Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220515-043455_OGInsta%2B.jpg
 
Maboresho mapya kutoka WhatsApp;

- Uwezo wa makundi umeboreshwa, ambapo kundi litaweza kua na idadi ya watu mpaka 512 kutoka 256 ambayo ndio ulikua uwezo wa mwisho hapo awali.

- Uwezo wa 'emoji reactions' kwenye meseji, hautakua na ulazima tena wa ku reply' meseji na emoji' kama ilivyokua awali. Uwezo wa emoji reactions' unamuwezesha mtu moja kwa moja kujibu ujumbe kwa emoji bila kufanya kama ana reply ili kujibu.

- Uwezo wa kutuma faili mpaka 02GB, hapo awali mwisho ilikua ni 100MB lakini kuanzia hivi karibuni utaweza kumtumia mtu mpaka ukubwa huo na faili zote zitakua na end to end encryption (yaani haziwezi kusomwa kwa njia ambazo si halali na watu wengine).

Una maoni gani kuhusu mabadiliko haya mapya?
Screenshot_20220515-050316_OGInsta%2B.jpg
 
Maboresho mapya kutoka WhatsApp;

- Uwezo wa makundi umeboreshwa, ambapo kundi litaweza kua na idadi ya watu mpaka 512 kutoka 256 ambayo ndio ulikua uwezo wa mwisho hapo awali.

- Uwezo wa 'emoji reactions' kwenye meseji, hautakua na ulazima tena wa ku reply' meseji na emoji' kama ilivyokua awali. Uwezo wa emoji reactions' unamuwezesha mtu moja kwa moja kujibu ujumbe kwa emoji bila kufanya kama ana reply ili kujibu.

- Uwezo wa kutuma faili mpaka 02GB, hapo awali mwisho ilikua ni 100MB lakini kuanzia hivi karibuni utaweza kumtumia mtu mpaka ukubwa huo na faili zote zitakua na end to end encryption (yaani haziwezi kusomwa kwa njia ambazo si halali na watu wengine).

Una maoni gani kuhusu mabadiliko haya mapya?View attachment 2224869
Nimekumiss
 
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imesema Wabunge 19 waliovuliwa uanachama na CHADEMA, waendelee kufanya shughuli zao za kibunge hadi Mahakama itakaposikiliza maombi yao ya zuio la muda kuhusu ubunge wao.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji John Mgeta baada ya kusikiliza kesi hiyo kwa ajili ya kutoa uamuzi kama Wabunge hao waendelee kuwa Bungeni ama laah, ambapo June 13, 2022 ndio atasikiliza zuio hilo.
Screenshot_20220516-174903_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI Innocent Bashungwa @innocentbash akiwa Dodoma leo amemuagiza Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia TAMISEMI Ramadhan Kailima kuwafuatilia Watumishi 12 Mkoani Tanga waliogushi barua za uhamisho na haraka warudishwe kwenye vituo vyao vya kazi vya awali.

Bashungwa pia ameagiza Watumishi hao 12 wachukuliwe hatua stahiki za kinidhamu kwa kosa la kugushi nyaraka za Serikali.

"Naagiza wote wote waliofanya hivyo watambuliwe kisha Katibu Tawala wa Mkoa awape barua za kuwataka kwa kipindi cha siku tano wawe wamerejea vituo vyao halali kwa gharama zao na iwapo walilipwa pesa za kujikumu (per diem allowance) na usumbufu (disturbance allowance) zilizotokana na uhamisho huo wa kugushi, waelekezwe kuzirejesha ndani ya kipindi cha miezi miwili ya Mei na Juni, 2022"

"Mamlaka za nidhamu kwenye Halmashauri zao zielekwezwe kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa kosa la kugushi, kuitia hasara Serikali kwa kujipatia fedha (posho ya kujikimu na usumbufu) isivyo halali, kuufanya utumishi wa umma kudharaulika, kwenda kinyume cha maadili ya utumishi wa umma n.k na pia Mamlaka za Usalama, Polisi na PCCB ziwahoji ili wamtaje aliyegushi saini ili kupata mtandao mzima"
Screenshot_20220516-175100_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa hotuba Bungeni leo kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya fedha ya Wizara ya Afya 2022/2023 ambapo amesema "Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe katika kipindi cha Julai 2021 hadi Machi 2022 ilihudumia jumla ya Wagonjwa 28,325 kati yao 26,761 ni Wagonjwa wa akili wa nje (OPD) na Wagonjwa wa akili wa ndani (IPD) 1,564"

"Aidha, Wagoniwa wa msamaha waliopewa huduma walikuwa 3,985 ambao waliigharimu Hospitali kiasi cha Tsh. 60,217,746 katika kipindi hicho, jumla ya Wagonjwa 123, walipata huduma za kibingwa za Saikolojia na Wagonjwa 443 wa Neuro-psychiatry na Wagonjwa wapatao 123 walifanyiwa uchunguzi na kuandikiwa taarifa za Kisheria"

"Vilevile, katika kliniki ya afya ya akili kwa Watoto na vijana Wagonjwa 1,121 walihudumiwa, Taasisi pia, ilipokea Wagonjwa wapya 225 wenye matatizo ya utumiaji wa madawa ya kulevya na hivyo kufanya jumla ya waraibu wanaohudumiwa na kituo cha Itega kufikia 548 toka kilipoanza kutoa huduma mwaka 2020"
Screenshot_20220516-181851_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom