Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mara baada ya kumpigia simu mkewe, María Isabel Santos Caballero—Mwamba “Pablo Escobar” alikamatwa na huo ndo ulikuwa mwisho wake.

The Drug Lord “El Chapo” naye alikamatwa mara tu baada ya kufanya mawasiliano na Manzi yake “Kate De Castillo”

Star Boi “El Mencho” akiwa kwenye mjengo wake huko Tapalpa (Jalisco) nchini Mexico,

Lokesheni yake ilitambulika mara tu baada ya kufanya mawasiliano na bebe yake “Guadalupe Moreno Carrillo”

Alivamiwa na kikosi maalumu cha jeshi la Mexico, na kuuawa.

Wahuni waliwalinda sana MaBosi zao, tena kwa uaminifu wa hali ya juu bila ya USNITCHI wowote ule.

Maanguko yao yametokea vilevile kama ilivyokuwa kwa Babu yetu Adamu (EVA) au Mzee wetu Samsoni (DELILA).

siasamakini-20260225-0001.jpg
 
Mara baada ya kumpigia simu mkewe, María Isabel Santos Caballero—Mwamba “Pablo Escobar” alikamatwa na huo ndo ulikuwa mwisho wake.

The Drug Lord “El Chapo” naye alikamatwa mara tu baada ya kufanya mawasiliano na Manzi yake “Kate De Castillo”

Star Boi “El Mencho” akiwa kwenye mjengo wake huko Tapalpa (Jalisco) nchini Mexico,

Lokesheni yake ilitambulika mara tu baada ya kufanya mawasiliano na bebe yake “Guadalupe Moreno Carrillo”

Alivamiwa na kikosi maalumu cha jeshi la Mexico, na kuuawa.

Wahuni waliwalinda sana MaBosi zao, tena kwa uaminifu wa hali ya juu bila ya USNITCHI wowote ule.

Maanguko yao yametokea vilevile kama ilivyokuwa kwa Babu yetu Adamu (EVA) au Mzee wetu Samsoni (DELILA).

View attachment 3548347
Seran hiki kipande asikione Natafuta ajira 😄
 
“El Mencho” amezikwa rasmi kwenye makaburi yaliyopo katika mji wa Zapopan pale kwenye mtaa wa Guadalajara.

Chini ya ulinzi mkali wa MANJAGU waliokuwa na silaha nzito za moto, jeneza la dhahabu lilishushwa huku likipambwa na mashada makubwa ya maua.

Wahuni kibao walijitokeza kumzika “Star wa Mchezo” huku tukio kubwa la kuvutia ni kuonekana kwa mtoto wake wa kike ambaye kwa miaka mingi amekuwa akitafutwa na jeshi la Mexico.

Unaambiwa kwamba,

Binti wa El Mencho “Laisha Michelle Nemesio Oseguera González” amekuwa kwenye maseke ya kutafutwa na MAPOTI kutokana na mishe za kuuza poda.

Kwa miaka mingi, amekuwa “WANTED” lakini jana kwenye mazishi ya baba yake, amejitokeza hadharani huku MAPOTI wakimtazama bila ya kufanya lolote (Tazama Slide ya 3)

Wahuni siyo watu wazuri, laiti kama wangejitikisa tu na kuleta utoto, basi moto ungewaka hapo hapo msibani.

Usilolijua ni kwamba, harakati zote za mazishi hayo zilisimamiwa na Kiongozi mpya wa Genge la Jalisco New Generation Cartel (CJNG)

Siyo mwingine bali ni Juan Carlos Valencia González maarufu kama “03” au “El Pelón” ambaye ni mtoto wa kambo wa “El Mencho” Namba chafu kabisa.

Mama yake, ambaye ndo alikuwa mke wa “El Mencho” anaitwa Rosalinda González. Pale mitaa ya Mexico wanamtambua kama “La Jefa” yaani “The Boss”

Yaani Baba Mhuni, Mama Ngoma Nagwa, halafu Mtoto ndo Mhuni zaidi ya wazazi wake
siasamakini-20260304-0001.jpg
siasamakini-20260304-0002.jpg
siasamakini-20260304-0004.jpg
siasamakini-20260304-0003.jpg
siasamakini-20260304-0006.jpg
siasamakini-20260304-0005.jpg
 
Heri ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani.

Wanawake wote mlio ndani humu, ninyi ni sababu jukwaa hili halipoi. Give to Gain ndo theme ya mwaka huu
 
Eid Mubarak wadau wote wa jukwaa hili.
Wote tuliomaliza salama funga zetu basi na tulipwe sawia. Na wote watu wema tulipwe kama inavyostahili.

Mtakie kheri kila unayekutana naye, na kwa mtu wako nyumbani, mkumbatie ajue wewe ni mtu sahihi
 
Jeshi la Magereza limesema Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu yuko salama na afya yake ni njema.

Jeshi hilo limekanusha taarifa zinazosambaa kwenye baadhi ya vyombo vya habari zikidai kuwa hali ya Lissu ni mbaya, likisisitiza kuwa taarifa hizo zinalenga kuleta taharuki katika jamii.
swahilitimes-20260325-0001.jpg
 
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema ameshtushwa na kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), William Lukuvi kwani walizungumza jana na kupanga mkutano.
Screenshot_20260325_163531_InstaPro%20.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema taifa limepoteza kiongozi shupavu, mwenye uzoefu mkubwa na mzalendo kufuatia kifo cha William Lukuvi, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, kilichotokea leo jijini Dodoma.

Rais pia ametuma salamu za pole kwa Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, familia ya marehemu, wananchi wa Isimani pamoja na Watanzania wote, akisisitiza kuwa mchango wake utaendelea kukumbukwa.
swahilitimes-20260325-0002.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom