Serikali imesema kuendelea kuuza korosho ghafi nje ni kupeleka ajira nje Watanzania, utajiri wa Wakulima na mapato ya Tanzani, hivyo ifikapo mwaka 2026/2027 korosho zote zinazozalishwa nchini zitabanguliwa hapahapa Tanzania na kuondokana na kuuza korosho ghafi nje ya Nchi.
“Kuendelea kuuza korosho ghafi nje ni kupeleka ajira zetu, utajiri wa wakulima wetu na mapato ya nchi yetu, hili hatuwezi kulikubali na lazima lifike mwisho ifikapo mwaka 2026/2027, ni lazima tuhakikishe zaidi ya tani 300,000 zinabanguliwa nchini kwa mwaka ikiwa ni pamoja na kukamua maganda ya korosho hizo”
Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde @anthonymavunde amesema hayo alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho mwaka 2023 “Dhamira na shabaha ya Serikali yetu chini ya uongozi mahiri wa Mh. Dkt.Samia Suluhu Hassan, ni kuhakikisha zao la korosho linachangia kuongeza ajira na kipato kwa wakulima kupitia uongezaji wa thamani
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mariam Ditopile @mariam_ditopile amesema juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kilimo zinaonyesha utayari wake kuiletea maendeleo Sekta ambapo ametaja moja ya maeneo ambayo Rais Samia ameweka nguvu ni kuongeza Bajeti ya kilimo kila mwaka.