Makapuku Forum

Makapuku Forum

SIMBA wanaendelea kutambia usajili unaofanywa na mabosi wao hadi sasa, huku utamu zaidi ni taarifa za winga Peter Banda kukubali kumpisha Luis Miquissone anayejiandaa kutua kambi ya timu hiyo iliyopo Uturuki katikati ya wiki hii kurejesha burudani Msimbazi.
.
Banda ndiye aliyekuwa mrithi wa Luis mara alipouzwa Al Ahly ya Misri na kupewa jezi namba 11 aliyokuwa akiitumia winga huyo kutoka Msumbiji ambaye Simba inamrejesha klabuni kwa mkopo baada ya kumalizana na Wamisri.
.
Habari za ndani ya Simba zinasema, Sio Banda tu, bali hata winga Msenegal, Pape Ousmane Sakho naye dili la kutaka kuuzwa Ulaya limekaa vizuri na kutoa nafasi kwa Simba kuingiza majembe mawili ya kuhitimisha idadi ya nyota wa kigeni kwani kwa sasa tayari ina wachezaji 12.
Screenshot_20230717_122537_Instagram.jpg
 
.
Kiungo Clatous Chama aliyetakiwa kuondoka na wenzake leo kwenda Uturuki, ishu yake BADO kwani kesho ana kikao kingine na mabosi wa Simba.

Kwa mujibu wa chanzo changu makini, Chama atakutana na viongozi kesho Jumanne kuendelea kujadili ishu yake, hivyo ni ngumu kuondoka na wenzake, huenda atasafiri Alhamisi akiwa na wachezaji wengine akiwamo Luis Mkandaji Miquissone kwenda kuongeza nguvu kambini.
Screenshot_20230717_122623_Instagram.jpg
 
JUST IN: Nimepenyezewa taarifa kwamba Yanga imeshamleta kocha mpya wa mazoezi ya viungo, Taibi Lagrouni aliyewahi kufanya kazi na Florent Ibenge ndani ya RS Berkane tayari ameshaanza kazi ndani ya timu hiyo. Lagrouni anakuja kuchukua nafasi ya Helmy Gueldich ‘Manywele’.
Screenshot_20230717_122732_Instagram.jpg
 
WAMILIKI wa Manchester United Familia ya Glazer wanadaiwa kulazimika kuidhinisha usajili wa straika wa Atalanta, Rasmus Hojlund mwenye umri wa miaka 20, kama njia mojawapo ya kuwawezesha kuiuza timu hiyo kwa kiasi cha pesa inachohitaji kwani bila ya kufanya hivyo itapunguza thamani ya timu.
.
Hadi sasa mazungumzo baina ya Atalanta na Man United juu ya staa huyo wa kimataifa wa Denmark yamefikia hatua nzuri
Screenshot_20230717_122923_Instagram.jpg
 
Newcastle United imeweka mezani Pauni 82 milioni kwa Mabingwa wa Ligi Kuu ya Italia, Napoli ili kuipata saini ya winga wa timu hiyo Khvicha Kvaratskhelia katika dirisha hili.
.
Winga huyo wa kimataifa wa Georgia anayecheza upande wa kushoto amewekewa kiasi hicho cha pesa na iwapo kitakubaliwa kitaenda kuvunja rekodi ya usajili ya Newcastle na kumfanya Kvaratskhelia awe mchezaji ghali zaidi kuwahi kusajiliwa na Newcastle.
Screenshot_20230717_123012_Instagram.jpg
 
Kiungo wa Barcelona Frenkie de Jong, 26, huenda akawa sehemu ya ofa itakayotumwa na Barca kwenda Manchester City kwa ajili ya kuipata huduma ya Bernardo Silva, 28, katika dirisha hili.
.
De Jong ambaye amekuwa kuhusishwa na Manchester United tangu dirisha lililopita atajumuishwa kwenye dili hilo ili Barca isilipe pesa kwenye dili la Bernardo Silva. Barca ilihitaji huduma ya Silva tangu dirisha lililopita la majira ya kiangazi lakini dili lilifeli baada ya Man City kugoma kumuuza.
.
Kocha wa Barcelona, Xavi Hernandes amekuwa akimhusudu sana fundi huyu akiamini uwepo wake utasaidia kuboresha eneo lake la kiungo
Screenshot_20230717_123100_Instagram.jpg
 
NYOTA wa Manchester United waliocheza mechi za kimataifa wamerejea rasmi Carrington na tayari wameanza matizi ya kufa mtu, kwaajili ya kujiandaa na msimu mpya wa 2023-24.
.
Kikosi cha Erik ten Hag kilisafiri kwenda Norway na kitaendelea na maandalizi ya mechi ya kirafiki dhidi ya Lyon, hata hivyo, Wachezaji kama Bruno, Casemiro, na Rashford wataendelea na mazoezi ya kujiweka fiti jijini Manchester kabla ya kwenda Marekani kwenye ziara na wakiwa huko watacheza mechi za kirafiki dhidi ya Arsenal, Wrexham, Real Madrid na Borussia Dortmund.
Screenshot_20230717_123157_Instagram.jpg
 
Farha Jr

Kuna wakati kuna maswali mengi hayana majibu, kama Fiston Mayele yupo Yanga kwa mkopo inakuwaje hajaondoka mpaka sasa na klabu inayommiliki ikamuuza? Kwanini inasalia kuwa Yanga ndio ina maamuzi ya mwisho? Maana yake ni Mchezaji wao.

Kuna swali lingine wengine wanasema Mchezaji anamilikiwa na Mtu flani ambaye yeye ndio ana hati miliki ya Mchezaji, kuna mstari hapa tunashindwa kuuvuka kuna CLUB vs AGENCY, Klabu inamiliki Mchezaji ambaye inamchukua kutoka kwenye Agency, hakuna namna Mayele akawa anamilikiwa na taasisi mbili, kinachosoma TFF, CAF na FIFA ndio inayommiliki, thats YANGA ila Agency ina percent yake na influence yake.

In football kuna Third Party Yes kama Tevez na Masche waliokuwa chini ya Global Soccer Agency na kila Mtu alishangaa waliendaje Corinthians kisha West Ham na sio team kubwa? Watu wanaweza tumia hapa kama hoja ya kupinga ila nitakuja na andiko lake maalum tuelewe FIFA wanasemaje.

Kuna misconcept sehemu! Sio kwamba Fiston Mayele anaondoka Yanga bali Yanga inamuuza Fiston Mayele, imefanya biashara na imeingiza pesa nyingi kupitia yeye, moja kati ya biashara kubwa kwenye historia ya mpira wetu.

Dau lake linatajwa kuanzia Billion (kutoka kwa vyanzo) basi ieleweke kuwa Wananchi wamefanya biashara kubwa sana ambayo inakaribiana na mapato ya jezi ya timu zote mbili kwa mwaka, inakaribiana na bajeti ya timu nyingi Ligi Kuu, proper business.

Na hivi ndio namna Mchezaji anaondoka kwenye timu kwa amani! Anakuomba kuondoka, anakutajia timu inayomtaka, anakwambia mahitaji yake na timu inayomtaka inakupa mahitaji yake, Yanga wanakaa chini wanapitia kisha wanafanya maamuzi yao, umeona mgogoro wowote?

Mwisho wa siku nani Mshindi? Mshindi ni Fiston anayeenda kula zaidi na Mshindi ni Yanga ambaye ametengeneza kiasi kikubwa cha pesa mara 10 zaidi ya kile alichotumia kumpata, thats football.

Mpira ni biashara kubwa, Viongozi huja na kuondoka, Wachezaji huja na kupita kisha Mashabiki ndio pekee husalia klabuni, thats football.

Hatimae anaondoka sasa maana tuliteseka sana, Mungu fundi bwana! Unafki sipendi NINA AMANI

Screenshot_20230717_123313_Instagram.jpg
 
Hapa duniani watu wanaweza kuamka tu wakasema leo tunamkomoa fulani... ndicho kilichotokea kwa mchezaji huyu wa Man City ya Uingereza, Benjamin Mendy.

Akiwa katika ya mafanikio wanawake wanalalamika kwamba amewabaki. Mendy anashtakiwa kwa makosa 8... katika utetezi wake Mendy anasema hawezi kamwe kubaka mwanamke.

"Mheshimiwa Jaji, Mpaka sasa nimeisha lala na wanawake elfu 10, nashindwaje kumtongoza mwanamke mmoja mpaka nimbake".

Mendy alisema katika utetezi wake Mahakamani. Mahakama imetoa hukumu kwamba Mendy hana hatia katika makosa yote 8 aliyokuwa ameshtakiwa nayo...!
Screenshot_20230717_123625_Instagram.jpg
 
.
Kiungo Clatous Chama aliyetakiwa kuondoka na wenzake leo kwenda Uturuki, ishu yake BADO kwani kesho ana kikao kingine na mabosi wa Simba.

Kwa mujibu wa chanzo changu makini, Chama atakutana na viongozi kesho Jumanne kuendelea kujadili ishu yake, hivyo ni ngumu kuondoka na wenzake, huenda atasafiri Alhamisi akiwa na wachezaji wengine akiwamo Luis Mkandaji Miquissone kwenda kuongeza nguvu kambini.View attachment 2690797
Mambo ninayopenda kuyasikia kwa sasa Auntie....
Ligi na Ianze tu...
 
.
Kiungo Clatous Chama aliyetakiwa kuondoka na wenzake leo kwenda Uturuki, ishu yake BADO kwani kesho ana kikao kingine na mabosi wa Simba.

Kwa mujibu wa chanzo changu makini, Chama atakutana na viongozi kesho Jumanne kuendelea kujadili ishu yake, hivyo ni ngumu kuondoka na wenzake, huenda atasafiri Alhamisi akiwa na wachezaji wengine akiwamo Luis Mkandaji Miquissone kwenda kuongeza nguvu kambini.View attachment 2690797
Maji ya MDIMU: Chama anatua YANGA
✍️
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom