Makapuku Forum

Makapuku Forum

CAF CHAMPIONS LEAGUE - LEO
.
JS KABLIE VS ESPERANCE
Huu ni mchezo ambao utakutanisha timu zenye upinzani mkubwa Afrika utakaopigwa kwenye Uwanja wa Novembre 1954, nchini Algeria.

Timu hizi ambazo zina rekodi tofauti, Kablie wamechukua ubingwa huu mara mbili wakiwa mara ya mwisho 1996, lakini watavaana na wababe wa Tunisia, Esperance au Es Tunis ambao wametwaa ubingwa mara nne, mara ya mwisho waliuchukua 2019.
.
Takwimu zinaonyesha Kablie ni hatari inapokuwa nyumbani, ikiwa imeshinda michezo mitano kimataifa hivi karibuni, lakini si kigezo cha kuitisha Esperance ambayo imeshinda mchezo mmoja ugenini kwenye makundi.

Katika michezo minane ambayo wamekutana, Esperance wameshinda minne, sare mbili na kupoteza miwili jambo linaloendelea kuzua joto la mchezo huu utakaopigwa leo Ijumaa saa nne usiku.
.
Kablie siyo timu tajiri sana kama zilivyo nyingine za nchi za Kiarabu, kwani kikosi kina thamani ya Sh7.5 bilioni ambapo watakuwa wakivaana na Esperance wenye thamani ya Sh19.8 bilioni.
Screenshot_20230421_134332.jpg
 
PEMBENI YA KITI CHA SHETANI KUNA JINA LA FISTON MAYELE.

Big Thinker mmoja aliwahi kuistaajabisha dunia katikati ya usiku wa mateso na maumivu ya wafia timu juu ya ardhi tukufu ya Mwalimu Julius Nyerere. Usiku wa waswahili na kelele za Wananchi pembeni ya dimbwi la maji na foleni kubwa Jangwani, ila bado kila mmoja anaikumbuka ile kauli yake

Wakati Atlas inatuonyesha Dar es Salaam Tanzania, kalenda inakutukumbusha usiku mmoja wa Agosti 29 mwaka 2021 kwenye kelele nyingi mshale wa saa ya tajiri Gharib Said Mohammed GSM umesimama juu ya saa 1 na dakika 29 usiku, ndipo yule Big Thinker akaishangaza dunia.

Ilipigwa pasi ya upendo umbali mrefu kidogo kutoka Zenji mpaka Congo, Feisal Salum Abdallah aliubariki mpira uliotua kwa Mkongo mmoja pembeni ya uwanja nae akaingia kwenye Box akiwa na speed kali. Ni Ruud Van Nestrooy ndani ya Lupaso akadeshi kama anaachia shuti kali beki mmoja akaruka huku ameficha uso, kisha akarudia tena kama anapiga mlinzi mwingine akaanguka chini.........
Screenshot_20230421_134649.jpg
 
SALIM APEWA MKATABA, MSHAHARA MNONO SIMBA
.
Kipa namba tatu wa Simba, Ally Salim amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu baada ya kuonyesha kiwango kizuri dhidi ya Yanga. Na habari mpya ni kwamba hata mechi ya Jumamosi dhidi ya Wydad Casablanca, Salim ana nafasi kubwa ya kusimama langoni.
.
Awali, Simba ilitaka kumtoa kwa mkopo Salim kabla ya kudaka dhidi ya Yanga ambayo ni kama imemsaidia kuendelea kusalia klabuni hapo hadi 2027 na akivuta mkwanja mnene wa Sh4 milioni.
.
Mshahara wake utakuwa Sh.4 milioni ambayo ni nyongeza ya asilimia 50 ya mshahara wa awali.
Screenshot_20230421_134825.jpg
 
BEKI kipenzi cha mashabiki wa Simba, Henock Inonga:
.
“Tumetoka kucheza na timu ambayo inaongoza msimamo wa ligi na tumepata matokeo ni kipimo kizuri tunaendelea kujifua na kujiweka imara kwa ajili ya Wydad tutaingia kwa kuwaheshimu lakini na sisi pia tuna kikosi kizuri ambacho kipo kwenye hali nzuri ya ushindani dakika 90 zitaamua ubora wa timu zote mbili lakini kwa upande wetu tunapambana kuhakikisha tunatumia vizuri uwanja wetu wa nyumbani,”

………..
Screenshot_20230421_135030.jpg
 
MIGUU YAO INAONGEA
.
09—Lautaro Martínez amefunga mabao tisa kwa Inter Milan kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, Ni wachezaji wanne pekee waliofunga mabao mengi zaidi kwa wababe hao katika mashindano ya Ulaya muda wote waliokipiga klabuni hapo - Adriano (14), Julio Cruz (13), Hernán Crespo (11) na Samuel Eto’o (10).
Screenshot_20230421_135132.jpg
 
HE! ETI UPAMECANO ANAITWA UPAMAGUIRE
.
Mashabiki wa soka wameachwa kwa kicheko cha kuvunja mbavu baada ya mtangazaji wa mechi ya Bayern Munich na Manchester City kumuita beki Dayot Upamecano jina la “Upamaguire“ akiwa na maana ya kufanya makosa mengi uwanjani kama ambavyo amekuwa akifanya nahodha huyo wa Man United.
.
Upamecano, 24, alikuwa akisifiwa kuwa mmoja wa mabeki bora kabisa duniani kabla ya Bayern hawajakutana na Man City kwenye robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
.
Beki huyo Mfaransa alicheza hovyo kwelikweli kwenye mechi ya kwanza ambayo Man City ilishinda 3-0 uwanjani Etihad, kabla ya kurudia kucheza kwa kiwango cha hovyo kwenye mchezo wa marudiano wa sare ya 1-1 uliofanyika Allianz Arena usiku wa juzi.
.
Upamecano alishindwa kabisa kumdhibiti Erling Haaland alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhabu straika huyo ndani ya boksi, lakini aliokolewa na VAR ilipofuta kadi hiyo kwa madai Haaland alikuwa ameokoa. Upamecano alifanya makosa mengine dhidi ya Haaland na safari hii, straika huyo aliweka mpira kwenye nyavu.
.
Mtangazaji wa mechi alishindwa kuvumilia kwa makosa hayo ya Upamecano na kumlinganisha na mtaalamu wa makosa mengi, beki wa Man United, Harry Maguire kwa kumwita Upamaguire. Upamecano akiwa na mpira dakika tano za mwisho, mtangazaji huyo Mwarabu alisema: “Upamaguire” kitu kilichowafanya mashabiki kuangua kicheko na kupendezwa na utani huo.

Screenshot_20230421_135317.jpg
 
ZINCHENKO ARUDI
.
Arsenal imepata mzuka zaidi kwenye vita yao ya kusaka ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu baada ya kurejea mazoezini kwa staa wao Oleksandr Zinchenko.
.
Beki huyo wa kushoto alikosa mechi ya sare ya 2-2 dhidi ya West Ham United wikiendi iliyopita kutokana na kuwa majeruhi ambapo alichezeshwa Kieran Tierney.
.
Sasa mkali huyo anaonekana kuwa amepona maumivu yake ya misuli aliyoyapta kwenye mechi dhidi ya Liverpool wiki mbili zilizopita na anatazamiwa kuwa fiti kwa ajili ya mechi ya Southampton itakayopigwa leo Ijumaa.
Screenshot_20230421_135456.jpg
 
ZINCHENKO ARUDI
.
Arsenal imepata mzuka zaidi kwenye vita yao ya kusaka ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu baada ya kurejea mazoezini kwa staa wao Oleksandr Zinchenko.
.
Beki huyo wa kushoto alikosa mechi ya sare ya 2-2 dhidi ya West Ham United wikiendi iliyopita kutokana na kuwa majeruhi ambapo alichezeshwa Kieran Tierney.
.
Sasa mkali huyo anaonekana kuwa amepona maumivu yake ya misuli aliyoyapta kwenye mechi dhidi ya Liverpool wiki mbili zilizopita na anatazamiwa kuwa fiti kwa ajili ya mechi ya Southampton itakayopigwa leo Ijumaa.View attachment 2595105
Paja kama paja🙈🙈
 
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amekataa kutia saini muswada wa sheria dhidi ya mapenzi ya jinsia moja unaotoa adhabu ya kifo katika baadhi ya makosa, akiomba ufanyiwe marekebisho kabla ya kuutia saini kuwa sheria.

Uamuzi wa Museveni ulitangazwa Alhamisi baada ya kikao cha wabunge wa chama tawala ambao karibu wote waliunga mkono muswada ulioidhinishwa na wabunge mwezi uliopita.

Taarifa zinasema, wabunge hao wamekubaliana kuurejesha bungeni ili ufanyiwe marekebisho, huku Msemaji wa ofisi ya Rais, Sandor Walusimbi akisema kuwa Rais Museveni hapingani na adhabu zilizopendekezwa katika mUswada huo, bali alitaka wabunge kuangalia suala la urekebishaji wa watu hao.
Screenshot_20230421_135859.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom