Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mahakama Kuu ya Kanda ya Morogoro imewahukumu kifungo cha maisha washtakiwa wanne kwa kusafirisha bangi (viroba 16).

Waliotiwa hatiani ni Silvanus Julius, (49) mkazi wa Tambuka Reli - Mikumi, Joyce Gidion (49) mkazi wa Yombo Vituka Dar es Salaam, Sophia Samweli (45) mkazi wa Mogo - Mikumi na Frolian Magoha, (36) mkazi wa Idege -Mikumi.
swahilitimes-20260325-0003.jpg
 
Mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah, amefikia makubaliano na klabu hiyo ya kuondoka mwishoni mwa msimu huu.

Salah ameisaidia Liverpool kutwaa mataji mbalimbali ikiwemo Ligi Kuu Uingereza, UEFA Champions League, Kombe la Dunia la Klabu, UEFA Super Cup na FA Cup. Hadi sasa ameifungia klabu hiyo mabao 255 katika mechi 435, akishika nafasi ya tatu katika orodha ya wafungaji bora wa muda wote wa Liverpool.
swahilitimes-20260325-0004.jpg
 
Wachezaji Simon Msuva, Yusuf Kagoma na Abdullah Bacca hawajaungana na kikosi cha Taifa Stars kuelekea Kigali, Rwanda kwa ajili ya mashindano ya FIFA Series 2026.

TFF imesema Msuva ameshindwa kujiunga na timu kutokana na changamoto za usafiri, huku Bacca na Kagoma wakikosa nafasi hiyo kutokana na majeraha.
swahilitimes-20260325-0005.jpg
 
Mahakama Kuu ya Kanda ya Morogoro imewahukumu kifungo cha maisha washtakiwa wanne kwa kusafirisha bangi (viroba 16).

Waliotiwa hatiani ni Silvanus Julius, (49) mkazi wa Tambuka Reli - Mikumi, Joyce Gidion (49) mkazi wa Yombo Vituka Dar es Salaam, Sophia Samweli (45) mkazi wa Mogo - Mikumi na Frolian Magoha, (36) mkazi wa Idege -Mikumi.View attachment 3562629
Kusafirisha bangi hukumu ni kifungo cha maisha!
Wakate rufaa kwa kweli .
 
Kuanzia mwaka 2021, Jeshi la Indonesia na Jeshi la Polisi walitangaza rasmi kukomesha utaratibu wa vipimo vya bikira.

Kabla ya hapo, jeshi na polisi nchini Indonesia waliamini kuwa:

- Bikira ilikuwa ishara ya "maadili mema" ya mwanamke.

- Waliona kuwa mwanamke ambaye si bikira ameshapoteza sifa ya kiroho na kimaadili ya kulitumikia taifa.

Utaratibu huo uliitwa "Two-Finger Test" na ulikuwa unakosolewa vikali na mashirika ya kutetea haki za binadamu kama Human Rights Watch na WHO, wakisema ni udhalilishaji na hauna uhalali wowote wa kisayansi.
Screenshot_20260325_164326_Gallery.jpg
 
Kundi la mbwa mwitu ni familia: wazazi ndio viongozi, na watoto wao huishi pamoja.

Mbwa mwitu hushirikiana kama familia, wanawinda, kulea watoto, na kulinda eneo lao kwa ushirikiano, na si kwa kupigana.

Wazo la “alpha” lilitokana na tafiti za zamani kwa mbwa mwitu waliowekwa pamoja bila uhusiano, jambo lililosababisha mapigano makali sana.

Kutumia mfano wa “alpha” kwa binadamu pia ni makosa, kwa sababu maisha ya watu yanategemea ushirikiano na siyo ubabe.
Screenshot_20260325_164758_InstaPro%20.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom