Makapuku Forum

Watoto wawili wa Familia moja Anuari Salum (5), Mwanafunzi wa Darasa la Awali Shule ya Msingi Manzese na Nurat Shabani (12) Mwanafunzi wa Darasa la Sita Shule ya Msingi Mazinyungu Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamefariki baada ya kugongwa na gari wakati wakiwa pembezoni mwa Barabara wakisubri kuvuka.

Ajali hiyo imetokea eneo la Mazense Kata ya Mkwatani Wilayani Kilosa, Morogoro Barabara ya Kilosa - Dumila ambapo gari dogo lenye namba za usajili T I63 DJH liliacha njia na kuwafuata Watoto hao wakiwa pembezoni mwa Barabara.

Akiongea na @ayotv_ kwa njia ya simu RPC wa Morogoro, Alex Mkama, amesema chanzo cha ajali ni mwendokasi wa Dereva aliyekuwa anaendesha gari hilo, Endishi Christian (41).

Dereva huyo kwa sasa anaendelea kushikiliwa na Polisi na upelelezi utakapokamilika atafikishwa Mahakamani.
 
Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kipaumbele cha Urusi kwa sasa ni kudumisha uhusiano zaidi na Nchi za Barani Afrika wakati huu ambapo Urusi inatafuta Washirika wapya kukabiliana na vikwazo vya kimataifa juu ya vita ya Ukraine na Urusi.

Putin amesema hayo jana Jumatatu kupitia hotuba yake kwenye mkutano kati ya Urusi na Wajumbe kutoka Nchi za Afrika ambapo amesema Urusi inapanga kuongeza ushirikiano na Nchi za Afrika katika nyanja za nishati, matibabu na usambazaji wa dawa na pia kuongeza idadi ya Wanafunzi wa kutokea Afrika katika Vyuo Vikuu vya Urusi.

Katika mkutano huo uliodhuriwa na zaidi ya Wajumbe 40 kutoka Afrika, Putin amesisitiza kuwa Urusi imedhamiria kuendelea kujenga ushirikiano kamili wa kimkakati na Nchi za Afrika na kuunda ajenda za Kimataifa kwa pamoja.

Mkutano ujao wa Urusi na Afrika, unatarajiwa kufanyika July 26-29 mwaka huu Jijini St. Petersburg nchini Urusi ambapo Rais Putin amesema atauandaa vizuri mkutano huo na kuwaalika Viongozi wa Afrika na Mashirika ya Kikanda kushiriki.
 
Wazazi Nchini Ufaransa wanaweza kupigwa marufuku ku-post picha za Watoto wao kwenye mitandao ya kijamii iwapo mswada mpya uliowasilishwa wiki hii utapitishwa kuwa sheria.

Mswada huo utaipa Mahakama mamlaka ya kuwapiga marufuku Wazazi kuweka picha za Watoto wao mtandaoni ambapo wote wawili watawajibikia katika kusimamia haki za picha za Watoto wao huku uamuzi wowote wa kuzipost mtandaoni ukitakiwa kuzingatia umri wa Mtoto pamoja na kiwango cha ukomavu wake.

Sheria inayopendekezwa inakuja baada ya muamko wa wazazi wengi kupost picha za watoto wao mitandaoni jambo ambalo huitwa “sharenting” ikijumuisha moja ya jambo kuu linalo hatarisha haki za faragha za watoto, kulingana na taarifa ya maelezo ya mswada huo pia ilisema asilimia 50 ya picha zinazotumiwa kwenye majukwaa ya ponografia ya watoto hapo awali zilichukuliwa kupitia picha zilizopostiwa na wazazi wenyewe kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa Daily Mail, mswada huo bado unahitaji kupitishwa katika Bunge la Seneti ya Ufaransa kabla ya kusainiwa na kutangazwa na Rais kuwa sheria.
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeishauri Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kuanza kuufanyia kazi ushauri wa kulifanya Daraja la Tanzanite kuwa la tozo na kila gari linalopita kwenye Daraja hilo lilipie fedha.

Ushauri huo umetolewa wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara kutembelea mradi wa Barabara wa njia nane kutoka Kimara hadi Kibaha ambapo waliongozana na Viongozi na Watumishi kutoka TANROADS, akiongea kwa niaba ya Wajumbe wa Kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Selemani Kakoso amesema ipo haja ya kuanza na mfumo wa Barabara zenye tozo katika mradi wa ujenzi wa Barabara hizo za njia nane kama ilivyo haja ya kuanza tozo Daraja la Tanzanite.

“Sheria inatukataza kujenga Barabara za tozo kama hauna Barabara mbadala lakini hapa kuna nia mbadala kwanini msingelianza na hizi hapa tukawa na Barabara za kulipia?, hii ni sawa na lile Daraja la Tanzanite tuliishauri Serikali wangelifanya kuwa la tozo yaani kila anayepita atozwe maana Daraja mbadala ambalo ni Salender lipo, kwa hiyo lazima haya myafanyie kazi”
 
Tetemeko kubwa la ardhi limesikika katika baadhi ya maeneo ya Afghanistan, Pakistani na India hali iliyosababisha wananchi kujawa na hofu na kutoka barabarani.

Ripoti za awali zilisema tetemeko hilo lilisikika katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, pamoja na miji kadhaa ya Pakistani, ikiwa ni pamoja na Islamabad na Lahore.

Hadi sasa hakuna ripoti ya mtu yeyote aliyejeruhiwa kutokana na tetemeko hilo lililotokea leo Jumanne Machi 21, 2023.

 
Mamlaka nchini Malawi zinasema kuwa idadi ya watu ambao bado hawajulikani walipo kufuatia Kimbunga Freddy imeongezeka kutoka 349 hadi 427 huku idadi ya vifo ikiongezeka kutoka 476 hadi 499 na majeruhi 1,332.

Idara ya Masuala ya Kukabiliana na Majanga ya Malawi (DoDMA) imesema hadi kufikia jana Jumatatu Machi 20,2023 idadi ya watu waliokimbia makazi yao walikuwa ni 508,244.

Nchi kadhaa zikiwemo Tanzania, Uingereza na Zambia zimetuma timu kusaidia katika shughuli za uokoaji nchini humo.
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amewataka viongozi wa chama hicho kuyaeleza kwa wananchi mambo mazuri yanayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Kinana ameyasema hayo leo Jumanne Machi 21, 2023 jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kuanzia ngazi ya Taifa hadi Wilaya.

“Katika maeneo yenu hakikisheni mnakisemea chama na mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Samia, wala msione haya kusema ili wananchi wajue na hata katika chaguzi zijazo tusipate shida.
 
Kiongozi wa chama cha Azimio la Umoja nchini Kenya, Raila Odinga ametangaza kuwa muungano huo umeazimia kufanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki.

Raila ametoa kauli hiyo leo Jumanne Machi 21, 2023 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nchini humo ambapo amesema kuwa watakuwa wakiingia mitaani kila siku za Jumatatu na Alhamisi hadi pale matakwa yao yatakaposhughulikiwa.

Odinga ambaye alishawahi kuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo amewataka wafuasi wake kususia bidhaa kadhaa ikiwa ni pamoja na chombo kimoja cha habari, benki moja ya kitaifa na kampuni moja ya simu.

 
CAF imetoa mabao bora katika mzunguko wa tano wa Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo Klabu ya Simba SC imetoa wachezaji wawili Sadio Kanoute na Clatous Chama ambao walifunga dhidi ya Horoya AC katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kwenye ushindi wa mabao 7-0.

Mabao yaliyochaguliwa ni lile la kwanza la Chama alilofunga dakika ya 10 kwa 'free-kick' na la Kanoute alilofunga lililokuwa la saba dakika ya 87 kwa shuti.

 
Wachezaji wawili wa Al Alhly (Mahmoud Kahraba na Percy) na Simba SC
(Clatous Chama na Sadio Kanoute) wamechagulia kuwania nafasi ya mchezaji bora wa wiki katika mzunguko wa 5 CAF.

Chama ambaye alishinda nafasi hiyo mzunguko wa nne amefunga hat trick na kutoa pasi moja ya bao katika mabao mawili ya Kanoute Simba ikiichapa Horoya mabao 7-0.

Upigaji wa kura hizo unafanyika kwenye page ya Twitter ya TotalEnergies CAFCL-TotalEnergies CAFCC.
 
Kiungo wa Yanga, Feisal Salum 'Fei Toto' baada ya kutua nchini Misri amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu maandalizi ya mechi dhidi ya Uganda kufuzu Afcon 2023.

Fei Toto akihojiwa na kituo cha televisheni cha Azam amesema wamejiandaa vizuri na wanaahidi ushindi kwa watanzania.

"Kweli kuna wachezaji wapya na mwalimu mpya ila Uganda tunawaheshimu ni timu nzuri ina wachezaji wazuri, ila tutaipambania Taifa Stars ili tupatematokeo,"

Ameongeza; " Katika mechi mbili watuombee dua na tutapata matokeo kwa uwezo wake Mungu,"

Taifa Stars itacheza mechi mbili na Uganda ikianzia ugenini Misri Machi 24 na kurudiana Machi 28 jijini Dar.

 
HAIJAWAHI KUTOKEA: Kikosi Bora cha WIKI hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika timu moja ikatoa wachezaji WANNE.

Hongera @simbasctanzania
 
Nani anastahili kuwa Mchezaji Bora wa Wiki Ligi ya Mabingwa Afrika ..!?
.
⌾ Clatous Chama (Simba SC)
⌾ Mahmoud Kahraba (Al Ahly)
⌾ Percy Tau (Al Ahly)
⌾ Sadio Kanoute (Simba SC)
.
 
Sports Arena Tz

Timu nyingi zinazoongoza kwenye makundi ya michuano ya Kombe la Shirikishoa hazina rekodi kubwa sana kwenye soka la Afrika. AS Rabat
imefanikiwa kuchukua ubingwa huo mara moja tu mwaka 2005 ikiongoza Kundi C, Rivers ya Nigeria
inaongoza Kundi B lakini ikiwa haijafuzu bado, haina makali ikiwa ni timu changa zaidi kwenye michuano hii na haijawahi kufika hatua hii ya robo fainali.
.
Mwingine ambaye anaweza kukwea juu ni Asec Mimosa
nayo inalingana pointi na Rivers lakini ikiwa imeishia Nane Bora kwenye michuano hii ikiwa haina makali sana. Timu nyingine ambayo haina makali lakini ipo kileleni ni Marumo ya Afrika Kusini
ambayo imeanzishwa mwaka 2021 ikiwa ndiyo mafanikio yake makubwa, zote ni kati ya timu ambazo zikikutana na YANGA inaweza kuzichapa na kwenda hatua ya nusu fainali.
 
MUSONDA, LOMALISA NDANI KIKOSI BORA CHA WIKI SHIRIKISHO AFRIKA.
.
3— Future FC
2— Yanga SC
1— Rivers United
1– Asec Mimosas
1— Real Bamako
1– Asko
1— FAR Rabat
1– Al Akhdar
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…