Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Kiwanda cha kwanza barani Afrika cha kuzalisha na kusambaza chanjo za Corona kilichozinduliwa 2021, kiko hatarini kufungwa baada ya kutopokea hata oda moja ya chanjo, amesema Afisa Mkuu wa kampuni hiyo.
Kampuni ya Aspen Pharmacare (APNJ.J) ya Afrika Kusini ilijadili mkataba wa kutoa leseni Novemba 2021 ili kuuza chanjo ya Johnson & Johnson (JNJ.N) ya COVID-19 na kuisambaza kote Afrika.
Huku ikiwa ni 1 ya sita tu ya Watu wazima barani Afrika waliopokea dozi kamili ya chanjo ya Corona kulingana na takwimu za hivi punde za WHO, makubaliano ya Aspen ya kuuza chanjo ya Aspen ya COVID-19, Aspenovax, barani Afrika yalionekana kuwa na ‘soko’ la uhakika lakini sasa imekua ndivyo sivyo.
"Hatujapokea oda ya chanjo za Aspenovax, kwa sababu hatujapata oda yoyote ya chanjo basi ni wazi kutakuwa na sababu ndogo sana za kubakiza njia ambazo tunatumia kwa uzalishaji” Mkurugenzi Mkuu wa Aspen Stavros Nicolaou ameliambia shirika la habari la Reuters kwa njia ya simu.
Lengo la Umoja wa Afrika ni kuzalisha asilimia 60 ya chanjo zote zinazotolewa barani Afŕika ifikapo mwaka 2040 kutoka asilimia 1 ya sasa, na mitambo kadhaa ya aina hiyo inaanzishwa.
Kampuni ya Aspen Pharmacare (APNJ.J) ya Afrika Kusini ilijadili mkataba wa kutoa leseni Novemba 2021 ili kuuza chanjo ya Johnson & Johnson (JNJ.N) ya COVID-19 na kuisambaza kote Afrika.
Huku ikiwa ni 1 ya sita tu ya Watu wazima barani Afrika waliopokea dozi kamili ya chanjo ya Corona kulingana na takwimu za hivi punde za WHO, makubaliano ya Aspen ya kuuza chanjo ya Aspen ya COVID-19, Aspenovax, barani Afrika yalionekana kuwa na ‘soko’ la uhakika lakini sasa imekua ndivyo sivyo.
"Hatujapokea oda ya chanjo za Aspenovax, kwa sababu hatujapata oda yoyote ya chanjo basi ni wazi kutakuwa na sababu ndogo sana za kubakiza njia ambazo tunatumia kwa uzalishaji” Mkurugenzi Mkuu wa Aspen Stavros Nicolaou ameliambia shirika la habari la Reuters kwa njia ya simu.
Lengo la Umoja wa Afrika ni kuzalisha asilimia 60 ya chanjo zote zinazotolewa barani Afŕika ifikapo mwaka 2040 kutoka asilimia 1 ya sasa, na mitambo kadhaa ya aina hiyo inaanzishwa.
na kisha kuelekea mkoani Lindi kwa gari ambapo kesho Mei 3 watakuwa wageni wa Namungo FC katika uwanja wa Ilulu, Lindi mechi ya Ligi Kuu.
️ Fernandes

Ahmed ally