Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20221204-052519_Opera%20Mini.jpg
 
DOKTA KASEMA NEYMAR ANACHEZA
.
Daktari wa Timu ya Taifa ya Brazil Rodrigo Lasmar amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo baada kufichua kuna uwezekano Neymar akawepo uwanjani kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora za Kombe la Dunia 2022 dhidi ya Korea Kusini kesho Jumatatu.
.
Kulikuwa na wasiwasi Neymar atakosa fainali zote huko Qatar, lakini daktari Lasmar amesema staa huyo na Alex Sandro wote wana nafasi kucheza.
Screenshot_20221204-075659_Instagram%20Lite.jpg
 
Kijana Albert Mrema ambaye alinusurika katika ajali ya gari iliyosababisha vifo vya Mama na Wanawe wawili na akawa amelazwa ICU Hospitali ya Mloganzila, nae amefariki dunia, Albert ndiye alikuwa Dereva wa gari hilo ambalo liliacha njia na kuingia Barabarani na kifo chake kinafanya Familia hiyo sasa kuwa imempoteza Mama na Wanae watatu.

Ajali hiyo imetokea Jumamosi iliyopita maeneno ya Kibamba na kusababisha vifo vya Watu watatu, Immaculata Byemerwa (49) ambaye ni Mama pamoja na Watoto wake Jolister Byemerwa (17), aliyekuwa anafanyiwa sherehe ya mahafali siku hiyo na Janeth Byemerwa (20), Mwanafunzi aliyekuwa anasoma mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Albert Mrema ambaye alizaliwa mwaka 1994 alikuwa Mtoto wa kwanza wa Immaculata kabla ya kufunga ndoa na Mhandisi Josephat Byemerwa, Baba wa Familia ambaye alifariki dunia mwezj May mwaka jana na sasa mwaka mmoja tu baada ya kifo chake Mkewe na Watoto watatu nao wamefariki.
Screenshot_20221205-040328_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20221205-040346_OGInsta%2B.jpg
 
Watu wanne waliotuhumiwa kuifanyia kazi Idara ya Ujasusi ya Israel, Mossad, wameuawa hii leo na Mamlaka za Iran baada ya kuhukumiwa kifo, hii ni kwa mujibu wa @dw_kiswahili.

Shirika la Habari la Taifa la Iran (IRNA) limeripoti kuwa Watuhumiwa wengine watatu wamehukumiwa kifungo cha maisha jela.

IRNA imesema Jeshi la kimapinduzi lenye usemi mkubwa nchini Iran lilitangaza kuwakamata Watu wa mtandao unaohusishwa na idara hiyo ya ujasusi ya Israel kadhalika jeshi hilo lilisema Watu waliokamatwa waliwahi kuwa na rekodi za uhalifu na walikuwa wakijaribu kuuvuruga usalama wa nchi.

Kwa mujibu wa ripoti ya Iran, Wanachama wa mtandao huo walihusika kuiba na kuharibu mali za Watu binafsi na za umma pamoja na kuwateka nyara Watu na kuwahoji, Iran inadai pia Watuhumiwa hao wa ujasusi walikuwa na silaha na walikuwa wakipokea malipo kutoka Mossad kwa njia ya sarafu ya mtandaoni.
Screenshot_20221205-040458_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara, imemuhukumu kifungo cha miaka 15 Jela Mkazi wa Kata ya Chikonji Mkoani Lindi, Omari Salum Hamisi (21),baada ya kukutwa na hatia ya kumuua Mke wake, Nasra Selemani (20) kisa alimfumania na Mwanaume mwingine (Mchepuko).

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji wa Mahakama hiyo, Dkt. Eliamini Issaya Laitaika, baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na mwenyewe kukiri kosa la kuua lililokuwa linamkabili.

Hamis alitekeleza mauaji hayo baada ya kutomkuta nyumbani Mke wake na alipomfuatilia alimkuta na Mchepuko ambaye alikimbia mara baada ya kuwakaribia, na alipomuhoji Mkewe alishindwa kujitetea ndipo ugomvi ulipoanza na kumchomoa kisu tumboni na kusababisha kifo chake.
Screenshot_20221205-040559_OGInsta%2B.jpg
 
Bunge la Indonesia linatarajiwa kupitisha baadhi ya marekebisho ya sheria mpya za makosa mbalimbali ya kihalifu ikiwemo kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kufanya ngono nje ya ndoa.

Marekebisho hayo ya sheria yatahusisha pia kosa la kuishi na Mume au Mke bila kufunga ndoa, kumtusi Rais au Taasisi za Serikali pamoja na kutoa maoni yoyote yanayokinzana na itikadi ya Serikali ya Indonesia.

Naibu Waziri wa Sheria nchini Indonesia, Edward Omar Sharif Hiariej amethibitisha kufanyika kwa marekenisho hayo ya sheria katika kuboresha kanuni na adhabu dhidi ya makasa ya kihalifu yanayopishana na maadili ya nchi hiyo ambapo mpaka kufikia tarehe 15 desemba mwaka huu, Bunge la chini hiyo litapitisha miswada mbalimbali ya sheria hizo.

Baadhi ya mabadiliko ambayo yatafanywa ni pamoja na kifungu cha sheria kinachoweza kuruhusu adhabu ya kifo kubadilishwa na kuwa kifungo cha maisha na kuharamishwa kwa utoaji mimba, isipokuwa waathiriwa wa ubakaji.
Screenshot_20221205-040906_OGInsta%2B.jpg
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Philip Mpango, kupitia Mkutano Mkuu wa 22 wa Sekta Binafsi Tanzania (Tanzania Private Sector TPSF) amemkabidhi Mkurugenzi Mtendaji (CEO) wa @silent_ocean_ltd Salaah Said Mohamed (@counsellorsalaah) tuzo ya ubora kwa usafirishaji kwa Kampuni za Silent Ocean na Kilimanjaro Star Cargo.

TPSF imetambua mchango wa Silent Ocean na Kilimanjaro Star Cargo katika kusaidia ukuaji wa Uchumi kwa Wafanyabiashara wa ngazi zote Tanzania ambapo zote kwa pamoja Silent Ocen Ltd na Kilimanjaro Star Cargo zina uzoefu wa miaka 18 ya ubora wa usafirishaji kwa njia ya bahari.
Screenshot_20221205-041330_OGInsta%2B.jpg
 
UFARANSA WANATINGA ROBO KIBABE !!
.
FT: FRANCE 3-1 POLAND
️ Giroud 44’
️ Mbappe 74’, 90+1’
️ Lewandowski (pen) 90+9’
Screenshot_20221205-041439_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kuna The Butcher pale Argentina watu hawamzingatii sana kwakuwa yupo Lionel Messi, kuna Bruno na Bernardo Silva pale Ureno ila kivuli cha Ronaldo kimewazidi nguvu, kulikuwa na Karim Benzema pale Madrid kwenye kivuli cha Ronaldo.

Hata pale Simba kuna Mzamiru Yassin anaishi kwenye kivuli cha Wachezaji wengine, ni ngumu kumtaja, ni ngumu kumzungumza kwakuwa huenda sio wa kanzu na tobo wala vyenga vingi.

Anaitwa Mzamiru Yassin ni ukimya kwenye kelele, ni cocktail yenye alcohol sifuri, ni Kiungo wa mpira kwenye dunia hii ya show game, bahati mbaya huenda Mzamiru hauzi headlines wala trend……

Sio kwamba hatukuoni Homeboy ila wakati mwingine taaluma ya habari ni Unfair kidogo kwenye issue ya PROMINENCE.

Screenshot_20221205-041731_OGInsta%2B.jpg
 
Jemedari Said

BOSS wa Silent Ocean Kampuni inayoidhamini Tanzania Prisons akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Yanga SC (picha sio ya leo)

Leo timu anayoidhamini (Tanzania Prisons) inacheza na Yanga SC na ametoa ahadi iwapo Prisons itaifunga Yanga basi watapata 20M na wakitoka sare watapata 10M.

TFF wanatakiwa kufanya homework yao vizuri sana na bahati mbaya hawafanyi. Wao kama mamlaka ya kusimamia mpira wana majukumu makubwa ambayo aidha hawayajui au wanayajua ila hawawezi kuyasimamia kwa sababu wanazozijua wenyewe.

Silaumu mfanyabiashara yoyote kutafuta kutangaza biashara yake kupitia kilabu chochote, lakini TFF ndiyo wanapaswa kupanga vitu viweje kwa maslahi mapana ya mpira wetu ili kuondoa shakashaka.

Vinginevyo itafika wakati watu hawatoamini tena kwamba vilabu vyetu vinapata ushindi wa HALALI.

TFF amkeni kwenye usingizi wa PONO choreni mistari kipi kinaweza kufanyika na kinafanyikaje na kipi HAKIWEZEKANI.

Let you guys set standards for our football for fair competition
Screenshot_20221205-041852_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Acha niwape kisa kimoja kuhusu Ndugu wawili nyuma ya ADIDAS na PUMA, Yes ni Ndugu wawili kama ilivyo kwa Salaah wa Silent Ocean na Gharib wa GSM, mmoja alikuwa anaitwa Adolf na mmoja anaitwa Rudolf maarufu kama THE DASSLER BROTHERS, acha niwape kisa.

Hawa Ndugu wawili zamani kabla ya vita ya pili ya dunia walikuwa na Kampuni yao inaitwa GEDA, waliendesha kwa pamoja kabla ya kufikia 1948 ambapo walipishana kwasababu mbalimbali na kila mmoja akaanzisha Kampuni yake.

Adolf akaanzisha kampuni ya ADIDAS iliyotokana na jina lake Adolf Dassler na mdogo wake akaanzisha kampuni ya PUMA na kuiita jina la Mnyama, biashara yao ya mapambano ilianzia hapo na hawakupikika chungu kimoja inapokuja suala la maslahi.

Turejee kwenye issue ya SILENT OCEAN ambao wao wamewekeza mzigo wao pale Prisons na GSM wameweka mzigo wao pale Yanga, licha ya kuwa ni Ndugu lakini hizi ni biashara, ni zaidi ya undugu na Ushabiki wao.

Mzee wangu Jemedari ameandika kitu kuhusu INTERGRITY, lakini hakuna sehemu duniani kwenye dunia ya kitaasisi ikapimwa kisa Undugu, hakuna hata mmoja kati ya hao ndugu wawili anayetaka kufeli kwenye biashara zake, amini hilo.

Una hofu na Silent Ocean? Wangewekaje Million 20 kama Prisons watamfunga Yanga? Remember dhidi ya Simba aliahidi Million20 pia! pesa ambayo aliahidi ushindi kama Prisons atamfunga Simba leo imekaa tena palepale, una hofu mpaka hapo? Na ahadi ni mpaka mechi tofauti na Kariakoo isipokuwa dau tofauti.

TFF hawana room ya kuingilia hii kwakuwa ni battle hii, ni pesa hapo imewekwa! Licha ya kuwa wao ni Ndugu sisi watu wa mpira tunawaona ni Washindani na ndio maana Silent hayupo popote kwenye jezi ya Yanga, wao wana utawala wao na GSM wana utawala na mfumo wao.

Salaah anaweza kuwa Yanga kama ambavyo President Karia ni Coastal, Mimi ni Simba, Javier Tebas ni Madrid lakini anaongoza LA LIGA, Ushabiki wa Mtu hauwezi kuathiri kazi, mapenzi na kazi ni vitu viwili tofauti mno, ndio maana hata Rais wa nchi anaweza kupangiwa cha kufanya na Watu wake kwakuwa ni mfumo unawaongoza.

Halafu kwenye dunia ya ushindani, mara nyingi Ndugu hukamiana sana kuliko kawaida.

The corporate world, works differently from streets.
Screenshot_20221205-043710_OGInsta%2B.jpg
 
Timu ya taifa Ufaransa imeiondosha Poland kwenye Fainali za Kombe la Dunia 2022 baada ya kuilaza mabao 3-1, mchezo uliochezwa Uwanja wa Al Thumama.
Ufaransa imetinga hatua ya robo fainali huku ikisubiri mshindi kati ya England dhidi ya Senegal.

FT: Ufaransa 3-1 Poland
️' Giroud
️' Mbappe
️' Lewandowski

Screenshot_20221205-044621_OGInsta%2B.jpg
 
Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons, mechi iliyochezwa uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Bao la dakika za mwisho katika mchezo huo lililofungwa na kiungo Feisal Salum akipokea pasi ya Farid Mussa limetosha kuihakikishia ushindi mbele ya Wajela jela hao.

Bao hilo pekee la 'Fei Toto' linawakosesha Prisons kitita cha Sh20 milioni kutoka kwa wadhamini wao Silent Ocean walichoahidiwa endapo wakipata ushindi au ikitoka sare na Yanga wangepata sh10 milioni.

Yanga imepanda kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu NBC na pointi 35 baada ya mechi 14.

FT: Yanga 1-0 Tanzania Prisons
Feisal.
Screenshot_20221205-044718_OGInsta%2B.jpg
 
Ndoto za Kocha Aliou Cisse kuiongoza Senegal kutinga hatua ya robo Fainali katika Kombe la Dunia kama alivofanya 2002 akiwa na kitambaa cha unahodha zinefeli baada kuondoshwa na England kwa mabao 3-0.
England imefanikiwa kuingia robo fainali na itakutana na Ufaransa katika hatua hiyo.
Senegal ndio timu ya kwanza ya Afrika iliyofungua hatua hii katika mchezo wa leo lakini mambo hayajaenda kama walivotamani hivyo muwakilishi pekee wa Afrika aliyebaki katika fainali hizo ni Morocco ambapo atacheza na Uhispania Disemba 6.

FT: England󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 3-0 Senegal
️' Henderson
️' Kane
️' Saka.
Screenshot_20221205-044808_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom