Makapuku Forum

Makapuku Forum

Serikali ya Uholanzi imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kuinua sekta ya kilimo cha mbogamboga ili iweze kuleta tija.

Akizungumza leo Alhamisi Machi 9,2023 katika uzinduzi wa programu iliyolenga kuinua na kukuza kilimo cha mbogamboga katika mikoa ya Kaskazini (Nohied), Balozi wa Uholanzi hapa nchini,Wiebe De Boer amesema wataendelea kushirikiana na Tanzania hasa katika sekta hiyo ili izidi kukua na kuongeza uchumi.

"Mradi huu utasaidia elimu inayotolewa kwenye vyuo vya ufundi kuakisi mazingira ya kisasa na kuwajengea wahitimu stadi husika za ujasiriamali ambapo pia tutashirikiana na Chuo cha mafunzo ya kilimo, mbogamboga, maua na matunda cha Tengeru," amesema.

Screenshot_20230310_050312_OGInsta%2B.jpg
 
Klabu ya Vipers ya Uganda imemfuta kazi Kocha wake, Beto Bianchi uamuzi ambao umetangazwa leo bila kutaja sababu ya kufikia maamuzi hayo.

Bianchi raia wa Brazil ameiongoza Vipers kwa siku 58 tangu Januari 11,2023 alipotangazwa kuwa mrithi wa Mbrazil mwenzake Roberto Oliveira 'Robertinho' ambaye alitimka klabu hiyo na kutua Simba.

Tangu apewe kibarua cha kuiongoza Vipers, Bianchi hakufanikiwa kushinda mchezo wowote katika mechi tano alizoiongoza timu hiyo.

Mpaka anaondoka Bianchi ameshindwa kuiona Vipers ikishangilia bao lolote kwenye mechi ya mashindano baada ya timu hiyo kushindwa kufunga kwenye mechi tano alizoiongoza huku ikiruhusu jumla ya mabao 7.
Screenshot_20230310_050421_OGInsta%2B.jpg
 
Yanga Princess imeendeleza uteja kwa Fountain Gate Princess ikifungwa tena leo bao 1-0 katika mzunguko wa pili Ligi Kuu ya Wanawake. Katika mzunguko wa kwanza Yanga Princess ilifungwa uwanja wa nyumbani bao 1-0.

Simba Queens ikiwa ugenini katika uwanja wa Jenerali Isamuyo imeikomalia JKT Queens kwa kutoa sare ya bao 1-1 wakifuta kumbukumbu ya kufungwa mzunguko wa kwanza.

Screenshot_20230310_051032_OGInsta%2B.jpg
 
WAKATI vigogo waliowahi kuongoza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakifichua kwamba sakata la Feisal Salum ‘Fei Toto’ linacheleweshwa na mchezaji mwenyewe na TFF haiwezi kulimaliza bila kuwepo kwa mazungumzo ya mchezaji na klabu yake, wameeleza kama Yanga italazimika kumuuza, basi dau lake halitazidi Sh 400 Milioni.
Baadhi ya makatibu wakuu wa TFF kwa nyakati tofauti, Selestine Mwesigwa na Aden Rage (wakati ikiitwa FAT) kwa nyakati tofauti wamefichua kwamba, wanaomshauri Feisal ndiyo tatizo kwenye sakata hilo ambalo ni jepesi na mchezaji huyo hazuiwi kuondoka.

Rage alisema, Feisal kuingiza Milioni 100 kwenye akaunti ya Yanga halikuwa suluhisho la yeye kuondoka kwani hajui klabu inataka nini.

Alisema Feisal anapaswa kuwa mkweli kwa Yanga, aeleze ni klabu ipi anahitaji kwenda na Yanga haiwezi kukataa kumuuza akifafanua kwamba dau lake halitakuwa zaidi ya Sh 400 milioni.

“Kama wakati anasainishwa ilikuwa ni milioni 100, sasa thamani imepanda haitokuwa chini ya milioni 350 hadi 400 kwa klabu inayomtaka kumnunua, Yanga wakiweka hesabu za ajabu, Fifa wanaweza kuingilia na utaratibu huko hivyo,” alisema Rage.

Screenshot_20230310_051214_OGInsta%2B.jpg
 
Mtazamo wa kenny_mchambuzii

Nawarudisha nyuma kidogo ikiwa leo ni Throwback Thursday, Klabu ya Yanga ilifanikiwa kumtanbulisha mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele kuwa mchezaji wake mpya.

Katika msimu wake wa kwanza tu ndani ya Yanga Sc katika ligi kuu alifunga magoli 16 na kuwa namba mbili huku kiatu cha mfungaji bora ikichukuliwa na George Mpole.

Msimu huu unavyoanza hakuanza kwa kufunga sana, hii inachangiwa na uchovu kwa kiasi kikubwa kutokana na kutumika sana msimu uliopita na kuisadia Yanga Sc kubeba Ubingwa wa Ngao ya Jamii,Ligi Kuu na Fa.

Gari lilivyoshika moto kwa Mshambuliaji mambo yakabadilika ghafla na kuanza kufunga na kuwa katika kiwango bora sana.

Fiston Kalala Mayele kwa sasa ndio Mshambuliaji wa mfano katika Ligi yetu, Umbo lake,anajua kukaa kwenye nafasi,ni ngumu kumnyang'anya mpira na ana jicho la kuona goli la wapinzani wake.

Mpaka sasa katika Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu tayari ana magoli 15 huku anayemfatia (Saido na Phiri) wakiwa na magoli 10 kila mmoja.

Wakati Mwamba wa Umalila @baraka_mpenja akimpa Fiston Mayele jina la (KING) Mayele hakika Ufalme wa Mayele unaonekana.

Jicho la @caamil_88 na jopo la SCOUTS waliohusika kumleta FISTON MAYELE Yanga Sc kwa hakika wameonyesha ukubwa wa Yanga Sc na sasa Wananchi wanafurahi.

Kipindi cha nyuma Yanga Sc walikua na Washambuliaji lakini viwango vyao havikuridhisha na ngumu kumaliza Ligi wakiwa na magoli 15+ lakini kwa sasa wamepata mtu haswa na aliyekata kiu yao kwa muda mfupi.
Screenshot_20230310_052108_OGInsta%2B.jpg
 
VIPERS YATIMUA KOCHA

Klabu ya Vipers imempiga chini Kocha Beto Bianchi kutokana na mwendelezo wa matokeo mabaya tangu Kocha huyo alipotangazwa kuchukua nafasi ya Kocha Robert Oliveira ambaye alijiunga na Simba.

Bianchi alitangazwa Januari 10, 2023 na katika majukumu yake amekiongoza kikosi cha Vipers kwenye jumla ya mechi saba (7) za mashindano tofauti.

Katika mechi saba (7) ambazo Bianchi alikuwa kwenye benchi la Vipers, timu hiyo haijashinda mchezo wowote wala kufunga goli ndani ya dakika 90!

CAF Champions League
Simba 1-0 Vipers
Vipers 0-1 Simba
Vipers 0-0 Horoya AC
Raja Casablanca 5-0 Vipers

Uganda Premier League
Vipers 0-0 Wakiso Giants

Stanbic Uganda Cup
Jinja North UTD 0-0 Vipers [Pen 6-7]
Bujumbura United 0-0 Vipers [Pen 1-4]

Mechi 7
Ushindi 0
️ Magoli ya kufunga 0
Magoli ya kufungwa 7
Screenshot_20230310_052313_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

INTRODUCTION TO TRIPLE C! WHAT IS CCC?

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)

Advance Certificate of Secondary Education Examimation (ACSSE)

EXAM: GENERAL STUDIES (GS)

1. What is CCC?

- Ni jina la Mwanasoka bora wa muda wote kuwahi kutokea Tanzania kwa maili nyingi mbali, CCC ni kifupisho cha maneno matatu ya Kiingereza ama Lugha ya Malkia.

C- FOR CLASS, hili ni darasa huru la mpira Tanzania kazi yake ni kuelekeza kwa vitendo nini maana ya Kiungo wa mpira, nini maana ya kucheza soka kwa ajili ya furaha ya Binadamu wa dunia ya tatu ambapo hatuna furaha sana.

Darasa hili linataka uwe na viatu vya mpira, ukae mbele ya TV ulipe 500 yako mbele ya visimbuzi vya AZAM au decorder za DSTV! Piga kelele wakati anafundisha kwakuwa darasa hili halina Monitor.

C FOR CLASS, wana msemo maarufu kuwa “Form is temporary but Class is permanent” wamesahau maneno na hawatukuzi ishara! Assists 14 kwenye ligi kuu na mabao kwenye Champions League! Hawasemi hawoangei na wala hawatikisiki.

This is Clatous Chama na ndie muda wote anaamua yeye kwa ajili ya wote, Football vitamin hii wala haina mipaka, Simba walimleta kwa ajili ya Watanzania wote.

C FOR CHAMBUZI, karibu Tanzania! Karibu kwenye nchi ya Uchambuzi, wakisema yupo slow anawakumbusha hata Kinyonga anaishi dunia hii hii ya kukimbizana, as simple as you like! Anadhihirisha ukuu wa Mungu alivyotuumba watu wake kila Mtu na kitu chake.

Chama hafai kwenye mpira wa kisasa? Rejea clip ya bao la jana! Chama hafit kwenye mfumo wa Mwalimu? Well Mwalimu yupo kwenye mfumo wake sasa na anampeleka hatua za mtoano, chukua hii!

This is CLATOUS CHOTA CHAMA, the Greatest is, the greatest was, the Greatest will ever be! THE GREATEST EVER TO DO IT, mkitaka namba tunawapa na mkitaka burudani tunawapa! Anything else?

Mchezaji bora wa muda wote by miles away, this case is closed you know! Hivi vitu ni gharama sana you know!

Photo @rabbihume

Screenshot_20230310_052556_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

NASREDINE MOHAMED NABI, niliitazama picha hii kutoka kwenye mazishi ya mtoto wa Mchezaji wako tegemezi kwa aina yako ya mpira, Salum Abubakar Sureboy ambaye amefiwa na huyo mtoto uliyembeba kuelekea makaburini pale Magomeni Mapipa.

Uliwahi kuongea na Sir Alex Ferguson? Hapana sidhani! Uliwahi kumsoma sana Babu Fergie? Yes hilo nina uhakika nalo Profesa Nabi! Aliwahi kusema Mskochi yule kuwa “One thing about football is not about football” kitu kimoja kuhusu mpira wa miguu wala hakihusu mpira wa miguu.

Profesa hana Kiungo wake Feisal Salum lakini akaamua kubadilika kulingana na rasilimali alizonazo ndani, maisha yakaendelea na kila ulipoulizwa kuhusu Feisal ulijibu ni Mwanao unammiss lakini unamtakia heri kwenye maisha yake.

What is Wisdom Profesa? Ni kuelewa kuwa kitu kimoja kuhusu mpira wa miguu wala hakihusu mpira, ukatenga muda wako kwa ajili ya mazishi ya Mtoto wa Mchezaji wako lakini bado ukampa nafasi ya kupumzika kufuatia msiba huu mzito kwake.

Ni Profesa Nabi, ndani ya saa 24 zijazo alikuwa na mechi ya kiume sana lakini anakubali Kiungo kama Sureboy asalie nyumbani kwasababu za kifamilia, halafu anabadili mfumo kuendana na familia iliyopo Jangwani, can you imagine?

Kauchapa mpira mwingi wa hesabu bila engine zake mbili, moja ipo Umrah lakini maisha yanaendelea, mmoja yupo nyumbani anaomboleza na maisha yanaendelea kwa heshima ya vitabu vyake vya Ukocha na uchawi wa kimbinu, kwa Prof ni mfumo kisha Mchezaji, I love that.

Profesa ni muungwana na Allah hakumtupa! Kila alichoshika leo kiligeuka kuwa mkate! Alimtoa Aziz Ki, alimtoa Tuisila Kisinda kisha Ducapel Moloko na Khalid Aucho wakaja kuimaliza mechi yake, malipo ya muungwana ni ndani ya uungwana wake.

What is wisdom Prof? Ni uungwana huu wa kuelewa kitu kimoja kuhusu mpira wala hakihusu mpira, hongera sana Prof!

Screenshot_20230310_052701_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom