Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mkazi wa Kijiji cha Miule wilayani Tandahimba, amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 20 jela, baada ya patikana na hatia ya kukutwa na kucha za mnyama ajulikanaye kwa jina la Mhanga.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo, amesema kuwa, kesi hiyo ni kati ya kesi 76 zilizofikishwa katika mahakama mbalimbali na kutolewa hukumu.

“Yusuph Stephen Mkwemba (42) alikutwa na kucha hizo ambazo ni nyara za Serikali nyumbani kwake, zenye thamani ya Sh1.52 milioni. Mahakama imemtia hatiani na kumfunga kwa kuwa ni kosa kisheria kuwa na nyara hizo,” amesema.

(Imeandikwa na Florence Sanawa)
Screenshot_20230721_050927_Instagram.jpg
 
Wanasheria waliofungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya kupinga makubaliano ya ushirikiano wa kiuchumi baina ya Serikali za Tanzania na Dubai, yanayohusisha uwekezaji katika bandari ya Dar es Salaam, wameondoa shauri lao la maombi madogo ya kusimamishwa utekelezaji wa makubaliano hayo.

Wanasheria hao Alphonce Lusako, Emmanuel Kalikenya Changula, Raphael Japhet Ngonde na Frank John Nyalusi, walifungua kesi hiyo chini ya hati ya dharura wakipinga masharti ya baadhi ya ibara za makubaliano hayo.

Pamoja na kesi hiyo, pia wamefungua shauri dogo, wakiiomba mahakama hiyo itoe amri ya maelekezo kwa wadaiwa (Serikali) kusimamisha utekelezaji wa makubaliano hayo, kusubiri kumalizika kwa kesi ya msingi.

Hata hivyo kiongozi wa jopo la mawakili wa upande wa madai, Boniface Mwabukusi, amesema leo Alhamis Julai 20,2023 kuwa wameamua kuyaondoa maombi hayo baada ya kujadiliana na wateja wao ili kuiwezesha kesi ya msingi kusikilizwa na kuamuriwa haraka na kufuatia ushauri wa majaji wanaoisikiliza kesi hiyo.

(Imeandikwa na James Magai na Hawa Mathias)
Screenshot_20230721_051045_Instagram.jpg
 
| Timu ya Kaizer Chiefs imetua nchini leo alfajiri Ijumaa ikiwa na msafara wa watu 28 kwa ajili ya mechi yake ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Yanga, Julai 22 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika Kilele cha Wiki ya Mwananchi.
Screenshot_20230721_051226_Instagram.jpg
 
OFFICIAL & CONFIRMED:
.
Klabu ya Simba imethibitisha kukamilisha usajili wa beki HUSSEIN KAZI kwa Mkataba wa miaka miwili.
.
Hussein amecheza soka la kulipwa nchini Shelisheli kabla ya kujiunga na Mbeya Kwanza, Polisi TZ na Geita Gold.
Screenshot_20230721_051358_Instagram.jpg
 
OFFICIAL & CONFIRMED:
Klabu ya Simba imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo mkabaji ABDALLAH HAMIS akiwa mchezaji huru kwa Mkataba wa miaka miwili.
Screenshot_20230721_051506_Instagram.jpg
 
OFFICIAL & CONFIRMED:
Klabu ya Simba imethibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji SHABANI IDD CHILUNDA akiwa mchezaji huru kwa Mkataba wa miaka miwili.
Screenshot_20230721_051619_Instagram.jpg
 
Timu mbili [2] kutoka Magnet Academy zimeendelea kufanya vizuri katika mashindano maarufu zaidi ya vijana duniani ‘Gothia Cup’ huko nchini Sweden.

Timu hizo za Umri wa miaka 14 na 16 zimemaliza vinara katika hatua ya makundi. Magnet Academy wamecheza na timu mbalimbali ta kutoka Sweden, Ujerumani, Italia na Ugiriki.

Mashindano hayo hufanyika mara moja kila mwaka na kuhusisha timu zaidi ya 1800 kutoka mataifa zaidi ya 65.

Akiongea kutoka Sweden, Mkurugenzi wa Ufundi wa Magnet Academy Mkufunzi na Kocha Bw. Wane Mkisi anasema maendeleo ni mazuri sana na anaona mabadiliko chanya kila mwaka.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Magnet Academy Tuntu Mwambusi ameendeleea kuwashukuru watanzania walioko jiji la Gothenburg, Sweden kwa ushirikiano wao mkubwa.

Mmoja wa watanzania amenukuliwa akisema: “Tunafarijika sana na mpira wanaouonyesha vijana na hii inatufanya tuache kazi zetu na kuja kuona hii burudani. Vijana wanapambana sana na tunaomba serikali na wadau kuwapa support Magnet.”
Screenshot_20230721_051829_Instagram.jpg
 
Tuliamua kutengeneza thamani kwenye kipindi hiki cha dirisha kubwa la usajili, hapo ndipo likazaliwa wazo la kuichukua jezi namba 6 na kuifanyia promotion. Thamani yake ikapanda na watu wakaanza kuizungumza.

Halafu tukatengeneza uhitaji mkubwa kwenye usajili wetu, watu wakaanza kusema mbona Yanga hawasajili? Wengine wakasema Yanga wamefungiwa kusajili, wapo waliosema Yanga hawana hela!

Habari zikawa nyingi sana, kwa sisi tunaofahamu biashara tukaona uhitaji wa watu kujua kuhusu usajili wa Yanga ni mkubwa sana.

Baada ya hapo tukawatafuta CRDB Bank, tukavuta kibunda CRDB Bank ikiwa mdhamini wa video za kutambulisha wachezaji. Yanga ikawa klabu ya kwanza kunufaika na kutambulisha wachezaji.

- Ali Kamwe, Ofisa Habari Yanga.
Screenshot_20230721_052310_Instagram.jpg
 
WANANCHI 2023 Jumamosi hii imewekwa kwenye daftari la ‘hatari’ ya burudani na Afisa Usalama wa soka, Wananchi wenye hasira kali na mafanikio watajitokeza ‘kumzika’ Mwizi wao Kaizer Chiefs kutoka Kusini kwa Madiba Mandela.

Daftari la mahudhurio la Mwalimu wa Darasa la soka linasema kila ambaye anafahamu ni Mwanafunzi wa Yanga University basi awahi namba, ahakikishe mstari umenyooka na uniform yake ni safi usanifu wa Sheria Ngowi, asiyekuwepo atakuwa amenajisi maana halisi ya Class of 2023, ndio kwanza msimu unaanza.

Aseme nini Afisa Usalama barabarani wa soka? Ni hakika kila Mtumiaji wa barabara ya Ligi Kuu anataka amshuhudie Dereva Mkuu amejipangaje? Ni hakika Djigui Diarra atasema Abnormal Wide Load na wengine mpishe mbali nawaambia, mweleko ni Lupaso ama kwa Mkapa kwakuwa ndio njia pekee ipo wazi siku hiyo.

Let SKUDU dance, MVP wa Ivory Coast atakaribishwa, DJ AllyB ataburudisha nani wewe usiwe sehemu ya historia!? Uvamizi wa burudani ya soka, ulevi wa soka safi la Garmondi na starehe kali ni WANANCHI DAY, kata tiketi yako
Screenshot_20230721_052417_Instagram.jpg
 
Ali Kamwe amefafanua na kutoa jibu kwa wote wanaohoji kwa imekuaje winga [Skudu] apewe jezi namba sita [6] ambayo mara nyingi huvaliwa na viungo wa katikati.

Roberto Carlos amewahi kuvaa jezi namba 6 wakati anacheza kama mlinzi wa kushoto, William Gallas alivaa jezi namba 10 akiwa Arsenal kwa hiyo zamani jezi zilivaliwa kutokana na nafasi ya mchezaji uwanjani. Sasa hivi mambo yamebadilika.

Siku hizi namba za jezi zinaweza kuvaliwa kutokana na vitu vingi, tarehe ya kuzaliwa, tarehe ya ndoa n.k. Kuna wachezaji wanavaa namba ya jezi ili kuenzi vitu/kumbukumbu zao katika maisha.

- Ali Kamwe, Ofisa Habari Yanga.
Screenshot_20230721_052727_Instagram.jpg
 
Yanga tumeongeza Wizara ambayo inakuja kungana na zilizopo, msimu uliopita tulikuwa na Wizara ya Ulinzi ambayo kuna wakati ilikuwa Mawaziri watatu Mwamnyeto, Job na Baka ikatupeleka hadi Fainali ya Kombe la Shirikisho.

Kushoto kuna Wizara ya Maji, Joyce Lomalisa akawa anafanya kazi yake vizuri wananchi wakawa wanapata maji inavyostahili kupatikana.

Msimu huu tumeamua kutambulisha Wizara mpya, Wizara ya Raha. Wizara hiyo inahusika na raha tu, tukamtafuta Waziri wa kusimamia Wizara hiyo ambaye ni Skudu.

- Ali Kamwe, Ofisa Habari Yanga.
Screenshot_20230721_052844_Instagram.jpg
 
Mshambuliaji wa zamani wa Azam FC Shabani Iddy Chilunda amesaini kandarasi ya miaka miwili na Simba SC hadi 2025 .

Chilunda amejiunga na Simba baada ya kumalizana na Azam FC hivyo amesajiliwa akiwa huru (free agent)
Screenshot_20230721_053234_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom