Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mohamed Mchengerwa ameteua Kamati maalum itakayokuwa na jukumu la kuratibu mdundo wenye asili ya kitanzania ambapo ndani yake kuna Ma-DJ wawili, Producers watatu na Msanii mmoja.
Mwenyekiti wa Kamati hii ambayo imetakiwa kufanya kazi toka jana July 20 2022 ni Dr. Kedmon Mapana ambaye ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambapo Katibu wa Kamati akiteuliwa kuwa Dr. Herbert Makoye, Mkuu wa Chuo cha Sanaa Bagamoyo huku Wajumbe wakiwa ni kama ifuatavyo.
DJ JD (John Dilunga Matlou),
DJ Fetty (Fatuma Hassan),
Producer P Funk Majani (Paul Mattysse), Producer Master J (Joachim Kimario), Producer Humphrey Domboka (Wanene), Msanii Mwana FA.
Wengine walioteuliwa ni Chifu wa Mwanza Aron Mikomangwa akiwa ni mzoefu wa midundo ya asili, Mkuu wa Kikundi cha Ngoma cha Taifa Zanzibar Abdallah Othman Abdallah na mwisho ni Mtangazaji Mkongwe Masoud Masoud kutoka TBC.