Makapuku Forum

SIMBA na Yanga zinahitaji ushindi tu katika mechi za klabu Afrika dhidi ya Horoya na Monastir mwishoni mwa wiki hii ili zitinge robo fainali.

Lakini kabla ya hilo kutimia, tayari timu hizo zimeshaipa neema Tanzania baada ya kuingiza timu nne kwenye mashindano ya klabu Afrika msimu ujao kwa mara ya tatu mfululizo.

Kitendo cha Simba kuwepo katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika hadi sasa kimeihakikishia Tanzania pointi moja wakati kwa Yanga kuwepo kwenye hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika hadi sasa kimeihakikishia Tanzania pointi 0.5.

Timu hizo mbili zimefanya Tanzania iwe na pointi 29 na kushika nafasi ya tisa katika viwango vya mafanikio ya nchi kutokana na ushiriki kwenye mashindano ya klabu Afrika ambavyo nchi 12 zilizo juu ndizo kila moja inapata nafasi nne za uwakilishi kwenye mashindano ya Afrika.
 
AZAM YAITAKA NAFASI YA TATU
.
Azam FC imejiondoa rasmi kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu na kujiweka kwenye wakati mgumu kumaliza ndani ya mbili bora na sasa baadhi ya nyota wake wakikiri wana kibarua kumaliza msimu kwa heshima katika mechi zilizobaki.
.
Kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Abdul Suleiman ‘Sopu’ amesema “Tumepoteza lengo la ubingwa tunahitaji nafasi ya tatu yenye ushindani kwa pointi tulizonazo tunahitaji 15 katika mechi tano zilizobaki, huku tukiwaombea Singida ichemshe,” alisema Sopu.
.
“Sisi kama wachezaji tunatakiwa kutumia muda huu kujitafakari ili kujiweka mazingira ya ushindani tukirudi tuanze upya kwa kukusanya pointi zote 15 kwenye mechi tano zilizobaki.”
.
Azam imebakiza mechi dhidi ya Mtibwa Sugar, Ruvu Shooting, Namungo, Coastal Union na Polisi Tanzania.
 
.
“Kama akifunga hat-trick mbili (mabao 6) katika umri wa miaka 22, 23, atakinai katika maisha yake. Atakuwa hana malengo ya kuyafikia huko mbele. Ndio maana nikamtoa alipofunga mabao matano,” kauli ya kocha Pep Guadiola akitoa sababu ya kumpumzisha Erling Haaland na kumnyima nafasi ya kufunga zaidi katika ushindi wa Man City wa 7-0 dhidi ya RB Leipzig juzi.
 
Yanga walianza kumuuguza mchezaji wao Yacouba Songne ambaye alikuwa na majeraha kwa muda mrefu hadi akapona, akacheza mashindano ya Mapinduzi Cup lakini inaonekana benchi la ufundi lilimshauri atafute timu nyingine kutokana na ushindani wa nafasi uliopo kwa sasa kikosini.

Yacouba akajiunga na Ihefu na sasa anafanya vizuri ikiwa ni pamoja na kuchaguliwa mchezaji bora wa mwezi Februari baada ya kufunga magoli mawili na kutoa assist moja katika mechi mbili alizocheza mwezi huo.

Sasa hivi tunaona Hassan Dilunga amerejea kwenye kikosi cha Simba baada ya kuwa nje kwa muda mrefu akiuguza majeraha ya goti.

Kwa hiyo benchi la ufundi baada ya kuona uwezo wake litatoa mapendekezo yake ya kiufundi ili Dilunga aendelee kubaki Msimbazi au aruhusiwe kwenda mahali pengine.

Ni ustaarabu na utaratibu mzuri klabu kitu ambacho Azam FC wamekuwa wakikifanya kwa muda mrefu sana.
 
Kwa mujibu wa @FARPostZA, FIFA klabu ya Yanga huenda ikafungiwa kusajili wachezaji kwa madirisha matatu (3) mfululizo baada ya kushindwa kumlipa fidia ya kuvunja mkataba aliyewahi kuwa Kocha wao Luc Aymael.

Kocha huyo raia wa Ubelgiji ambaye pia amewahi kuzifundisha Free State Stars na Polokwane City za Afrika Kusini, Oktoba 2022 alishinda kesi ya kuvunjiwa mkataba na Yanga bila kufuata utaratibu.

Klabu ya Yanga ilipewa maelekezo ya kumlipa Kocha huyo jumla ya dola za Marekani 152,000 kufuatia kumfuta kazi pasipo kufuata taratibu miaka miwili iliyopita.

Baadae klabu ya Yanga ilipanga kulipa kiasi hicho kwa awamu tano (5) ambapo awamu ya kwanza alipaswa kuwa Oktoba 2022.

Kwa mujibu wa FARPost, Yanga ililipa deni hilo kwa awamu mbili, Oktoba na Novemba 2022.

Kwa maana hiyo, Yanga bado wanadaiwa na Eymael dola za Marekani 99,000 pamoja na ada ya adhabu ambayo ni dola za Marekani 5,000.
 
Gianni Infantino amechaguliwa kwa mara nyingine tena kuwa Rais wa FIFA na sasa ataongoza kwa kipindi kingine cha miaka minne (4) [2023-2027]. Uchaguzi huo umefanyika Jijini Kigali, Rwanda.
 
Mwamba Imara kabisa TARIBO WEST moja kati ya Mafundi wa mpira kuwahi kuhudumu AC Milan na Inter Milan pamoja na timu ya taifa ya Nigeria.

Ni Mchungaji wa kanisa la Pentekoste, ambaye anatumia muda wake hivi sasa kuhubiri neno la Bwana, huku akiweka wazi alijiona ana upako tangu yupo Milan ambapo aliwasaidia Wanawake kutoka Nigeria waliopelekwa Italia kujiuza, akawabadili na kuwapa maisha na baadae ajira.

Unamkumbuka Fundi huyu??
 
Farhan Jr Kihamu

GODFREY BONNY NDANJE, hisia kali kwenye mchana wa jua kali kabla ya kuanza safari ya kurejea Ifakara stendi ya Makali imenipasa kwanza nishike daftari kwa tahadhali kuandika kuhusu Kiungo huyu hatari, naomba muda tafadhali.

GBN zimebarikiwa zile mvua za Tukuyu, hazikunyesha kustawisha Parachichi pekee bali Mbuyu mmoja kwenye eneo la Kiungo cha mpira, kitovu chako kilifukiwa kwenye ardhi ya Tukuyu Stars na ukawaahidi kuwa legacy will live on na Tukuyu itaishi daima kwenye ramani ya mpira Tanzania.

Ndanje! Ungekuwa hai ningesema Mbula Tukete, lakini haupo tena! Syosa amenye Kyala sina budi kusema! Kyala Nnunu napaswa kuandika, Kiungo mwenye Upara The Pride of Kusini and Nyakyusa land, mikono inatetemeka sioni cha kuandika Ndanje.

Umepumzika sasa kwenye migomba huko Tukuyu lakini kumbukumbu zako zitaishi daima, sijui unacheza mpira huko ulipo basi kutakuwa na mechi bora sana kati yako na Patrick Mafisango, kama kuna maisha mengine huko basi Ndanje endelea kuburudisha kwa hicho kipaji chako.

Wanyakyusa na Wahehe ni Rafiki zangu, wamenilea kwenye ardhi zao! Nawahusudu sana kama navyohusudu kipaji chako, Nkamu pumzika kwa amani, ulishamaliza kazi yako ya namna ya kuwa Kiungo wa mpira mwenye maamuzi magumu na pass za uhakika, umekata sana risiti za Niyonzima na Mafundi wengine.

Miaka imesogea na mvua zinaendelea Tukuyu, naamini kuna siku mbegu nyingine itamea, iwe Msasani, Bagamoyo, Ushirika, KKK, Kiwira au Ntokela ila naamini Bonny mwingine atazaliwa! Pumzika GBN.

Tukuyu will rise again, the Legacy of Nyakyusaland will live on forever japo Madogo zako wanauza Iphone Makumbusho siku hizi🫡

Syosa Amenye Kyala
!

 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…