Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Vyombo vya Habari nchini Burundi, Gabby Bugaga amefariki dunia alfajiri ya Alhamisi Aprili 16, 2026.
Kiongozi huyo amekutwa akiwa amefariki ndani ya gari katika shamba la michikichi lililopo eneo la Kivoga, kaskazini mwa jiji la Bujumbura.

Picha zilizosambaa mitandaoni, ingawa hazijathibitishwa rasmi, zinaonyesha mtu anayedhaniwa kuwa ni Bugaga akiwa ameegemea usukani wa gari aina ya Toyota Pick Up, huku akivaa fulana ya mistari ya kijani na kaptura.

Gari hilo lilionekana kuharibiwa upande mmoja, hali iliyozua hisia kuwa huenda kulikuwa na ajali ya barabarani.
Aidha, mguu mmoja wa marehemu uliripotiwa kuwa nje ya mlango wa gari, jambo lililoongeza utata kuhusu tukio hilo.

Hata hivyo, mazingira ya kifo hicho bado hayajawekwa wazi, huku taarifa kutoka chombo cha habari cha Iwacu zikidai kuwa ufunguo wa gari hilo ulikutwa ndani ya begi badala ya kuwapo ndani ya gari, hali inayozua maswali zaidi kuhusu chanzo cha tukio hilo.

Msemaji wa Serikali ya Burundi, Jérôme Niyonzima, amethibitisha kuwa Bugaga amefariki kutokana na ajali, lakini hakutoa maelezo ya kina kuhusu ajali hiyo.

“Serikali inatoa pole kwa familia, ndugu, marafiki na wananchi wote walioguswa na msiba huu,” amesema Niyonzima, akimsifu Bugaga enzi za uhai wake kwa ujasiri na kujitolea kwake katika kulitumikia taifa hilo.

mwananchi_official-20260417-0006.jpg
 
“Kuhusu wachambuzi wanaoandika au kuongea habari zenye lengo la kuichafua Klabu ya Yanga, viongozi wanashughulikia jambo hilo na muda si mrefu nitawajuza hatua zitakazochukuliwa.”- Ally Kamwe, Afisa Habari Yanga SC
swahilitimes-20260418-0002.jpg
 
“Uongozi wa Young Africans Sports Club haujafanya mazungumzo na klabu au mtu yeyote kuhusu kumhitaji mchezaji Seleman Mwalimu. Hizi ni taarifa za uzushi na hazina ukweli wowote.” – Ally Kamwe, Afisa Habari Yanga SC
swahilitimes-20260418-0003.jpg
 
Klabu ya Mamelodi Sundowns imetinga fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuiondoa Espérance Sportive de Tunis kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-0 katika michezo ya nusu fainali.

Katika hatua ya fainali, Mamelodi itasubiri mshindi wa pambano kati ya AS FAR na RS Berkane, ambao wanatarajiwa kukutana leo saa 4:00 usiku.

Katika mchezo wa awali wa nusu fainali hiyo, AS FAR iliibuka na ushindi wa mabao 2-0, matokeo yanayowapa faida kuelekea mchezo wa marudiano dhidi ya Berkane.
mwananchi_official-20260418-0001.jpg
 
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra) imetangaza viwango vipya vya nauli kwa mabasi ya masafa marefu, mabasi ya mijini (daladala), teksi mtandao pamoja na pikipiki mtandao.

Tangazo hilo limetolewa jana Ijumaa Aprili 17, 2026 kupitia Gazeti la Serikali ambapo zitaanza kutumika siku 14 tangu kutangazwa rasmi kwa mujibu wa gazeti hilo.

Aidha, imeeleza kuwa marekebisho hayo yamefanywa kwa mujibu wa kifungu cha 19 cha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini, Sura ya 413, kinachoiruhusu LATRA kupanga na kurekebisha viwango vya nauli na tozo za huduma za usafiri.

Kwa mujibu wa jedwali lililotolewa, nauli za mabasi ya masafa marefu zimepangwa kulingana na daraja la basi na hali ya barabara. Kwa mabasi ya kawaida (ordinary), abiria atalipa Sh57.93 kwa kilometa moja katika barabara ya lami na Sh66.62 kwa barabara ya vumbi.

Kwa upande wa mabasi ya kati (semi-luxury), nauli kwa kilometa moja kwenye barabara ya lami ni Sh74.18.

Pia, mabasi ya mijini (daladala), viwango vipya vinaonyesha kuwa safari ya hadi kilomita 10 itagharimu Sh700, huku nauli ikiongezeka kulingana na umbali hadi kufikia Sh1,500 kwa safari ya kilomita 36 hadi 40.

mwananchi_official-20260418-0002.jpg
mwananchi_official-20260418-0003.jpg
 
Habari zenu wana Makapuku!

Nimecheka sana na stori zenu za namba na miamala, mko poa sana! Ni furaha kuona familia inakutana na kupata muda wa kucheka pamoja. Shunie , hata sisi tumekumiss magazeti yako, tunajua tu u busy!

Lakini pia, nikikumbuka madhumuni ya uzi huu, ni muhimu sana kuwa na sehemu kama hii ya kupeana moyo na kushare changamoto zetu. Maisha yana mambo mengi, na kuwa na jamii inayokuelewa na kukupa support ni baraka kubwa.

Kama kuna jambo lolote, tusisite kushare. Pamoja tunaweza kusaidiana na kupeana mbinu. Mimi nipo hapa pia kuunga mkono.

Karibuni sana wote!
Atoto Seran leo dada moudgulf Tresor Mandala Obe win-one makaveli10
Shwari mkuu.
Pamoja🤘
 
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmail Baghaei amesema Marekani haijaonyesha uzito katika kuanza duru mpya ya mazungumzo na Iran akisisitiza kuwa hali hiyo inaendelea kuwa kama mchezo badala ya juhudi za kujenga.

Akizungumza leo April 20, 2026, Baghaei ameongeza kuwa haitegemewi kwa Marekani kusema ukweli kwa madai kuwa mara kwa mara imekuwa ikiilaumu Iran bila msingi, huku akionyesha kutoridhishwa na mwenendo wa mazungumzo hayo.

Aidha, amesema inaonekana wazi kuwa Marekani haina nia ya dhati ya kushiriki mazungumzo hayo kwa umakini huku akibainisha kuwa Iran inaendelea kufuatilia kwa karibu hatua zinazochukuliwa na upande huo.

“Marekani haina uzito kuhusu mazungumzo mapya na Iran mchezo huu unaendelea badala ya wao kuchukua nafasi chanya lakini hatuwezi kutarajia Wamarekani kusema ukweli kwa sababu siku zote wanatulaumu sisi inaonekana wazi kuwa Marekani siyo makini kabisa”
millardayo-20260420-0001.jpg
 
Korea Kaskazini imesema imefanya jaribio jipya la kurusha makombora ya masafa mafupi yenye vichwa vya mabomu ya kusambaa ikiwa ni mara ya pili ndani ya mwezi huu kuendesha majaribio ya aina hiyo.

Kwa mujibu wa Shirika rasmi la Habari la KCNA majaribio hayo yamefanyika Jumapili Aprili 19, 2026 karibu na Pwani ya Mashariki ya Nchi hiyo ambapo Makombora yalirushwa yakielekezwa kwenye shabaha maalum baharini huku yakidaiwa kufanikiwa kulenga malengo yaliyokusudiwa.

Picha zilizotolewa na KCNA zimemuonyesha Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un akiwa ameambatana na binti yake anayedaiwa kuwa mrithi wake wakishuhudia zoezi hilo, huku Makombora matano aina ya Hwasong-11 Ra yakirushwa yakiwa na vichwa vya mabomu ya kusambaa pamoja na mabomu ya vipande ambapo Kim amesema majaribio hayo yamekuwa na umuhimu mkubwa katika kuimarisha uwezo wa mashambulizi yenye nguvu na msongamano mkubwa.

Mabomu ya kusambaa hutoa vipande vidogo vinavyosambaa katika eneo kubwa na kufanya kuwa vigumu kuyadhibiti ambapo zaidi ya Nchi 120 zimesaini mkataba wa kuyapiga marufuku ingawa Korea Kaskazini haijajiunga na makubaliano hayo, huku majaribio haya yakiendelea kufanyika katika kipindi ambacho mvutano wa kisiasa na Kijeshi unaendelea kuongezeka katika maeneo mbalimbali duniani ikiwemo Mashariki ya Kati hali inayozua wasiwasi zaidi kuhusu usalama wa kimataifa
millardayo-20260420-0002.jpg
 
Mwanaume mmoja amewaua Watoto wanane na kuwajeruhi Watu wawili wazima katika shambulio la risasi lililotokea katika Mji wa Shreveport, Nchini Marekani, ambapo Polisi Nchini humo wamesema tukio hilo linahusiana na mgogoro wa kifamilia.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Polisi, Chris Bordelon, Mshukiwa anayetambulika kwa jina la Shamar Elkins amewaua Watoto wake saba pamoja na Mtoto mwingine mmoja, na kumjeruhi mama wa Watoto hao pamoja na Mwanamke mwingine, Watoto waliouawa wana umri wa kati ya mwaka mmoja hadi miaka 12, huku majeruhi wakiripotiwa kuwa katika hali mbaya.

Aidha, Polisi wameeleza kuwa tukio hilo limetokea katika maeneo manne tofauti ndani ya kitongoji cha Cedar Grove, hali inayoonyesha ukubwa wa shambulio hilo, na baada ya uhalifu huo, Mshukiwa alikimbia na kuhusika katika utekaji wa gari kabla ya kuuawa kwa kupigwa risasi na Polisi wakati wa msako.

Pamoja na hayo, Mkuu wa Polisi, Wayne Smith, amethibitisha kuwa Mshukiwa alikuwa na historia ya kukamatwa mwaka 2019 kwa kosa la silaha, huku Viongozi mbalimbali wakilaani tukio hilo, akiwemo Meya wa Mji huo, Tom Arceneaux, ambaye amelitaja kuwa ni janga kubwa kwa jamii, Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Mike Johnson, naye amesema tukio hilo ni la kuhuzunisha na amewataka Wananchi kuwaombea waathirika na familia zao katika kipindi hiki kigumu.
millardayo-20260420-0003.jpg
millardayo-20260420-0004.jpg
millardayo-20260420-0005.jpg
 
Mwandishi wa habari mkongwe nchini Uganda ameuawa kwa kupigwa risasi alipokuwa karibu na nyumba yake huko Kawanda, Wilaya ya Wakiso katika Mji Mkuu wa Kampala, hayo yameelezwa Jumapili na Polisi.

Joe Nam, mwenye umri wa miaka 55, alifanya kazi katika Vyombo vya Habari vya Serikali kwa miongo mitatu kabla ya kustaafu na aliandika kitabu kinachozungumzia matokeo yanayoweza kushuhudiwa Uganda pale Rais Yoweri Museveni aliyetawala nchi hiyo kwa muda mrefu atakapoondoka madarakani.

Naibu msemaji wa Polisi Luke Owoyesigyire amesema uchunguzi unaendelea lakini ule wa awali umebainisha kuwa Joe Nam aliuawa usiku wa kuamkia jana Jumapili na mtu aliyekuwa ameficha uso wake na kwamba mshambuliaji huyo alifanikiwa kuondoka eneo la tukio.

millardayo-20260420-0006.jpg
 
Serikali ya Iran imesema haina mpango wowote wa kuhudhuria mazungumzo mapya ya amani na Marekani yanayotarajiwa kufanyika kuanzia leo April 20, 2026, Mjini Islamabad.

Hii ni baada ya Rais wa Marekani, Donald Trump kusema kuwa amewatuma Nchini Pakistan Wawakilishi wake wakiongozwa na Makamu wa Rais JD Vance kuendelea na majadiliano ya kumaliza vita, huku akitishia kuishambulia Iran ikiwa haitakubali masharti yake.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la Iran IRNA limeandika kuwa Iran imesusia duru hiyo ya pili ya mazungumzo kutokana na masharti makubwa na yasiyotekelezeka ya Marekani pamoja na hatua yake ya kubadili msimamo kila wakati na kuendeleza vizuizi katika Bandari zake, mambo iliyosema kuwa ni uvunjaji wa wazi wa makubaliano ya kusitisha mapigano.

Hayo yanajiri wakati Trump akisema kuwa Jeshi la Marekani limeshambulia meli ya mizigo ya Iran katika Ghuba ya Oman na kwamba kwa sasa wanaidhibiti Meli hiyo inayofahamika kama Touska ambayo ilijaribu kukiuka vizuizi vya majini vilivyowekwa na Marekani. Iran imesema itajibu haraka shambulio hilo.


millardayo-20260420-0007.jpg
 
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limesema picha mjongeo inayosambaa mitandaoni ikidai kichwa cha treni ya SGR kinatoa mlio usio wa kawaida ni uzushi.

TRC imesema treni zote za SGR zinafanya kazi kwa ufanisi na ziko katika hali ya usalama.
swahilitimes-20260420-0001.jpg
 
“Kwa mujibu wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2021, vijana wameendelea kukabiliwa na ukosefu wa ajira kwa asilimia 12.2 (wanaume asilimia 8.1 na wanawake asilimia 16.1).” - Joel Nanauka, Waziri wa Maendeleo ya Vijana akiwasilisha bungeni Bajeti ya mwaka 2026/27
swahilitimes-20260420-0002.jpg
 
“Kwa mujibu wa Utafiti wa Nguvu Kazi wa Mwaka 2020/21, vijana wanachangia zaidi ya asilimia 55 ya nguvu kazi ya Taifa. Takwimu hizi zinaonesha wazi kuwa vijana ndio sehemu kubwa zaidi ya nguvu kazi inayoshiriki katika shughuli za kiuchumi nchini.” – Joel Nanauka, Waziri wa Maendeleo ya Vijana akiwasilisha bungeni Bajeti ya mwaka 2026/27
swahilitimes-20260420-0003.jpg
 
Iran imeshambulia meli za Marekani nchini Oman, ikiwa ni kulipiza kisasi baada ya Marekani kukamata meli ya mizigo iliyokuwa na bendera ya Iran.

Iran imesema kitendo cha Marekani ni ukiukwaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano.
swahilitimes-20260420-0004.jpg
 
Back
Top Bottom