Farha Jr
Kuna wakati kuna maswali mengi hayana majibu, kama Fiston Mayele yupo Yanga kwa mkopo inakuwaje hajaondoka mpaka sasa na klabu inayommiliki ikamuuza? Kwanini inasalia kuwa Yanga ndio ina maamuzi ya mwisho? Maana yake ni Mchezaji wao.
Kuna swali lingine wengine wanasema Mchezaji anamilikiwa na Mtu flani ambaye yeye ndio ana hati miliki ya Mchezaji, kuna mstari hapa tunashindwa kuuvuka kuna CLUB vs AGENCY, Klabu inamiliki Mchezaji ambaye inamchukua kutoka kwenye Agency, hakuna namna Mayele akawa anamilikiwa na taasisi mbili, kinachosoma TFF, CAF na FIFA ndio inayommiliki, thats YANGA ila Agency ina percent yake na influence yake.
In football kuna Third Party Yes kama Tevez na Masche waliokuwa chini ya Global Soccer Agency na kila Mtu alishangaa waliendaje Corinthians kisha West Ham na sio team kubwa? Watu wanaweza tumia hapa kama hoja ya kupinga ila nitakuja na andiko lake maalum tuelewe FIFA wanasemaje.
Kuna misconcept sehemu! Sio kwamba Fiston Mayele anaondoka Yanga bali Yanga inamuuza Fiston Mayele, imefanya biashara na imeingiza pesa nyingi kupitia yeye, moja kati ya biashara kubwa kwenye historia ya mpira wetu.
Dau lake linatajwa kuanzia Billion (kutoka kwa vyanzo) basi ieleweke kuwa Wananchi wamefanya biashara kubwa sana ambayo inakaribiana na mapato ya jezi ya timu zote mbili kwa mwaka, inakaribiana na bajeti ya timu nyingi Ligi Kuu, proper business.
Na hivi ndio namna Mchezaji anaondoka kwenye timu kwa amani! Anakuomba kuondoka, anakutajia timu inayomtaka, anakwambia mahitaji yake na timu inayomtaka inakupa mahitaji yake, Yanga wanakaa chini wanapitia kisha wanafanya maamuzi yao, umeona mgogoro wowote?
Mwisho wa siku nani Mshindi? Mshindi ni Fiston anayeenda kula zaidi na Mshindi ni Yanga ambaye ametengeneza kiasi kikubwa cha pesa mara 10 zaidi ya kile alichotumia kumpata, thats football.
Mpira ni biashara kubwa, Viongozi huja na kuondoka, Wachezaji huja na kupita kisha Mashabiki ndio pekee husalia klabuni, thats football.
Hatimae anaondoka sasa maana tuliteseka sana, Mungu fundi bwana! Unafki sipendi NINA AMANI