Makapuku Forum

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. John Dodoma, Winfrida Michael (24), aliyekuwa anasoma Diploma ya Medical Laboratory amefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa kuchomwa kisu na Mpenzi wake, Julius Gervas (26), RPC Dodoma Martin Otieno amethibitisha .

Winfrida alifariki wakati anapelekwa Hospitali baada ya kuwa amevuja damu nyingi na Julius baada ya kufanya tukio hilo alijaribu kujichoma kisu tumboni lakini Watu walimuwahi na kumchukua kisha kumpeleka Hospitalini ambako anaendelea na matibabu chini ya ulinzi.

Inaelezwa kuwa Winfrida alikuwa amepanga nje ya Chuo na alikuwa na mahusiano na Kijana huyo kwa muda fulani lakini walikuwa wameachana na Kijana alikuwa anamsumbua Msichama hivyo alimuahidi kuwa akimaliza mtihani atamjulisha.

Juzi Msichana alikuwa amemaliza mtihani wake wa mwisho na kwa mujibu wa Mama mwenye nyumba walikutana wakaongea sana pale ndani na ilipofika saa nne na nusu walitoka nje akawa anamsindikiza ndio lilipotokea tukio la kuchomwa kisu na akawa anaomba msaada na walimchukua na kumpeleka Hospitali lakini akawa amefariki, mwili wa Marehemu umeagwa na kusafirishwa kwenda Ukerewe kwa mazishi.
 
Hamna mtu wa kujiua humu 😂🤣
 
Kampuni ya MeTL Group ya Tanzania na Panasonic Life Solutions ya India wametangaza muungano wa kuuza bidhaa za umeme nchini Tanzania muungano ambao unakusudia kunasa soko jipya ambalo linaangalia ubora wa bidhaa za umeme.

Mkurugenzi wa Masoko wa METL, Bi. Fatema Dewji akiikaribisha Panasonic India alisema Kampuni hizi mbili zinaamini katika kutengeneza ulimwengu bora kwa Wateja “Panasonic inasimamia maisha bora, Ulimwengu bora’ na sikuweza kuona kauli mbiu bora zaidi inayofanana na inayokamilisha "kugusa maisha ya Watu".

Akizungumza katika hafla hii, Vishal Nangalia San, Mkuu wa Biashara ya Mauzo ya Bidhaa wa Panasonic Life Solutions India alisema “Tunayo furaha kushirikiana na METL Group inayoongoza jumuiya ya biashara ya Afrika Mashariki na tunatarajia mafanikio ya kusisimua.

Aidha Mkurugenzi wa Mauzo wa MeTL, Hussein Dewji amesema ushirikiano kati ya METL na Panasonic ni wa kihistoria hapa nchini unaolenga kumsaidia Mtanzania wa hali ya kawaida kupata bidhaa za Panasonic kwa urahisi, uharaka na kwa bei nafuu kokote nchini.
 
Huyu ndie Princess Diana, sasa hivi ndie angekuwa Malkia.

Sio pesa wala ukuu unaoweza kufanya ndoa yako idumu, bali heshima na upendo. Kama ungekuwa ukuu au pesa basi ndoa ya Diana na Charles isingekufa. Princess Diana alikutana kwa mara ya kwanza na Prince Charles akiwa binti mdogo kabisa mwenye umri wa miaka 16, wakati huo Prince Charles alikuwa anatoka na dada yake Diana. Diana alimpenda Charles, wakafanya mafekechee wakazama penzini japo kwa siri. Baadae wakahalalisha mahusiano yao na kufunga ndoa mwka 1981, Diana akiwa na miaka 20.

Sio kwamba Diana alitoka katika familia isiyokuwa na heshima, hapana, familia yake ni mojawapo ya familia zenye hadhi ya juu nchini Uingereza. Baada ya ndoa Diana alikuwa ni mwanamke wa Tatu mwenye heshima nchini Uingereza, baada ya Malkia na Mama yake Malkia.

Licha ya ukuu aliokuwa nao lakini Princess Diana hakuwa na furaha kwenye ndoa yake. Mume wake kuwa na mahusiano ya nje ilimtesa sana Diana. Mimba ya mtoto wake wa kwanza ikiwa na wiki 12, Diana alijirushwa kutoka kwenye ngazi na kuanguka, hata hivyo mimba haikurabika. Diana alisema alifanya hivyo kwa sababu alikuwa mpweke sana. Baada ya kujifungua mwanae wa kwanza Diana aliugua ugonjwa wa Sonona.

Baada ya miaka 5 ya ndoa kulikuwa na migogoro mikubwa sana ambayo haswa ilichangiwa na tofauti ya umri. Diana alikuwa na mchepuko wake wakati huo mumewe pia mahusiano yake na Camilla yalikuwa yamenoga. Migogoro na utofauti iliendeleq kukuwa na kupelekea ndoa yao kuvunjika miaka 15 baadae.

Akizungumza na mwandishi wa BBC, Diana alisema waliamua kutengena kwa sababu mahusiano yao yalikuwa kama ofisi ya umma, siku hizi mnasema Azam Burudani kwa Wote. Pia Diana alisema alikuwa ana mashaka sana kama Prince Charles alikuwa anafaa kuwa Mfalme wa Uingereza.

Baada ya kutengana Princess Diana alinasa kwenye penzi zito la mtoto wa Kiarabu, penzi lao halikudumu sana. Princess Diana alifariki dunia kutokana na majeraha aliyopata kutokana na ajali ya gari. Alifariki mwaka 1997, ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kutalakiana na Charles. Princess Diana alifariki akiwa na umri wa miaka 36, katika ndoa yao walibahatika kupata watoto wawili ambao ni Prince William na Prince Harry.
 
Sasa akifa huyo chalz nani atakuwa mfalme wakati hajazaa!?
 


FOOTBALL ECONOMY || Mishahara

.
Kwa mujibu wa kijana mwenzetu @kenedymosestz huo ndio mpangilio wa mshahara wa Mchezaji wa Yanga Fiston Mayele baada ya kusaini mkataba mpya.
.
Nami nimeingia mzigoni ili kujua malipo ya wachezaji wanaocheza ligi kuu na ligi ya Championship. Nitawajulisha nani analipwa sana na nani analipwa kidogo kutoka vilabu vyote.
.
Nitawajulisha mzawa gani anakula pesa ya kutosha na nani anakula Pesa kiduchu na kisha kuwaletea bajeti ya mishahara ya klabu kwa ujumla na kadirio la matumizi kwa msimu.
.
Che Guevara

.
NB:
Kuna timu zitakwambia mshahara ni siri
.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…