Makapuku Forum

Makapuku Forum

Medrad Mbigi (28) Mfanyabiashara katika Mtaa wa Mpechi Halmashauri ya Mji wa Njombe anashikiliwa na Polisi Mkoa wa Njombe kwa tuhuma za kumbaka mara kadhaa Mtoto wake wa kufikia mwenye umri wa miaka nane huku sababu ikitajwa kuwa ni imani za kishirikina.

RPC wa Njombe Hamis Issah amesema wanaendelea kufuatilia ili kubaini ulikoanzia ushirikina na kumkamata aliyesababisha jambo hilo.

"Alichokifanya huyu Baba amekuwa anambaka Mtoto wa kufikia wa Mke wake ambaye anakaa nae , tumebaini tukio hilo ni kweli na sasa hivi tunaendelea na uchunguzi na kwakuwa limehusisha ushirikina sasa tunachokifanya kule ushirikina ulikoanzia ndio tutafuatilia mpaka tuhakikishe huyu aliyesababisha hili anakamatwa"

Kamanda Issah ametoa wito kwa Wananchi wa Njombe kuwa makini na Watoto wao na kutoa taarifa mapema wanapoona vitendo vya ukatili kwa Watoto wao ili kudhibiti vitendo hivyo.
Screenshot_20230316_045451_OGInsta%2B.jpg
 
Bibi mwenye umri miaka 80, Fatuma Kimbawala, Mkazi wa Mtaa wa Magongo Halmashauri ya Mji wa Makambako Mkoani Njombe ameuawa kwa kunyongwa kisa mali huku Watoto wake wanne wakikamatwa kwa kuhusishwa na tukio hilo.

RPC wa Njombe, Hamis Issah amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiwataka Wananchi Mkoani Njombe kutumia Vyombo mbalimbali vilivyo sahihi ili kupata ufafanuzi juu ya mgawanyo wa mali.

"Watoto wa huyu Mama tumewakamata baada ya kuhusishwa na tukio la huyu Mama, bado kuna maswala ya kugombania mali za urithi kwenye Jamii Mkoani Njombe, tunawaomba Wananchi kama kuna mali inagombewa kuna Vyombo ambavyo vinaweza kutumika"
Screenshot_20230316_045540_OGInsta%2B.jpg
 
"Tumesambaza miundombinu ya mawasiliano kwa asilimia zaidi ya 96, imebaki asilimia nne kwa upande wa Tanzania Bara nikiwa namaanisha minara, Zanzibar tumesambaza asilimia 99 na juzi tumewasha minara takribani 44.

"Changamoto kubwa ni baadhi ya minara iliyokuwa imejengwa kwa muda mrefu inatoa huduma ya 2G ambayo mtu anayoweza kuitumia kupiga simu kwa njia ya sauti na si kutuma picha au kufungua picha.

"Serikali katika bajeti tumetenga fedha kwa ajili ya kwenda kuibadili na kuiongezea uwezo ili iwe 3G." Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Screenshot_20230316_045705_OGInsta%2B.jpg
 
''Vyama viboreshe namna ya kuwapata wagombea kwa kujua tabia na mienendo yao mapema zaidi, kuliko twende na mtu kwa mihemko ikafika wakati kwa katiba na mifumo tuliyonayo yeye ndiyo anadhibiti mifumo badala ya mifumo imdhibiti yeye.

"Hii miaka miwili ya Rais Samia Suluhu Hassan katuonyesha dira nzuri lakini hii dira nzuri haituambii kama kesho na kesho kutwa anaweza akaendelea kuwa nayo.

Inawezekana ikafika wakati naye ni binadamu akashauriwa vinginevyo, sisi tunapaswa kulilia sana mifumo, nilikuwa naangalia sana ripoti ya tume ya taifa ya uchaguzi.

"Katika miaka miwili ambayo tunafurahia Rais Samia kuupiga mwingi tusisahau kuboresha mifumo yetu, tunaweza kujikuta siku hatujaboresha mifumo yetu mwisho umepigwa mwingi hadi nje ya magoli, umepigwa mwingi hadi tukacheza nje ya uwanja

"Hii kumsifia Rais na kumpongeza ni jambo jema kabisa lakini tusipongeze na kusahau misingi ambayo inayopaswa kuendesha Taifa letu kwa kizazi cha sasa na baadaye.'' Salehe Mohammed, Mhariri wa Siasa Gazeti la Mwananchi.
Screenshot_20230316_045759_OGInsta%2B.jpg
 
''Kuna mambo ambayo kila wakati yanatuvuta shati nyuma sasa hivi watu wanazungumzia ulimwengu wa kidigitali, sisi tumezindua 5G ulimwengu unaelekea kwenye 6g, yapo mataifa yanahamia huko.

Mataifa ya wenzetu yanajadili namna yanavyoweza kutia viongozi vijana wa kesho watakokuwa na uwezo wa kumudu uchumi wa kidigiti, kwenye uchumi huu kuna fursa nyingi za kuonheza ajira, kuondoa taifa kwenye umasikini na kuoata huduma na bidhaa mpya lakini sisi tunafanya nini.

Fursa tunazo nyingi tumejenga mkongo wa Taifa na Mfuko wa UcSaf unaendelea kuhakikisha unafikisha huduma ya mawasiliano kwa watu wengi zaidi lakini wakati hayo yanafanyika tukumbuke kuna vijiji kama 3000 ambavyo havina huduna ya intaneti kati ya vijiji 12000 vilivyopo ambayo ni takribani robo

Unapokosa intaneti, kwa mataifa yaliyoendelea kama nchi ya Histonia, intaneti ni haki ya binadamu, popote ulipo na unachokifanya ni haki yako ukiikosa unaruhusiwa kwenda kushtaki.

Kuna nafasi ya mawaziri waangakie ni kwa namna gani uchumi wa kidigitali unaweza kushirikisha watu wote na hili linawezekana hata kwa kutenga maeneo ya intaneti za bure,'Julius Mnganga Mhariri wa Uchumi wa Gazeti la Mwananchi.

Screenshot_20230316_045851_OGInsta%2B.jpg
 
''Hadi sasa ardhi yenye ukubwa wa ekari milioni 1.63 imeridhiwa na Rais Samia Suluhu Hassan ili iweze kumegewa wananchi ambao sasa wataitumia baada ya kupangiwa mpango wa matumizi na kuondoa muingiliano baina yao na hifadhi zetu.

Kuna mgogoro wa Mbarali ambao umekuwa wa siku nyingi sana lakini umekwisha kwa mwaka huu, niwaombe watu wa Mbarali waheshimu kile ambacho Serikali imeelekeza, zoezi la uwekaji wa nukuu katika mipaka ile unaendela, lengo la Serikali ni zuri kuhakikisha kuwa tunatunza mazingira yetu vizuri.

Tunatunza vyanzo vya maji ili miradi ya kimkakati ikiwemo Bwawa la Mwalimu Nyerere lisiweze kukwama,''Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula.

Screenshot_20230316_045945_OGInsta%2B.jpg
 
''Changamoto kubwa ninayoiona katika sekta ya afya na inaniogopesha ni ongezeko kubwa la watu wenye magonjwa yasiyo ya kuambukizwa, kisukari, magonjwa ya moyo, shinikizo la damu na saratani.

Mzigo sasa umekuwa mkubwa sana, magonjwa haya kwa mfano mtu apate tatizo tu la ugonjwa sugu wa figo, akiambiwa asafishe damu awamu moja ni Sh200,000, daktari anamuambia walau fanya mara tatu Sh600,000, kwa mwezi ukifanya mara nne ni gharam kubwa.

Hili ni eneo ambalo tunakwenda kuongeza nguvu katika kuongeza huduma za kinga kwa sababu vingine ni vitu vidogo kwenye vyakula kama chumvi, sukari, mafuta mengi, mtu akiweza kupunguza chumvi, sukari, mafuta akazingatia ulaji wa mbigamboga na kufanya mazoezi na kula matunda tunaweza punguza magonjwa haya kwa kiasi kikubwa." Ummy Mwalimu Waziri wa Afya
Screenshot_20230316_050109_OGInsta%2B.jpg
 
''Kuhusu suala la Toto Afya Kadi tunaomba Watanzania wawe watulivu kwa sasa.

Miaka saba tangu kuanzishwa kwa bima ya TotoAfya Kadi ambayo tulilenga kutoa matibabu kwa watoto mwaka sifuri mpaka miaka 18 waliopo shuleni wamejiandikisha watoto zaidi ya 200,000 pekee na asilimia 90 ya hawa watoto wamekatiwa bima tayari wakiwa ni wagonjwa.

Hii imeondoa dhana ya bima ya afya, ambayo ni kuchangiana wanatakiwa watoto 100 wanaoweza kuwachangia wenzao 10 kama itakuwa tofauti hiyo bima haiwezi kuwa stahimilivu.

Nimewaagiza Mfuko wa Bima wa Taifa (NHIF) wakalimishe hili haraka, waweke mfumo rahisi ili tupate watoto wengi tuweze kujenga utaratibu wa kuwa na bima ya afya ili kufikia afya kwa wote.Tuwaache NHIF ndani ya wiki mbili wakamilishe hilI,'' Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu

Screenshot_20230316_050324_OGInsta%2B.jpg
 
''Tunakoelekea Watanzania wataacha kuhesabu vituo vya afya, zahanati, hospitali za rufaa za mikoa zilizojengwa na watadai huduma bora za afya na huo ndiyo uelekeo wetu sekta ya afya.

Tunapozungumza ubora wa huduma tunaangalia muktadha mzima tangu mgonjwa anafika katika kituo cha afya hadi anaondoka." Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Screenshot_20230316_050754_OGInsta%2B.jpg
 
'' Ili hii nchi iweze kutawalika na tuweze kusema demokrasia imeenda mbele, mabadiliko ya sheria zote kandamizi yaweze kufanyika.

Nilimsikiliza Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari anayehusika na vyombo vya habari alizungumza mwaka jana akasema ataleta muswada mapema wa mabadiliko ya sheria ya vyombo vya habari nikasikitika sana kuwa haukupelekwa bungeni.

Kuna sheria nyingine nyingi ambazo ni kandamizi, ushauri wangu ni kuwa ili tuweze kuwa na demokrasia kamili ni lazima tukubaliane sheria tulizonazo ziko kinyume na Katiba na nchi.

Ushauri wangu sheria ambazo ziko kinyume na Katiba ya nchi ziweze kufanyiwa maboresho ili tujenge Tanzania ambayo kila mmoja ataweza kujivunia kuwa Mtanzania'', Kumbusho Dawson Kagine
Screenshot_20230316_051127_OGInsta%2B.jpg
 
''Suala la afya ni mtambuka, japokuwa lina mazonge mengi, lina kelele nyingi na zinahitaji kuweza kushughulikiwa. Rais Samia Suluhu Hassan anapokwenda kutimiza miaka miwili madarakani Machi 19, 2023 amefanya mambo mengi.

"Rais ameonyesha jitihada kubwa kutekeleza ahadi za CCM za kuimarisha afya nchini, tumeona namna wanavyopambana ujenzi wa hospitali na ununuzi wa vifaatiba CT Scan, MRI. Tunahitaji kujua kwa changamoto zilizopo sasa wanakwenda kujipanga vipi kwa miaka hii miwili iliyosalia.

Juzi tumeona kuna mzozo wa bima ya afya kwa mtoto na kwa sasa hivi tunaona kulikuwa na mkwamo wa bima ya afya kwa wote. Tunahitaji kujua huduma za wajawazito na watoto hali ya huduma za afya iko vipi na katika kuajiri watumishi wa afya hali ikoje huko?,' Mhariri wa Habari Gazeti la Mwananchi- Lilian Timbuka
Screenshot_20230316_051255_OGInsta%2B.jpg
 
"Katika kipindi cha miaka miwili ya Rais Samia Suluhu Hassan, ahadi nyingi ameweza kuzitekeleza kwa kiwango chake, nchi ni kubwa na Watanzania wameshuhudia mengi na yote yanamtazama yeye.

"Tumeona ndani ya miaka hii miwili amefanya makubwa mengi alichokiahidi ndani ya miaka miwili na aliyoyatekeleza hatuna budi kumpa kongole.

"Amekwenda kwa hatua kubwa katika huduma za jamii katika sekta muhimu zinazomgusa mtu moja kwa moja.

"Sekta ya maji utekelezaji amekuwa akizungumza tangu alipoingia madarakani Machi 19, 2022 nia yake ya kumtua mama ndoo kichwani amefanikiwa lakini bado changamoto ni kubwa.

"Ripoti ya NPS ya mwaka 2021 kabla ya miaka miwili kulikuwa na kaya asilimia 40 zenye kupata maji safi na salama ndani ya miaka miwili ripoti ya Benki ya Dunia imeonyesha upatikanaji wa maji Tanzania imefikia kaya asilimia 61 zinapata maji ambapo ni sawa na ongezeko la asilimia 21 sawa na kaya tatu kati ya tano zinapata huduma ya maji.

"Bado kuna changamoto nyingi katika sekta ya maji, Waziri mwenye dhamana atuambie baada ya Machi 19 nini kitakwenda kufanyika kuondoa kero za maji, ndani ya miaka mitano wangapi watapata maji safi na salama." Lilian Timbuka- Mhariri wa Habari Gazeti la Mwananchi.
Screenshot_20230316_051713_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela mkazi wa Kongowe, Singbard Buchard na ndugu zake wawili baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumshambulia na kumdhuru mwili Rashid Mohamed na Anitha Rauyan.

Pia mahakama hiyo imeamuru washtakiwa hao kulipa jumla ya Sh1 milioni kwa ajili fidia ya maumivu waliyoyapata wakati waliposhambuliwa walalamikaji hao.

Akitoa hukumu hiyo hakimu Mkazi Mkuu, Evodia Kyaruzi alisema mahakama hiyo imetoa adhabu hiyo baada ya kuzingatia kuwa washtakiwa hao ni kosa lao la mara ya kwanza.

Kyaruzi alisema kitendo walichokifanya washtakiwa hao kwa kuwapiga, kuwatembeza mitaani na kuwafunga mikono walalamikaji hao inaonyesha ni zaidi ya kipigo hivyo haikubaliki kwenye jamii.

"Mtuhumiwa Singbard anasema Anitha ni mke wake hata kama alijihusisha na haya alitakiwa asichukue sheria mkononi kwa kumpiga mkewe kufanya hayo si sahihi,"alisema Kyaruzi.

Screenshot_20230316_051824_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela mkazi wa Kongowe, Singbard Buchard na ndugu zake wawili baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumshambulia na kumdhuru mwili Rashid Mohamed na Anitha Rauyan.

Pia mahakama hiyo imeamuru washtakiwa hao kulipa jumla ya Sh1 milioni kwa ajili fidia ya maumivu waliyoyapata wakati waliposhambuliwa walalamikaji hao.

Akitoa hukumu hiyo hakimu Mkazi Mkuu, Evodia Kyaruzi alisema mahakama hiyo imetoa adhabu hiyo baada ya kuzingatia kuwa washtakiwa hao ni kosa lao la mara ya kwanza.

Kyaruzi alisema kitendo walichokifanya washtakiwa hao kwa kuwapiga, kuwatembeza mitaani na kuwafunga mikono walalamikaji hao inaonyesha ni zaidi ya kipigo hivyo haikubaliki kwenye jamii.

"Mtuhumiwa Singbard anasema Anitha ni mke wake hata kama alijihusisha na haya alitakiwa asichukue sheria mkononi kwa kumpiga mkewe kufanya hayo si sahihi,"alisema Kyaruzi.

View attachment 2553217
 
Mkoa wa Kigoma umepokea waomba hifadhi ya ukimbizi 2,643 kutokana na machafuko yanayoendelea katika Mkoa wa Kivu, Kaskazini mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Akizungumza leo, Machi 15, 2023, Mratibu wa Kanda, Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Nashon Makundi amesema walipokea watu hao wachache walianza kuingia nchini Machi 5, Mwaka huu, huku wengine waliingia kuanzia Septemba 2022 hadi Januari 2023 na kujificha katika Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu na maeneo jirani ya kambi hiyo.

Makundi amesema watu hao wahawakuwa na taarifa sahihi kuhusiana na namna ya kuomba hifadhi nchini, huku wengi wakidhani nchi imefunga mipaka ya waomba hifadhi.

Amesema baada ya kujua mipaka ya nchi iko wazi na waomba hifadhi wanapokewa ndipo walianza kujitokeza kila mahali walipo na kuanza kuomba hifadhi kwani wengi walianza kuingia nchini na kuishi kinyume na taratibu za nchini.

Makundi amesema ilipofika Machi 10, 2023 idadi ya kuingia kwa watu hao ilikuwa ni kubwa ambapo wamekuwa wakipokea watu 300 hadi 600 kwa siku hadi wakati huo, huku hadi kufikia Machi 14 walipokea jumla ya waomba hifadhi 2,643.
Screenshot_20230316_052049_OGInsta%2B.jpg
 
Mwanamke aliyefahamika kwa jina Jessica Hawayu katika Kaunti ya Tana River nchini Kenya amenusurika kifo baada ya kumeza pete ya uchumba iliyokuwa imewekwa ndani ya pilau kwa ajili ya mchumba wake kumfanyia ‘sapraizi’.

Jessica aliokolewa na baba yake mzazi baada ya kupewa huduma ya kwanza kisha kuitema pete hiyo. Sherehe ya uchumba ya Jessica ilipangwa na familia yake kwa ushirikiano na mchumba wake Johanna Charo.

Tovuti ya Tuko ya nchini Kenya ilieleza kwamba sherehe hiyo ya kutoa mahari iliiingia dosari baada ya Jessica kumeza pete iliyokuwa imefichwa kwenye sinia la pilau, katika hali isiyo ya kawaida akajikuta ameichota kwenye tonge kisha kula na muda mfupi alikabwa kooni.

Hata hivyo, mchumba wake Johannah Charo alieleza kuwa kusudio lake ilikuwa kumfanyia ‘surprise' mchumba wake ili asijue ni jambo gani lilikuwa limewakutanisha kusherehekea siku hiyo.

Screenshot_20230316_052200_OGInsta%2B.jpg
 
Mkongwe wa kupiga gitaa la rythm kutokea nchini Congo, Lokassa ya M'bongo (80) amefariki dunia Jumanne usiku nchini Marekani baada ya kuugua muda mrefu.

Lokassa ambaye alikwa kiongozi wa bendi maarufu ya Soukous Stars alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari.

Lokassa atakumbukwa kwa nyimbo kali ambazo alishiriki kuziandaa na kupiga gitaa kama Bonne Annee, Monica, Marie-Josse na Assito

GENTAMYCINE natamani uje umuelezee kidogo hii sekta nakukubali sana nakumbuka kuna siku jukwaa la Entertainment nilikukuta unawaelezea wacongo siwakumbuki nilitamani tu uendelee kuwaelezea
Screenshot_20230316_052253_OGInsta%2B.jpg
 
Maombi ya Ofisa Habari wa timu ya Geita Gold, Hemed Kivuyo kutamani wakutanishwa na Yanga katika robo fainali Kombe la Azam Shirikisho yametimia baada ya droo hiyo kufanyika leo jijini Dar es Salaam.

Kivuyo alisema anatamani wakutane na Yanga kwasasbu mara nyingi wamekuwa wakiwaponyoka.

"Kama ikitokea hiyo bahati Yanga wameangukia kwenye mdomo wetu tena tunachezea kwetu tutashukuru sana," alinukuliwa Kivuyo.

Droo hiyo imefanyika leo na Geita Gold imepangiwa kucheza na Yanga katika robo fainali itakayochezwa jijini Dar.

Mechi mbili walizokutana katika Ligi Kuu msimu huu Geita imefungwa zotr (1-0 CCM Kirumba, Mwanza) na 3-1 katika Uwanja wa Azam Complex, Dar

Screenshot_20230316_052620_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mchengerwa amezindua boti ya utalii iitwayo Tawa Sea Cruiser katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara yaliyopo katika Mkoa wa Lindi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jana Machi 14,2023, Mchengerwa amewataka wananchi kutumia boti hiyo itakayounganisha shughuli za utalii katika Kanda ya kusini pamoja na ukanda wa Pwani ili kuendelea kukuza utalii wa ndani.

Boti ya Tawa Sea Cruiser yenye uwezo wa kubeba watalii 50 kwa mara moja, imelenga kuimarisha shughuli za usafirishaji wa watalii wanaotembelea katika Hifadhi ya Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara.

Screenshot_20230316_053055_OGInsta%2B.jpg
 
Maombi ya Ofisa Habari wa timu ya Geita Gold, Hemed Kivuyo kutamani wakutanishwa na Yanga katika robo fainali Kombe la Azam Shirikisho yametimia baada ya droo hiyo kufanyika leo jijini Dar es Salaam.

Kivuyo alisema anatamani wakutane na Yanga kwasasbu mara nyingi wamekuwa wakiwaponyoka.

"Kama ikitokea hiyo bahati Yanga wameangukia kwenye mdomo wetu tena tunachezea kwetu tutashukuru sana," alinukuliwa Kivuyo.

Droo hiyo imefanyika leo na Geita Gold imepangiwa kucheza na Yanga katika robo fainali itakayochezwa jijini Dar.

Mechi mbili walizokutana katika Ligi Kuu msimu huu Geita imefungwa zotr (1-0 CCM Kirumba, Mwanza) na 3-1 katika Uwanja wa Azam Complex, Dar

View attachment 2553221
Hayajatimia kwasababu hawachezei kwao, tusubiri kwanza, ili yatimie inatakiwa wachezee kwao (Nyamkumbu) Geita
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom