Mwanamke Mmoja ajulikanaye kwa jina la Milembe Seleman (43) Mfanyakazi wa Mgodi wa Geita Gold Mining (GGML) Kitengo cha Ugavi Mkazi wa Mseto Wilaya na Mkoa wa Geita ameuawa kwa kukatwa sehemu mbalimbali za mwili wake na Watu wasiojulikana .
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita Bethaneema Mlay amethibitisha tukio hilo na kusema chanzo cha mauaji hayo bado hakijajulikana na kusema Watu wanne wanashikiliwa kwa ajili ya uchunguzi.
"Tulipata taarifa kwamba huko Mtaa wa Mwatulole Kata ya Buhalahala Tarafa na Wilaya ya Geita Mwanamke mmoja ameuawa na Watu wasiojulikana na Timu yetu ya Makachero walifika eneo lile na na kubaini mwili wake umekatwa maeneo mbalimbali na amepoteza maisha”
Mlay amesema watakapo kamilisha uchunguzi wa kifo hicho watatoa taarifa juu ya waliohusika na mauaji hayo huku akisema kwa mujibu wa waliofika eneo la tukio wanasema alikuwa amekatwa kichwani usoni na mikono yote miwili ambapo mkono wa kulia umeondolewa kiganja”
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.