Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230521_051526_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20230521_051541_Opera%20Mini.jpg
 
SIMBA, YANGA MWENDO WA NOTI
.
Simba imeng’olewa hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, lakini taarifa njema kwao ni kule kuongezwa mkwanja ikijihakikisha kuvuna Dola 900,000 (zaidi ya Sh 2.1 bilioni) baada ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuongeza mzigo wa fedha za zawadi kwa michuano ya msimu huu.
.
Ongezeko hilo la fedha halijainufaisha Simba tu, bali hadi watani wao, Yanga ambao wametinga fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kwani hadi sasa ina uhakika wa kuvuta Dola 1 milioni (Sh 2.35 bilioni, badala ya 1.8 bilioni zilizokuwa kwenye kiwango cha zawadi cha awali ikimaliza ya pili.
.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi jioni kwenye mtandao wa CAF, zawadi za msimu huu zimeboreshwa kwa asilimia 40 ikiwa ni utekelezaji wa ratifa zilizowahi kutolewa na Rais wa Shirikisho hilo, Dk Patrice Motsepe mapema mwaka huu juu ya ongezeko hilo.
.
Kwa mujibu wa viwango vya sasa vya zawadi hizo kwa Ligi ya Mabingwa, Bingwa anazoa Dola 4 milioni (zaidi ya Sh 9.4 bilioni), huku anayemaliza wa pili atanyakua Dola 2 milioni (zaidi ya Sh 4.7 bilioni) na zile zilizoingia nusu fainali zinakomba Dola 1.2 milioni ( zaidi ya Sh 2.8 bilioni) na zile za robo ambayo Simba nayo ipo hapo ni Dola 900,000 ( zaidi ya Sh 2.1 bilioni).
Screenshot_20230521_140016.jpg
 
KLOPP AWATIKISA TENA MABOSI FA
.
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp ametishia kwamba hatalipa faini yake ya Pauni 75,000 (Sh 220milioni) aliyopigwa na FA kama tu hajaelezwa hiyo pesa itakwenda kufanya nini.
.
Bosi huyo wa Anfield amefungiwa pia mechi moja kutokana na maneno yake aliyotoa dhidi ya mwamuzi Paul Tierney kwamba ana shida zake na Liverpool katika mechi yao ya ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya Tottenham.
.
Kocha huyo Mjerumani amedaiwa atazidi kutibuana na mabosi wa FA kama hatakuwa ameambiwa hizo pesa zinakwenda kutumika kwenye nini, akisema: “Nilitarajia adhabu hii na kila kitu kilichosema kilikuwa sawa. Ningependa kufahamu, kama ilivyo kila siku, hii pesa inakwenda wapi, kama kutakuwa na sababu nzuri, nitakuwa mwenye furaha kulipa. Kama FA watahitaji tu pesa kisha waziweka, basi nitahitaji tuzungumze tena kwa sababu hii haitakuwa sawa.”
Screenshot_20230521_140704.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa
Mabalozi mbalimbali ambapo amemteua Gelasius Byakanwa kuwa Balozi, kabla ya uteuzi huo Byakanwa alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kisha baadaye akawa Afisa Mkuu Ubalozi wa Tanzania, Korea ya Kusini.

Rais Samia amemteua pia Meja Jenerali Ramson Godwin Mwaisaka kuwa Balozi, kabla ya uteuzi huo, Meja Jenerali Mwaisaka alikuwa Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Wanamaji (WTZ), amemteua Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli kuwa Balozi, kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Simuli alikuwa Mkuu wa Utumishi Jeshini (JWTZ).

Wengine walioteuliwa kuwa Mabalozi ni Mohamed Awesu, Dkt. Mohamed Juma Abdallah ambaye alikuwa Katibu Tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja, Hassan Mwamweta ambaye alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi na Mkuu wa Utawala, Ubalozi wa Tanzania, Uturuki, wengine ni Imani Salum Nialikai na Khamis Mussa Omar.

Uteuzi huu wa Mabalozi umeanza May 10, 2023 na wataapishwa kwa tarehe itakayopangwa baadae.
Screenshot_20230522_051716.jpg
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameondoka Zanzibar leo May 21, 2023 kuelekea nchini Qatar kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Jukwaa la Kimataifa la tatu la uchumi linalofanyika Jijini Doha.

Jukwaa hilo linadhaminiwa na Kampuni ya Kimataifa ya Bloomberg lenye kauli mbiu isemayo “ Simulizi za Ukuaji Kimataifa “ ambalo hufanyika nchini Qatar kila mwaka

Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na maelfu ya Washiriki ikiwa ni pamoja na Viongozi wa kampuni kubwa duniani, Viongozi wa juu wa Serikali, na pia Mamlaka zinazohusika za Qatar.
Screenshot_20230522_052235.jpg
 
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo Jumapili Mei 21, 2023 imeingiza mguu katika sakata la mgomo wa wafanyabiashara Kariakoo huku ikiitaka Serikali kutafuta kiini cha tatizo na kukitafutia ufumbuzi.

Kamati hiyo imetoa maelekezo hayo katika kikao chake maalum kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan baada ya kupokea na kujadili taarifa kuhusu mgogoro wa wafanyabiashara wa soko hilo la kimataifa.

“Kamati Kuu baada ya kujadili imeielekeza Serikali kufanya uchambuzi wa kina wa masuala yaliyoibuliwa na kulalamikiwa na wafanyabiashara wa Kariakoo ili kutafuta kiini cha tatizo halisi na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu,”imesema taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema.

Screenshot_20230522_052651.jpg
 
Fiston Mayele baada ya kufanya balaa pale Afrika Kusini akiipeleka Yanga fainali Kombe la Shirikisho Afrika na leo amefunga bao pekee dhidi ya Singida Big Stars ambalo limeipeleka timu hiyo fainali nyingine ya Kombe la Shirikisho Azam (ASFC).

Kwa ushindi huo wa 1-0 Yanga itakutana na Azam FC katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga ikiwa ni mara ya pili kukutana kwa timu hizo ambapo walikutana mara ya kwanza 2015/2016 na Yanga ilishinda 3-1.
Screenshot_20230522_052910.jpg
 
Francis Ngosa, mtoto mwenye umri wa miaka 12 kutoka Kijiji cha Katanga wilaya ya Mansa Mkoa wa Luapula nchini Zambia amefariki dunia baada ya kudaiwa kupigwa na marafiki zake watatu wakati wakicheza mchezo wa ‘mateke na makofi’.

Ofisa Mkuu wa Polisi wa Mkoa, Fwambo Siame amesema kulingana na shangazi wa marehemu, Mary Kabaso, mtoto huyo aliagizwa kuchota maji saa kumi jioni Alhamisi ya Mei 18, 2023 lakini alirejea nyumbani saa mbili usiku, huku akishindwa kutembea.

Shangazi Kabaso alipomuuliza kwa nini anashindwa kutembea na kwa nini alichukua muda mrefu kufanya kazi ambayo kwa kawaida ilikuwa ndogo, alimjibu kwamba alikuwa akicheza na marafiki zake watatu wanaodaiwa kumpiga.

Inadaiwa usiku huo huo hali ya Ngosa ilibadilika na familia yake iliamua kumkimbiza katika Zahanati ya Luamfumu ambako alifikwa na umauti.
Screenshot_20230522_053013.jpg
 
Farhan Jr

NDUGU MGENI RASMI uwaonao pichani ni Wanajeshi kutoka Jangwani walioanza msimu na kambi ya Avic Town hapo Kigamboni, wametetea ubingwa wao wa Ligi Kuu, wametetea ngao yao ya Jamii, wamerejea tena fainali ya FA na wapo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

NDUGU MGENI RASMI, Singida walitaka kuwa serious kidogo! Lakini wao ni nani wangeendana na busta iliyomshinda TP Mazembe, Monastir, Marumo na Club Africain? Ndugu Mgeni rasmi walisema ni mechi ya Beka na Bakari ila uwanjani leo ilikuwa mechi ya quality vs quality.

NDUGU MGENI RASMI, kama kuna Mtu ameumia sana basi avae na akwende zake maana hawa Yanga ni MAN CITY mtupu
Screenshot_20230522_054005.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom