Makapuku Forum

Makapuku Forum

Imeandikwa na @swalehmawele

FT: Simba SC 2-0 ST. George.

Simba SC wamehitimisha sherehe zao za Simba day kwa ushindi, performance nzuri hasa katika kipindi cha pili, kipindi cha kwanza timu iliweka lock mbele na ikawa haitengenezi nafasi za kutosha, ilikuwa rahisi kwa St George kuzuia kwa sababu mikimbio mingi ilifanywa katika zone ya pili.

Okrah, Kibu na Sakho wote ni wachezaji ambao aina yao ya uchezaji inafanana, wanapenda kukimbia na mpira muda wote hasa kutokea pembeni ( inverted ), athari yake Simba ikakosa mtu ambae anaweza ku control timu katikati ( zonal 14 ) kitu ambacho kingefungua mianya kwenye kushambulia.

St. George imewapa picha Simba SC ni namna gani wanaweza kuzipa njia wanapofanyiwa transition, wameonyesha uthubutu wa kucheza na kutengeneza nafasi za kufunga, bahati njema zipo nyakati ambazo walikutana na Benno Kakokanya aliekuwepo kazini, mwamba anaulizia nafasi yake kwa benchi la ufundi.

Mohammed Ouattara, ameonyesha kitu katika dakika tisini alizozicheza, mgumu, mzuri akiwa na mpira na uwezo wa kucheza mipira ya juu na kuanzisha mashambulizi kutokea chini, muda wote anafikiria ni vipi timu itasogea juu.
Yule Gattouch Panom wa Ethiopia mtu wa kazi sana, mtulivu na mzuri katika kuzuia, kiungo mgumu.

Vitu vya Chama hufanywa na Chama mwenyewe, what a player, sehemu ambayo unahisi atapiga yeye atafinya, si rahisi kufanya alichokifanya leo.

Kama Zoran atakuwa anatumia 4-2-3-1 nadhani Jonas Mkude ni mchezaji muhimu, naiona partnership yake na Vicent Akpan.
Screenshot_20220808-203354_OGInsta%2B.jpg
 
George Ambangile

ITS GOOD FOOTBALL

Simba SC na St George wameitendea haki hii siku ya leo , kwa kuonesha kandanda safi kwa dakika zote 90+ . Inawezekana ikawa mechi ya preseason ya mwisho kwa Simba SC kabla ya mitanange ya kimashindano kuanza

Kocha Maki alibadili mifumo kama mara tatu , alianza na 4-4-2 dakika kadhaa zikapita akabadilisha kwenda 4-2-3-1 ( Okrah nyuma ya Habib , Sakho na Kibu katika wing zote mbili, Mkude na Kanoute kwenye kiungo wa kati ) na mwisho baada ya kuingia Kapombe akabadilisha kwenda 3-4-2-1 ( Back 3 ya Kapombe Outtara na Inonga ) huku Akpan na Okwa katikati , Wingbacks Banda na Mzamiru na Chama Jr & Phiri nyuma ya Dejan . ( Tactically Flexible )

St George wenyewe wamecheza takribani dakika zote kwa kutumia 4-2-3-1 ambayo kuna wakati kwa kiasi fulani ilikuwa inabadilika kuwa 4-3-3 hasa wakiwa na mpira

Simba SC kuna wachezaji wengi wenye kasi, kitu kimoja nilichoona ambacho naamini hata kocha kaona ni wakipoteza mpira wanachelewa kufika kwenye tukio na pia wakiwa mpira kwenye kiungo wanaharakisha pasi na mipira kupotea . Nafikiri kama kutakuwa na ufanisi mzuri sana wa pasi katika wakati sahihi ile kasi ya ushambuliaji itafaidika ( Chama Jr anarahisisha soka )

St George wana wachezaji wengi sana ambao kiufundi wapo vizuri , wanacheza pasi fupi fupi kwa kutengeneza pembe tatu na wanahama kwa pamoja nafikiri kuna muda wanazidisha bila sababu ( over play )

NOTE

1: Nafikiri Okrah anacheza vizuri kwenye namba 10 na bado una Chama Jr ... hiyo ni kazi ya kocha Maki , ni faida kuwa na wachezaji wazuri kila eneo

2: Outtara , nafikiri baada ya kuondoka kwa Wawa Simba walihitaji Ball Playing CB .

3: Inonga anatakiwa kucheza " simple football " kuna muda anajitengenezea matatizo . Beno good game

4: Yule Abel miguu yake hatari

5: Kiungo cha St George , Nahodha wao na Panom Gattouch wanaubonda vizuri

6: Chama Jr hana adabu

7: Kwani dirisha la usajili limefungwa ? Kuna wachezaji pale St George
Screenshot_20220808-205143_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom