[emoji3578] Farhan Jr
Sijui lakini wengine ila binafsi nikiwa kama Shabiki wa Simba achilia mbali Uchambuzi naona hili dirisha hata wangesajiliwa wachezaji watatu au wanne ingekuwa sawa tu
Anahitajika beki wa maana ambaye washampata na atasaidia timu, alihitajika Kiungo Mkabaji mzuri tayari wamempata, alihitajika Kiungo Mshambuliaji ni tayari wamempata tena ni kama replacement ya Bwalya aliyeuzwa
Anahitajika Straika mwingine wa maana ikibidi, ambaye naona wanahangaika sokoni kisha hapo unafunga usajili wako na unaendelea kuandaa timu yako kwa ajili ya msimu mpya
Wamefanya inclusion nzuri sana ya Locals ambao ni Kapama na Habibu Kyombo, kuna muda unahitaji damu kama hizi kwenye timu, kuna muda tu Peter na Sakho huko mikoani itakuwa ngumu wao watacheza vyema
Nikiitazama hii timu sioni ubaya wake upo wapi, sielewi watu presha wanatoa wapi! Sokoni utapata wapi kiungo kariba ya Chama? Kipa kama Aishi? Beki kama Zimbwe na Shomari? Tena kwa bei nafuu, Majibu ni HAPANA
Sijui lakini wengine wanaonaje ila mimi kama Shabiki tu sioni shida na sioni sababu Viongozi wafanye panic buys, hii timu ni nzuri tu
Tumetofautiana lakini kwenye kutazama kitu na kukichakata, kukosa ubingwa haipaswi kutafsiri timu ni mbovu, ni mtazamo mbaya sana