Makapuku Forum

Makapuku Forum

| YANGA YAPAA KUIFUATA RIVERS UNITED
Screenshot_20230420_145833.jpg
 
KIPARA NI YEYEEE!!
.
2009—Barcelona
2010—Barcelona
2011—Barcelona
2012—Barcelona
2014—Bayern
2015—Bayern
2016—Bayern
2021—Man City
2022—Man City
2023—Man City
.
Pep Guardiola ndiye Kocha wa Kwanza katika historia kufika Nusu Fainali mara 10 za Ligi ya Mabingwa Ulaya
Screenshot_20230420_150014.jpg
 
BAYERN KUMPIGA CHINI MANE
.
Lisemwalo ni Bayern Munich wanafanya kila wanaloweza kuhakikisha wanampiga chini Sadio Mane mwishoni mwa msimu huu baada ya kumpiga faini ya Pauni 260,000 (Sh 760milioni) kwa kosa la kumpiga ngumi ya mdomo Leroy Sane.
.
Winga huyo wa zamani wa Manchester City, Sane alionyesha namna mdomo wake ulivyovimba baada ya kichapo hicho kutoka kwa mchezaji mwenzake, Mane, kufuatia kutibuana kwenye mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya robo fainali dhidi ya Man City iliyofanyika Etihad na wakali hao wa Allianz Arena kuchapwa 3-0.
.
Mane, ambaye alitua Bayern mwaka jana akitokea Liverpool alifungiwa kuchezea timu yake kutokana na kosa hilo. Sasa, mwandishi nguli wa habari Florian Plettenberg amesema klabu hiyo itafanya jaribio la kuachana na Msenegali huyo mwisho wa msimu.

……………….
Screenshot_20230420_150219.jpg
 
Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) limempanga Issa Sy kutoka Senegal kuwa mwamuzi wa mchezo wa Mkondo wa Kwanza wa Robo Fainali, Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Simba SC dhidi ya Mabingwa watetezi Wydad Casablanca
.
Takwimu za michezo 15 iliyopita ya michuano ya klabu Barani Afrika ambayo amechezesha mwamuzi huyo, timu mwenyeji zilishinda mara tisa, sare mbili na zilipoteza nne.
.
Ni mwamuzi ambaye Simba SC wanapaswa kuwa makini naye hasa katika suala la nidhamu kwani amekuwa na hulka ya kumwaga kadi na kuthibitisha hilo, katika michezo 15 iliyopita alitoa kadi 70 sawa na wastani wa kadi 4.5 kwa kila mchezo, kadi za njano 67 na kadi nyekundu tatu.

Screenshot_20230420_150427.jpg
 
Farhan Jr

FERGIE NA GUARDIOLA, MWANZO WA NA MWISHO WA ENZI.

Majira ya kiangazi huko nchini Uswisi, nyumba maalum ya UEFA wenyewe wanapaita UEFA Football House, pembezoni mwa Lake Geneva mandhari nzuri sana kama Lake Victoria jijini Mwanza, ndio ni makao makuu ya shirikisho la soka barani Ulaya kulikuwa na mkutano maalum wa Makocha Ulaya kujadili mpira na mabadiliko ya kimfumo na utawala.

Siti ya mbele ameketi Don Carlo Ancelotti, nyuma yupo Arsene Wenger The Professor, Marcelo Bielsa na Mafundi wengi ila Jose Mourinho ameketi pembeni ya Sir Alex Ferguson, ila nyuma yao yupo Pep Guardiola Sala amevalia suti yake ameketi kwa unyenyekevu sana! Mwanafunzi bora zaidi wa mchezo huu pendwa.

Wakati wa mapumziko Makocha wengi walikuwa wanapiga stori ila Pep alijitenga peke yake maana hana historia kubwa Ulaya na ni 2008 punde tu baada ya kupewa kibarua Barcelona, Pep ni Kijana mkimya aliyependa kujifunza sana kwa wakongwe.

Alikuwa ni Jose Mourinho aliyemfuata Pep na kumwambia sogea jumuika nasi, Pep akamwambia anatamani sana kuongea na Sir Alex Ferguson! Basi Jose Mourinho akamwambia Mzee atachukua kahawa ataelekea Balcony basi mfuate akienda kule ili useme nae, Pep alimshukuru sana Mourinho kumbuka ni wana sana hawa japo huwa wanapasuana sana

Ni kweli Babu Fergie alichukua kahawa kisha akatoka taratibu kuelekea Balcony kutazama mandhari ya Ziwa Geneva, zuri la kuvutia kama Victoria kasoro yake hili ni kuwa halina Wasukuma! Ndipo Pep akaenda kuongea na Babu, alipofika akamsamilia kwa heshima sana! Babu akamjibu kwa upendo sana kwakuwa ni Mtu safi Mskochi.

Guardiola kumbuka alishasafiri mpaka Argentina kupata madini ya Marcelo Bielsa ‘Priest of the Nun’ kisha amekaa na Godfather Johann Cruyff na sasa ni zamu ya Fergie kumpa baraka zake, hawa hapa Watalaam wawili wanazungumza mpira wa miguu.

Dunia haikuwahi kufahamu kama msimu huo wa 2008/09 watakutana fainali pale Roma, ila wapiga picha haswa Steve Arnolds alipiga picha akijua ni ya kawaida kati ya Fergie na Shabiki wake tu, ila ilikuwa picha ya Fergie na mrithi wake kwenye ufalme wa mbinu na mamlaka kwenye soka la kisasa! Yes the Senior na Junior wake.

Babu Fergie akawa……

ITAENDELEA!
Screenshot_20230420_150642.jpg
 
Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema kikosi chao kipo sawa kwa 100% wanakwenda kupambana Nigeria ili kufuzu Nusu Fainali licha ya kujua soka la Afrika lina mambo mengi nje ya uwanja lakini tayari wamewaandaa wachezaji wao kiakili.

“Wachezaji wote wako vizuri hadi wale ambao walicheza mechi ya derby [Simba vs Yanga] hakuna majeruhi wala ambaye atakosekana kutokana na adhabu ya kadi.”

“Tunaamini tumejipanga vya kutosha kuelekea hiyo mechi ya kwanza, tunaamini hii mechi itakuwa tofauti kwa sababu vikosi viko tofauti. Wao kikosi chao kimebadilika na sisi kikosi chetu kimebadilika kwa kiasi kikubwa.”

“Tumefatikia mechi zao kwenye Ligi, wapo nafasi ya pili kwenye Kundi lao [wanacheza Ligi kwa mtindo wa Makundi], tumefatilia mechi zao za hatuaya makundi ya Kombe la Shirikisho. Ni timu tofauti na tunajua nini tunapaswa kupanya ili kupata matokeo mazuri kwenye hiyo mechi ya kwanza.”

“Tunajua mpira wa Afrika lakini kitu kikubwa ni kuwa makini na yale yatakayotokea ndani ya dakika 90 na kujipanga vyema kwa mchezo wenyewe. Tumejiandaa kiakili kwa kila kitakachotokea, tusisahau tupo kwenye njia ya kwenda Nusu Fainali kwa hiyo mazongira hayatakuwa rahisi.”

“Tutacheza kulingana na mpinzani mwenyewe kakini tukijua hii ni mechi ya kwanza na kuna mechi ya pili.”
Screenshot_20230420_151330.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom