Kiungo mshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza ameendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwania kiatu cha ufungaji bora Ligi Kuu Bara baada ya kufunga mabao matano katika mchezo dhidi ya Polisi Tanzania na kumkaribia kinara Fiston Mayele.
Ntibazonkiza baada ya kufunga mabao hayo amefikisha 15 nyuma moja ya kinara amabye ni Mayele wa Yanga mwenye 16.
Simba na Yanga zote zimebakiwa na mechi moja ya Ligi Kuu ambapo Simba itaivaa Coastal Union katika Uwanja wa Chamazi na Yanga ikicheza Sumbawanga dhidi ya Tanzania Prisons.
View attachment 2648529