Makapuku Forum

Makapuku Forum

BOSI wa Maendeleo Soka la Vijana Yanga, Mwinyi Zahera amerudishwa tena kuwa kocha wa timu ya Taifa lao la DR Congo akichukua nafasi ya Mkongomani mwingine aliyetemwa katika mabadiliko.

Taarifa iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Congo ni imesema Zahera anarudi katika kikosi hicho kuwa kocha msaidizi akimsaidia Muargentina Hector Cuper.

Zahera anachukua nafasi ya kocha Daouda Lupembe ambaye ameondolewa katika kikosi hicho baada ya kupata kazi katika timu ya Sanga Balende inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo.
Screenshot_20220427-035425_OGInsta%2B.jpg
 
Beki wa Chelsea, Antonio Rudiger ameshaafikiana makubaliano binafsi na miamba ya Hispania Real Madrid na kumpa ofa ya mkataba wa miaka minne hadi 2026.
Hili linakuja baada ya kocha wa timu hiyo, Thomas Tuchel na kuthibitisha beki huyo ataondoka mwisho wa msimu huu.
Screenshot_20220427-035607_OGInsta%2B.jpg
 
Kocha Mkuu wa RS Berkane, Florent Ibenge amepata ajali ya gari wakati akitoka mazoezini jana.

Taarifa ya klabu yake imesema ajali hiyo imempa maumivu makali ya mgongo kocha huyo Mkongomani.

Vipimo vilivyofanywa kwenye Hospitali ya Chuo Kikuu cha Mohammed VI vimeonyesha kocha huyo ameumia katika eneo hilo na atalazimika kupumzishwa kwa muda wa wiki moja mpaka siku 10.
Screenshot_20220427-035708_OGInsta%2B.jpg
 
CAF YATOA ORODHA YA LIGI 12 BORA
.
1. Moroco
2. Egypt
3. Algeria (1)
4. Tunisia (1)
5. South Africa
6. DR Congo
7. ANG (3)
8. Sudan (3)
9. Libya (6)
10. Guinea(3)
11. TANZANIA (1)
12. Nigeria (4)
.
Tanzania imepanda kwa nafasi moja….Ikumbukwe Ligi hizi 12 zinapata nafasi ya kutoa vilabu vinne katika mashindano ya CAF
Screenshot_20220427-035905_OGInsta%2B.jpg
 
NABI: TUTAMKOSA MCHEZAJI MMOJA TU
.
“Tuna timu kamili nafikiri hii itakuwa sapraizi ya kwanza sijajua tumtumie mchezaji gani kuelekea mechi hii. Kila mtu yuko tayari na wachezaji wanataka kucheza hii mechi,” amesema Nabi ambaye juzi alipewa gari mpya aina ya Toyota Vanguard na uongozi wa GSM.
.
“Tutamkosa Yacouba (Songne) pekee, lakini tuna nafasi kubwa ya kuchagua watu bora ambao tutawaona wako tayari kutupa ushindi. Hii ni mechi ambayo tunatakiwa kushinda kwa namna yoyote.”
Screenshot_20220427-040056_OGInsta%2B.jpg
 
DE JONG ATIBUA BARCA, AIWAZIA MAN
.
Kiungo fundi wa mpira, Frenkie de Jong bayana kabisa ameonyesha hasira za wazi baada ya chama lake la Barcelona kumtoa katika mechi ya kipigo dhidi ya Rayo Vallecano juzi Jumapili na sasa amezidi kuibua uvumi wa mpango wake wa kwenda Manchester United.
.
Kocha mteule huko Man United, Erik ten Hag anaripotiwa kuwa na mpango wa kumvuta De Jong wakafanye kazi pamoja Old Trafford baada ya kupata mafanikio makubwa ndani ya miaka miwili waliyokuwa Ajax
.
Kiungo huyo wa Kidachi alicheza soka la kiwango bora kabisa kipindi yupo Ajax ya kocha Ten Hag. Huduma yake bora iliwafanya Barcelona kutoa pesa kunasa saini yake mwaka 2019.
Screenshot_20220427-040207_OGInsta%2B.jpg
 
KICHUYA: SIJUTII KUREJEA NYUMBANI
.
Winga wa Namungo, Shiza Kichuya ameeleza kutojutia uamuzi wa kurejea nyumbani kucheza soka baada ya kuachana na Pharco FC ya Misri.
.
“Kama kwenda tena nje naweza kwenda ila siwezi kujutia kurudi kwangu nyumbani maana mimi ndiye ninayejua kilichotokea.”
Screenshot_20220427-040434_OGInsta%2B.jpg
 
| Nasreddine Nabi:
.
“Tunaingia katika maandalizi ya mechi ya Simba tukiwa na kundi kamili la wachezaji, tulimpumzisha Job (Dickson) kutokana na alikuwa na kadi mbili za njano kama angepata kadi ingetupa shida, lakini Feisal (Salum) na Aucho (Khalid) nimefurahi jinsi walivyorejea na kucheza kwa utimamu mzuri.
.
“Mtu aliyebaki ni Saido (Said Ntibazonkiza) ambaye naamini tunapoingia kambini leo atakuwa tayari kwa mchezo huo, huyu ni mchezaji mkubwa ambaye ni muhimu kuwa naye katika mechi kubwa kama hii inayokuja,”
Screenshot_20220427-040619_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kuna muda Pablo anaongea maneno machungu sana pengine Viongozi au Mashabiki kama huyatafakari vyema unaweza kumchukia lakini wenzetu wapo hivyo, wanaishi kwenye neno UKWELI

Juzi juzi Rangnick alikuwa anawachana Bodi na wamiliki kuwa timu ipo chini haipo kwenye level za Liverpool, Chelsea wala Man City, kwake anaiona United ni timu ya kawaida tu sana

Ndivyo Pablo jana anakiri kuwa Pirates wapo mbali sana, sio kwa uwekezaji tu bali hata wachezaji, yeye kama Kocha kuna kitu atakuwa amekiona ambacho akisema Mwandishi inakuwa ngumu kueleweka

Ukinichukua Farhan kama Shabiki wa Simba naweza kuona kama Kocha anatuvua nguo, ila ukinichukua Farhan kama Mwandishi naona Mwalimu yupo sahihi tu sana, amezungumzia project kwa lugha ya kificho

Simba imepambana sana, nguvu inayotumika kufika robo ni kubwa sana, wachezaji wanajituma sana! Kiasi ambacho hakuna anaewadai

Ukweli ulio wazi sasa ni MO DEWJI kuilinda project, kama watauza wachezaji muhimu kila msimu itakuwa ngumu kuanza upya kila siku, kama tutaenda sokoni kupata wachezaji wengi kama INONGA that means kweli tutasogea Afrika

Hili tena sio suala la Kocha, Mashabiki wala wachezaji, reality check ni MO DEWJI sasa kuendelea kuweka pesa kweli kupata quality kubwa zaidi!

Nafurahi sana kumsikiliza Pablo kwenye interview zake, jana hakutumia muda kupiga kelele za VAR, yeye kazungumzia Mchezo kisha kagusa quality! MO DEWJI kazi kwako Kiongozi

Project ilindwe sana ipo siku Simba anaenda kufanya makubwa zaidi Afrika
Screenshot_20220427-040824_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom