are Still the One".
Anyway, basi jana ndugu yenu kama kawaida, bundle halijagomba, nikatune Amazon Prime, wakirusha live toka Las Vegas, Nevada. Nikavutiwa na show, muziki live, show za wababe ikiwemo ile ya Blake Sheldon na wengine. Ila hapa leo nataka nikupe wimbo bora wa mwaka toka kwa Ella Langley ukiitwa Choosing Texas.



View: https://www.youtube.com/watch?v=hLOheGDwD_0&list=RDhLOheGDwD_0&start_radio=1
 
Imetangazwa tume ya rais ya kuchunguza jinai, rais anapambana kweli kweli kutaka kurejesha picha nzuri aliyoichafua kwa kutotaka kutoa nafasi sawa wakati wa uchaguzi. Hapa ni kama kuvaa suti mpya ya bei ghali na ukaamua kusimama jalalani.

Kama inaundwa tume ya kijinai, je tutegemee tume nyingine itakayoangalia masuala ya kijamii yaliyosababisha kadhia ya Oct 29? Tusichezee kodi za wananchi, jinai haiji kwenye haki, jinai inakuja pale masuala muhimu ya kijamii yanaposhindwa kuangaziwa na kupatiwa ufumbuzi. Utapata wapi haki ikiwa CCM wanapewa haki zaidi ya vyama vingine, utapata wapi haki ikiwa ajira ni tatizo ambalo halijapatiwa dawa sahihi, na mbaya zaidi ajira serikalini zimekuwa ni za kujuana ana upendeleo.
Utaikosaje jinai pale ambapo kwenda hospitali inaonekana ni anasa, health ineqaulities, utaikosaje jinai pale tabaka la maskini linakuwa kubwa kila kukicha na huku viongozi wakigawana minofu ya kasungura ketu bila kujali wote tunataka kula.

Viongozi wamekuwa matajiri na chanzo cha utajiri wao hakieleweki, ukihoji unaambiwa 'fanya kazi'. Kama hawajatajirika kwa kutuibia mali zetu kwanini kila siku wanaongeza mageti sehemu wanazosihi? Wanahofia nini?
Jinai haikosekani pale ambapo haki inaonekana kutoa upendeleo kwa wenye nacho na masikini wakibinywa kwa kutengenezewa sheria za kikuda za kuwambia achama ila usiongee.
Hapa Makapuku hatuongelei siasa tukiamini tunaweza kukudua kwenye umande, kumbe masika hayakuduliwi. Kudua
 
Back
Top Bottom