Makapuku Forum

Makapuku Forum

Hukuwahi Kuniita Kwa Jina Langu

Harakati za kukimbilia mapenzi zilinifikisha mbali sana, ndugu yenu nikatoka Mtwara hadi Dom, hapo nikakaa ila Moro ikanivutia sababu kulikuwa na muziki wa zamani unaopendwa na vijana. Ndugu yenu kijana mwenye mambo ya kizee na kwa sasa ujana unanikimbia, mvi zinakaribia kukicheka kitambi.

Mambo ya kizee yakanifanya nipende muziki wa zamani, ndugu yenu millennial ila mawazo ya kizazi cha X (mawazo machafu ukisikia X unawaza zile video zetu za kina mandingo zilizopotezwa na connection za kina Giggy Money). Kizazi X kilichotoa muziki unaoweza kuusikiliza bila kupata karaha za moyo. Na hapa ndo hoja yangu inapokuja sasa.

Mkongwe sana wa muziki wa country akienda kwa jina David Allan Coe kafariki jana, mkongwe alijua kupiga gitaa na wimbo wake " You Never Even Called Me by My Name" ullitamba sana enzi hizo, mashairi yaliyosimama sana, ukishajenga nchi kwa kunywa bia ya nne, unaenda mbele na kuanza kuimba, karaoke hiyo. Coe aliandika mashairi ya wimbo wa ukitaka sababu ya kuacha kazi "Take This Job and Shove It'

Ningepandisha fidyo hapa, lakini kama hujasoma mpaka mwisho, utawezaje kusikiliza gitaa linaloteta raha kama mshangazi aliyetoa meno ya bandia ili kupuliza inanda cha kushika na mkono.

Its almost furahiday, let it be an easy one. Tabasamu, na huna sababu ya kutoniita kwa jina langu
 
Kwema moudgulf kama upo mtwara msalimie Obe popote alipo, kama upo ukerewe msalimie leo dada, kama upo gamboshi salamu zangu mfikishie Seran

Na pia kama upo mabatini mwanza mjulie hali dosho12, kama ni mkwajuni hapo kino mjulie hali Atoto

Salamu zangu zingine zifikishe kwa win-one mwambie aache jeuri.
Nipo Mkomaindo hapa Masasi.
Kama kuna mdau hapa mshitue nikutane naye
 
Uzima na mauti upo kwenye vinywa venu😂😂 atakae tumia vizuri atakula matunda yake😂😂 no sio kapuku mimi nimekosea njia😂😂
 
Uzima na mauti upo kwenye vinywa venu😂😂 atakae tumia vizuri atakula matunda yake😂😂 no sio kapuku mimi nimekosea njia😂😂
 
Uzima na mauti upo kwenye vinywa venu😂😂 atakae tumia vizuri atakula matunda yake😂😂 no sio kapuku mimi nimekosea njia😂😂
...kama hujui unakokwenda, hukosei njia.
Hivi hivi vinywaa ambavo mchana vinasifu, kuabudu na usiku vinanyonya na kunyonyana. Kuzeeka hakukufanyi kuwa smart, kinafanya watu wakujue ujana wako ulikuwaje
 
Tofauti ya michembe na matobolwa na ile ya kuitwa mapalage ni ipi leo dada
Matobolwa ni viazi vinakatwa slace ndogo ndogo , vinachemshwa na kuanikwa. Vikikauka vinakuwa tayari kwa kuliwa.
Michembe ni viazi vinakatwa kat

Mkuu leo dada kumbe unapatikana kisiwani Ukerewe!!
Nitakutafuta kisiwani kwenu, niandalie Furu na Sato😎
Sawa sawa karibu sana
 
Back
Top Bottom