Makapuku Forum

Makapuku Forum

OFFICIAL & CONFIRMED:
.
Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo fundi ZOUZOUA PACOME (26) kutoka Asec kwa Mkataba wa miaka miwili.
.
Pacome ni kiungo mshambuliaji, Ndiye MVP wa Ligi Kuu ya Ivory coast ni mchezaji mkubwa mwenye thamani kubwa.
Screenshot_20230720_054208_Instagram.jpg
 
NEWCASTLE United ipo kwenye hatua za mwisho kukamilisha dili la winga wa Leicester City, Harvey Barnes na ikiwa dili hilo litakamilika Newcastle ndio itakubali kumuuza mshambuliaji Allan Saint-Maximin, 26, anayehitajika na Al Hilal ya Saudi Arabia.
.
Al-Hilal inadaiwa kuwa tayari kutoa Euro 25 milioni ili kuipata huduma ya Saint-Maximin ambaye ameitaka Newcatle ikubali kumuachia kutokana na ofa nono aliyowekewa mezani.
Screenshot_20230720_081847_Instagram.jpg
 
LIVERPOOL haina mpango wa kukubali ofa ya Euro 50 milioni kutoka Al-Hilal ya Saudi Arabia ili kuwauzia mshambuliaji Luis Diaz, 26, katika dirisha hili la usajili wa majira ya joto huko Ulaya.
.
Mabosi wa Liverpool hawataki kumuuza mchezaji huyu wa kimataifa wa Colombia kwa sababu bado yupo kwenye mipango ya kocha wa sasa, Jurgen Klopp. Diaz alitumikia sehemu ya msimu uliopita akiwa majeruhi.
Screenshot_20230720_081959_Instagram.jpg
 
ARSENAL haijamaliza na sasa inapiga hesabu za kuvamia tena Ajax kumnasa staa wa Pauni 40 milioni Mohammed Kudus, lakini shida italazimika kuuza wachezaji saba kwanza.
.
Mkurugenzi wa michezo, Edu ni lazima aondoe watu kwenye kikosi ili kupunguza bili ya mishahara na jambo hilo linawahusu wachezaji saba kuna uwezekano wa kufunguliwa mlango wa kutokea ambao ni Kieran Tierney, Cedric Soares, Nicolas Pepe, Albert Lokonga, Nuno Tavares na Rob Holding.Kiungo, Thomas Partey naye anahusishwa na mpango wa kuondoka kwenye timu hiyo na ada yake inaweza kuwa Pauni 30 milioni.
Screenshot_20230720_082045_Instagram.jpg
 
Manchester City imeripotiwa kuwekewa mezani ofa ya wachezaji watatu wa kiwango cha dunia na miamba ya soka Paris Saint Germain ili tu wao wamchukue Bernardo Silva. Mabingwa hao wa mataji matatu makubwa ya msimu uliopita, Man City wapo kwenye wakati mgumu wa kumbakiza kiungo huyo mchezeshaji dirisha hili la usajili wa majira ya kiangazi.
.
Kwa mujibu wa Foot Mercato, wakala Mreno Jorge Mendes anafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha Silva anang’oka Etihad na kwenye hilo kuna majina ya mastaa watatu wanaweza kuhusika akiwamo kipa Gianluigi Donnarumma, kiungo Marco Verratti na beki Presnel Kimpembe.
Screenshot_20230720_082135_Instagram.jpg
 
MMESIKIA hii? Mauricio Pochettino ameishtua bodi ya wakurugenzi wa Chelsea baada ya kuwaambia: “Nataka wachezaji.”
.
Na licha ya kutumia Pauni 600 milioni kwenye usajili wa mastaa wapya katika madirisha mawili ya usajili, mmiliki wa The Blues, Todd Boehly ameambiwa wanahitajika wachezaji zaidi ili kuja kuboresha kikosi na kuwa cha kibabe:
.
Pochettinho alisema: “Nahitaji wachezaji sahihi kuletwa kwenye kikosi. Hilo linatakiwa kufanyika haraka. Leo ni bora kuliko kesho. Tunahitaji kufanya kazi kwelikweli kwenye kunasa mastaa tunaowahitaji. Tunahitaji vijana wenye njaa.“Ni changamoto. Tuna uhakika tutatengeneza kikosi kizuri kitakachokuwa tayari kushindana kwenye Ligi Kuu England.
Screenshot_20230720_082226_Instagram.jpg
 
EDWIN van der Sar anawashukuru mashabiki kwa dua na sapoti na kuwaambia kwa sasa hayupo tena wodi ya wagonjwa mahututi.
.
Gwiji huyo wa Manchester United na Ajax bado yupo hospitali baada ya kukumbwa na tatizo la damu kuvuja kwenye ubongo alipokuwa mapumziko Croatia.
.
Aliweka na ujumbe uliosomeka: “Kwanza kabisa, tunapenda kuwashukuru wote kwa maoni na meseji zetu za sapoti. Nafurahi kuwaambia kwamba sipo tena kwenye chumba cha wagonjwa mahututi. Hata hivyo, bado nipo hospitali. Natumaini nitaruhusiwa kwenda nyumbani wiki ijayo na kwenda kupambana na hatua nyingine ya kupona.”
Screenshot_20230720_082328_Instagram.jpg
 
SRAIKA Kylian Mbappe jana Jumanne aliripotiwa kuwa na kikao maalumu na rais wa Paris Saint-Ger-main, Nasser Al-Khelaifi kujadili hatima yake.

Rais wa PSG Al-Khelaifi alikiri kushtushwa na uamuzi wa mshambuliaji huyo kwamba hawezi kubaki kwenye timu hiyo hadi 2025. Kutokana na hilo, PSG ilimpa Mbappe wiki mbili za kuamua kama anabaki Parc des Princes kwa maana ya kusaini mkataba mpya la basi auzwe kwenye dirisha hili hili la uhamisho wa majira ya kiangazi. Hivyo, Mbappe na Al-Khelaifi walitarajia kukutana jana ana kwa ana ana kwa ajili ya mazungumzo na kuwekana wazi juu ya hatima ya kila upande klabuni hapo.

Kuna ripoti zilidai kwamba Mbappe atakwenda kuambiwa hadi kufikia Julai 31 atatakiwa aweke wazi msimamo wake kama atabaki PSG hadi 2025 au milango ifunguliwe ya kupokea ofa ya kupiga bei mwaka huu. Real Madrid bado wanapewa nafasi kubwa ya kunasa saini yake, lakini miamba hiyo ya Bernabeu inaelezwa kwamba haina pesa za kugharimia uhamisho wake baada ya kumtumia mkwanja mrefu kwenye dirisha hili kunasa huduma ya kiungo Jude Bellingham kutoka Borussia Dortmund.

Kutokana na hilo, timu za Ligi Kuu England zinaweza kuingia kwenye mchakato wa kunasa saini yake ikiwamo Manchester United, Arsenal na Liverpool abazo zote zimeripotiwa kufuatilia kwa karibu mchakato huo.

Screenshot_20230720_082423_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom