Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230718_064213_Opera%20Mini.jpg
 
STAA wa zamani wa Ligi Kuu England ambaye ni shabiki mnazi wa Arsenal, Darren Bent amemwambia kocha Mikel Arteta ampige benchi Kai Havertz na badala yake aendelee kumpa nafasi kikosini kiungo Thomas Partey
.
Bent alisema: “Nitamwanzisha Thomas Partey. Partey, Rice, Odegaard hiyo ni kombinesheni safi kwenye kiungo. Mpe Rice uhuru wa kwenda mbele zaidi. Shabiki mmoja alijibu na kuuliza ni wapi Havertz atacheza, Bent alijibu: “Hachezi.”
.
Itakuwa sapraiz kubwa kwa mashabiki kama wataona Havertz haanzi kwenye kikosi licha ya kusajiliwa kwa Pauni 65 milioni kutokea Chelsea. Arsenal itakipiga na JITU KATILI Manchester City kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii utaochezwa Agosti 6 uwanjani Wembley.
Screenshot_20230718_065153_Instagram.jpg
 
Habari ndo hiyo. Marcus Rashford anajiandaa kusaini mkataba wa miaka mitano Manchester United. Iliwahi kuripotiwa huko nyuma Rashford atakuwa mmoja wa mastaa watakaokuwa wanalipwa mkwanja mrefu huko Old Trafford na sasa yametimia baada ya kupewa ofa ya mshahara wa Pauni 375,000 (Sh 1.2bilioni) kwa wiki ili abaki Man United.
.
Na sasa imewekwa wazi mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England ataongeza miaka mitano ya kuendelea kukipiga kwenye kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mdachi, Erik ten Hag. Rashford, 25, anaingia kwenye mwaka wa mwisho kwa mkataba wake wa sasa, lakini atasaini dili jipya baada ya maboresho makubwa kwenye malipo ambapo mshahara wake utaongezeka kutoka kwenye kiwango cha Pauni 200,00 kwa wiki anacholipwa kwa sasa.
Screenshot_20230718_065242_Instagram.jpg
 
OFFICIAL: Uongozi wa klabu ya Yanga umemtangaza, Taibi Lagrouni kuwa Kocha wa viungo wa timu hiyo. Mtaalamu huyo kutoka Morocco amejiunga na timu hiyo akichukua nafasi ya Helmy Gueldich kipenzi cha mashabiki wa Yanga.
Screenshot_20230718_065349_Instagram.jpg
 
JUVENTUS inapambana kuipata huduma ya kiungo wa Barcelona, Franck Kessie katika dirisha hili ili akazibe pengo la Paul Pogba ambaye huenda akaondoka.
.
Kessie ambaye amekuwa akitajwaa kuwa ataondoka Barca kwa sababu hapati nafasi ya kutosha kuonyesha uwezo wake uwanjani, tangu ajiunge nayo katika dirisha lililopita la majira ya kiangazi.
Screenshot_20230718_065446_Instagram.jpg
 
West Ham inaangalia uwezekano wa kuwasilisha ofa Manchester United ili kuipata huduma ya beki wa kati na kapteni wa timu hiyo Harry Maguire, 30, kwa mkopo katika dirisha hili.
.
Maguire ni miongoni mwa mastaa wanaohusishwa kuondoka Man United kwa ajili ya kutafuta changamoto mpya lakini timu nyingi zinaonekana kushindwa kumnunua kutokana na kiasi kinachohitajika na Man United kuwa kikubwa.
Screenshot_20230718_065538_Instagram.jpg
 
Straika wa Chelsea Pierre Emerick Aubameyang anadaiwa kuwa tayari kujiunga na Marseille katika dirisha hili na amekubali hadi kushusha mshahara wake ili kufanya dili hilo litokee.
.
Mojawapo ya sababu zinazotajwa kumfanya Aubameyang ashawishike kukubali ofa hiyo ni kutaka kurejea Ufaransa mahali ambako amezaliwa ingawaje anaitumikia timu ya Taifa ya Gabon.
Screenshot_20230718_065624_Instagram.jpg
 
“Sikupata nafasi ya kucheza kama nilivyotaka miaka yote niliokuwepo Chelsea, sikufikia kiwango cha soka ambacho nilitaka, kuna wakati nilikuwa natamani sana nipate nafasi za kucheza, kwasababu yoyote ile haijalishi, kama nilivyosema, nimefurahi kujiunga na AC Milan, nipo tayari kwa changamoto mpya.” Christian Pulisic.
Screenshot_20230718_065712_Instagram.jpg
 
KOCHA wa Bayern Munich, Thomas Tuchel ameweka wazi nafasi ya Sadio Mane ni ndogo sana kwenye kikosi cha mabingwa hao wa kihistoria wa Bundesliga. Mabingwa hao wanajiandaa kumpiga bei Mane kwa kitita cha Pauni 17 milioni, ili wapate pesa ya kuongezea kwaajili ya kunasa saini ya Harry Kane.
.
Kwa mujibu wa Sport1, Tuchel alisema: “Hakuwa na matarajio makubwa baada ya kujiunga, ushindani ni mkali sana, nafasi ya kikosi cha kwanza imekuwa ngumu na mchezaji anaelewa pia, anaelewa mawazo yangu na klabu kwa ujumla.”
Screenshot_20230718_065758_Instagram.jpg
 
Mpaka sasa Chelsea wana kila dalili ya kuinasa saini ya kiungo wa Brighton Moises Caicedo ,changamoto pekee Chelsea haiko tayari kulipia Pesa zaidi ya €70m hivyo mazungumzo yanaendelea

S/O Fabrizio Romano.
Screenshot_20230718_065943_Instagram.jpg
 
Baada ya Majuma kupita na kuwepo kwa taarifa kuwa uongozi wa Juventus unamtolea macho Lukaku , Mashabiki wa klabu hiyo wameweka wazi hisia zao kuwa hawamuhitaji mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Romelu Lukaku kwenye timu yao.
Screenshot_20230718_070028_Instagram.jpg
 
Ruvu Shooting imeshuka daraja na msimu huu [2023|24] itacheza Ligi ya Championship lakini baadhi ya nyota wake wanabaki Ligi Kuu baada ya kuonekana wanakidhi mahitaji kwenye baadhi ya timu.

Ihefu SC tayari imekamilisha usajili wa Shabani Msala na Mpoki Mwakinyuke [wote kutoka Ruvu Shooting] kuelekea msimu 2023|24.
Screenshot_20230718_070113_Instagram.jpg
 
Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania na Fenerbahce Mbwana Ally Samatta @samagoal77 amejiunga na klabu ya PAOK inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ugiriki akitokea Genk alipokuwa kwa mkopo

Hongera na kila la heri Captain @samagoal77
Screenshot_20230718_070205_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom