Makapuku Forum

Mtoto Jovin Simon (10) Mkazi wa Mtaa wa Elimu Wilaya ya Geita amefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa kupigwa na teke tumboni na Haruna Amini (16) Mkazi wa Mtaa wa Elimu.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Ally Kitumbu amesema Jovin alifariki dunia wakati akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Geita huku akisema chanzo cha tukio hilo ni ugomvi kati yao wawili .

"Huyu Mwanafunzi alikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita na alifariki dunia wakati akiendelea na matibabu na kiini cha tukio ni ugomvi mwili umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya uchunguzi wa Daktari”

Aidha Kaimu Kamanda amewaomba Wazazi kuhakikisha wanawakanya Watoto wao kucheza michezo isiyokuwa na staha wawapo majumbani na kusema mwili wa Mtoto huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Geita.
 
Mtoto Simon Seleman anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 11-13, Mwanafunzi wa darasa la nne Shule ya Msingi Ligundo amefariki dunia baada ya kugongwa na gari katika Kata ya Lulembela barabara ya Ushirombo Wilayani Geita.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Ally Kitumbu amesema Dereva wa gari lenye namba T.152 DMB. Khamis Daniel (33) Mwalimu Mkazi wa Kijiji cha Lulembela amemgonga Mwanafunzi huyo ambaye alikuwa akiendesha baiskeli na kumsababishia majeraha sehemu za mwili hali iliyopelekea kufariki dunia.

Kamanda Kitumbu amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa Dereva wa gari huku akisema mara baada ya kijana huyo kugongwa alikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Geita kwa matibabu lakini kwa bahati mbaya amefariki dunia akiwa anaendelea na matibabu.
 
Sasa wakosee wao, mwingine ashtakiwe!! Huu ni uonevuuu 🤣🤣🤣🤣
 
Huyu kiumbe wanamkosea sana aiseee....

Wampakazie watakavyoweza... ila sikomi...

Kuna mtu aliniambie mafuta yake ndiyo kiboko sasa.. kupikia mboga za majani na kukaangia chipsi Auntie
unaambiwa utajilambaaaa...
 
Na uroho wangu wotee hii nyama imenishinda haipiti hata
Dooh pole sana

Lakini sikushangai mwaya maana hata mimi pamoja na watu wengi kupenda nyama ya mbuzi ila mie ile nyama imenishinda kabisaaa sijawahi kuipenda yani

Mimi kwenye mdudu, ng'ombe, kuku na samaki (wenye magamba tu lakini) yani hapo ndio umenifikisha
 
Ndio mimi kwa kitimoto yaani nitakufa na njaa yangu
 
Kwanini kila siku Ufaransa? Baada ya sakata zito la Mathieu Valbuena na Karim Benzema, juu ya mkanda wa ngono ambapo inasemekana Benzema alihusika kumtapeli Mathieu, ikaigawa timu ya taifa ya Ufaransa.

Sasa ni zamu ya Paul Pogba na Kylian Mbappe, baada ya Kaka yake Pogba kusema Mdogo wake anatumia Mwalimu wa diin ya Kiislam kumroga Kylian Mbappe.

Didier Deschamps ana miezi miwili tu kuelekea Qatar na tayari mezani ana jambo zito kama Kocha.
 
Makocha waliopoteza ajira zao baada ya kufungwa na Jurgen Klopp wa Liverpool.

Guidolin (Swansea)
Bilic (West Ham)
Jokanovic (Fulham)
Mourinho (United)
Silva (Everton)
Parker (Bournemouth)

Chelsea mnasemaje
 
Shaffih Dauda

Yanga wapo zao Avic Town, wanapambana kujiweka fit kuelekea michuano ya ndani na ya kimataifa, wanaamini Avic ni sahihi kwao.

Ni hapo hapo Avic paliwapa Premier League, FA Cup na Ngao mbili, wameendelea kupaamini wala hakuna tatizo kwakuwa ni chaguo lao na pendekezo lao.

Binafsi naamini Yanga kwasasa wanalihitaji zaidi taji la Premier, taji la FA na Ngao kwakuwa wameyakosa kwa muda mrefu sana, wanapaswa kuendelea kuyabeba.

Msimu huu bado sitowadai chochote Yanga kimataifa, ila msimu ujao au miwili nawaona wanapaswa kupambania huko.
 
Inasemekana Paul Pogba, Cristiano Ronaldo na Raphael Varane walimfuata aliyekuwa Kocha wa Manchester United wakati huo Ralph Rangnick na kumwambia wazi kuwa Harry Maguire ni tatizo na hapaswi kucheza.

Rangnick nae aliwaambia kwakuwa wamemfuata ofisini ni vyema waseme mbele ya Harry Maguire kuwa yeye ni tatizo.

Wajerumani


[ Chanzo: Daily Mail ]
 
Msimu wa 2016/17 Man United walitoa kibunda cha maana kuipata saini ya Paul Pogba - Pound Milioni 115 na Ushee!

Kwangu mimi naona Pogba amecheza kawaida sana kipindi akiwa Man United ukilinganisha na Dau alilonunuliwa.

2019/20, Man United ikaona isiwe tabu, wakaingia tena sokoni wakachukua beki la dunia, Harry Maguire kwa gharama ya pound milioni 95, Lakini perfomance ya maguire wote tunaielewa, hapa naomba nisiseme sana.

2021/22, Man U wakapanda ndege mpaka Borrusia Dortmund, kama kawaida yao wakaweka mzigo mezani, na kumbeba Sancho mzima mzma kama alivyo kwa Pound milioni 93.50, perfomance yake mpaka sasa wote tunaielewa, Kama umeme wa Tanesco.

Soon, Man United watamtangaza Kinda Antony, huyu nae kwa taarifa zilizopo Man united wametoa karibia Pound milioni 104.5

Lakini, Ukiangalia vizuri hizi sajili za gharama za Man United mwisho wa siku haziwi na perfomance nzuri inayotegemewa na Mashabiki.

Ni kama vile Man United wanazitupa pesa zao bure, Inasikitisha sana.

Kumbuka hapo sijaongelea Usajili wa Angel Di Maria, Casemiro pamoja na Anthony Martial.
 
Atletico Madrid wanapaswa kuilipa Barcelona Euro Million 40 endapo Antoine Griezman atacheza kwa zaidi ya dakika 45 kwenye 50% ya mechi zake klabuni hapo.

Ikumbukwe Griezman yupo kwa mkopo Atletico, tayari pichani ndio takwimu zake mpaka sasa.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…