Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuendelea kusimamia kwa ukaribu na kuhakikisha shughuli za ujenzi katika kijiji cha Msomera kilichopo Handeni Makoani Tanga zinakamilika haraka.

Amesema kuwa Wizara hiyo inapaswa kuhakikisha inaendelea kutoa elimu kwa wakazi wa Ngorongoro waliojiandikisha kuhama kwa hiari "Zoezi hili linaloendea la kuimarisha miondombinu ikiwemo upimaji wa viwanja litawanufaisha wakazi wa Msomera pamoja na hao wanaohamia eneo hili"

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana Jumapili, Aprili 24, 2022 alipokagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika kijiji cha Msomera kilichopo Handeni Mkoani Tanga kwa ajili ya wakazi wa Ngorongoro waliokubali kuhamia kwenye Kijiji hicho ili kupisha shughuli za uhifadhi kwa maendeleo ya Taifa.

Aidha, Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuendelea kuandaa mazingira mazuri ya ufugaji "Wizara hii inapaswa pia kuhakikisha kwamba kunakuwa na miundombinu wezeshi ya wafugaji yakiwemo malambo ya kunyweshea mifugo, majosho, ujenzi wa kliniki ya kutibu magonjwa ya mifugo katika eneo hilo.”

Akitoa maelekezo kwa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Majaliwa ameitaka iendelee kuwekeza nguvu katika kuimarisha miundombinu ya elimu "Kama tunavyoona hapa shule ya msingi inajengwa, sekondari inajengwa, zahanati zinakarabatiwa lakini pia ujenzi wa kituo cha afya na barabara unaendelea, ongezeni nguvu"

Majaliwa pia ameitaka Wizara ya Maji iendelee kuhakikisha kiwango cha maji katika eneo hilo kinakuwa toshelevu kwa kuchimba zaidi ili hata majosho na malambo yapate maji ya kutosha. Maji ambayo tayari yameshachimbwa na kuyapata ni mengi kuliko mahitaji lakini tuongeze kiwango"
Screenshot_20220426-035715_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa amewaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa kuhakikisha vifaa vilivyotolewa leo kwa ajili ya Walimu vinafika katika vituo kwa kuzingatia mgao uliotolewa na TAMISEMI, ametoa agizo hilo leo wakati wa kuzindua usambazaji wa vifaa vya TEHAMA kwa ajili ya Vituo vya Walimu 150 vilivyopo katika Halmashauri 144 za Mikoa 26 ya Tanzania Bara uliofanyika Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa, Dar-es-salaam.

Waziri Bashungwa amewaagiza Ma -RAS kuhakikisha wanawasilisha taarifa ya mapokezi na usambazaji wa vifaa hivyo kimkoa kwa Katibu Mkuu TAMISEMI kabla au ifikapo tarehe 15 Mei, 2022 ambapo amesema Serikali imeamua kuvifufua vituo hivyo ili kusaidia Walimu kubadilishana uzoefu na Wataalamu wabobezi kupeana mbinu za ufundishaji wakiwa na Walimu, ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu ya msingi na sekondari nchini.

"Leo nimekabidhi mashine za photocopy 150, projekta 150, printer 150 na kompyuta 600 kwa ajili ya kwenda kwenye Vituo vya Walimu vilivyopo kwenye Halmashauri 144, vifaa vina thamani ya Tsh. Bilioni 2.5, nimeelekeza Halmashauri 39 zilizobaki kupatiwa vifaa hivi kwenye mwaka wa Fedha wa 2022/23"

"Dhamira ya Rais wetu, Samia Suluhu ni kuona Walimu wanajengewa uwezo kila Halmashauri karibu na maeneo yao ya kazi na tunawawezesha kutumia TEHAMA katika ujifunzaji na ufundishaji, bajeti ya TAMISEMI ya 2022/23 iliyopitishwa na Bunge tayari zimetengwa Bilioni 55.57 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 809 zenye uwezo wa kuchukua kaya 1,912"
Screenshot_20220426-040020_OGInsta%2B.jpg
 
Kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 13 yuko mbioni kupata degree yake ya shahada ya kwanza mwaka huu, kutokea Chuo Kikuu cha Minnesota, nchini Marekani.

Kijana huyo aitwaye Elliott Tanner, atapata degree yake baada ya kujikita kwenye masomo ya fizikia na hesabu na kwa sasa ana wastani wa GPA ya 3.78.

Tayari amekubaliwa katika programu ya PhD ya Fizikia ya Chuo Kikuu cha Minnesota na ana mpango wa kuwa mwanafizikia wa nadharia ya juu na kuwa profesa shuleni "Nina shauku ya ajabu ya fizikia,imekuwa moja ya mambo ninayopenda kufanya."

Tanner alianza kusoma na kufanya mazoezi ya somo la hesabu akiwa na umri wa miaka 3, kulingana maelezo ya mama yake Michelle Tanner, alimaliza masomo ya secondary na na shule ya upili katika mda wa miaka 2 tu na kuanza chuo kikuu akiwa na umri wa miaka 9 baada ya kusomea nyumbani kwao.

Hata kwa mafanikio yake ya ajabu, kijana huyu hatokuwa Mhitimu mdogo zaidi wa Chuo Kikuu kikuu, Cheo hicho kinashikiliwa na Michael Kearney, ambaye alipata stadhahada yake ya kwanza katika somo la anthropolojia kutoka Chuo Kikuu cha Alabama Kusini nchini Marekani mwaka 1994, alikuwa na umri wa miaka 10 tu.
Screenshot_20220426-040202_OGInsta%2B.jpg
 
Katika kuadhimisha siku ya Malaria Duniani, Naibu Waziri wa Afya Wziara ya Afya Dkt. Godwin Mollel ameungana na mwenyeji wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Pascal Patrobas Katambi (Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini) kugawa vyandarua kwa wanawake zaidi ya 400 pamoja na kufikia makundi mbalimbali ya wananchi katika jamii ndani ya Manispaa ya Shinyanga.

Dkt. Mollel ameipongeza Taasisi ya Doris Mollel @dorismollelfoundation kwa kushirikiana na Amref kuja na mkakati huo wa kuwafikia wananchi moja kwa moja na kuweza kutoa misaada mbalimbali inayogusa maisha ya Watanzania.

Katika Warsha iliyohudhuriwa na Wanawake wajawazito na wanaonyonyesha zaidi ya 400, Dkt. Mollel amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imelenga kuboresha huduma za uzazi, Mama na Mtoto na kuhakikisha jamii inapata elimu ya kutosha na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Mollel Doris Mollel amesema kuwa lengo la warsha hiyo ni kutoa elimu ya ugonjwa malaria na namna ya kujikinga pamoja na kuhamasisha Wanawake kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO-19 ili waweze kujikinga janga la Corona.

"Zoezi limefanyika katika mikoa mitatu kwa kushirikiana na Amref kwa mikoa ya Simiyu, Kagera na Shinyanga na tunaishukuru Serikali kwa kutuwekea mazingira wezeshi sisi taasisi binafsi kuweza kufanya kazi na kutoa mchango wetu ndani ya jamii"
Screenshot_20220426-040330_OGInsta%2B.jpg
 
Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imetoa ufafanuzi kuhusiana na habari iliyosambaa mitandaoni kuhusu hali ya matairi ya ndege zake ambayo inadaiwa kuwa hali yake inahatarisha usalama wa ndege na abiria.

"ATCL inamshukuru abiria huyu kwa kuonesha umakini kwa usalama wa abiria na ndege, ATCL hufanya ukaguzi wa lazima wa ndege zake zote katika maeneo yote ya ndege yakiwemo matairi baada ya safari zote za siku, kabla ya kuanza safari za siku na baada ya kila safari"

"Kwa mujibu wa rekodi zilizowekwa na ATCL, tairi ya ndege tajwa lilikuwa na mruko mmoja tangu tangu kubainika kulika kwa tabaka la kwanza hivyo kulikuwa na miruko saba zaidi hadi kufikia saba zaidi hadi kufikia ukomo wa matumizi yake kwa mujibu wa miongozo"

"Kwa misingi hiyo tairi hilo lilikuwa bado ni salama kutumia kwa mujibu wa miongozo iliyowekwa na Waundaji na kufuatwa ATCL
Screenshot_20220426-040418_OGInsta%2B.jpg
 
Kane Tanaka ambaye anaripotiwa kuwa Mtu mzee zaidi duniani amefariki nchini Japan akiwa na umri wa miaka 119, kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya, Kazi na Ustawi wa nchi hiyo.

Tanaka alizaliwa Januari 02, 1903 na kufariki Aprili 19 mwaka huu taarifa kutoka Wizara ya Afya nchini Japan imesema huku rekodi za dunia za Guinness zikisema zimesikitishwa na kifo cha Bibi huyo Tanaka na wakasema habari za kifo chake zimethibitishwa na Mshauri Mkuu wa gerontology Robert Young, ambaye pia alisaidia kuthibitisha rekodi yake kama Mtu Mzee zaidi aliye hai mnamo mwaka 2019.

Guinness World Records imesema "Alikuwa Mzee zaidi aliyeishi pia ni Mtu wa pili mwenye umri mkubwa zaidi kuwahi kurekodiwa, nyuma ya Jeanne Calment pekee aliyeishi hadi umri wa miaka 122"
Screenshot_20220426-040519_OGInsta%2B.jpg
 
Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa @gersonmsigwa kupitia taarifa yake aliyoitoa New York Marekani amesema filamu ya Royal Tour kwa Marekani pekee itarushwa na vituo vya televisheni 350 lakini itawekwa pia kwenye majukwaa mengine ya Applications za Amazon Prime na Apple TV Plus.

"Waandaaji wa filamu hii Peter Greenberg na Timu yake ya Royal Tour, hawa jamaa wana mtandao mkubwa wa kufikisha ujumbe duniani, hapa Marekani pekee filamu hii itarushwa na vituo vya TV 350 lakini wanakwenda kuiweka kwenye Applications za Amazon Prime na Apple TV Plus, huko Amazon Prime na Apple TV Plus filamu itauzwa lakini lengo letu Tanzania sio kufanya biashara ya kuuza filamu, lengo letu ni kuitangaza nchi na kuifungua nchi ili tupate Watalii na Wawekezaji kwa ajili ya kukuza uchumi wetu"

"Uzindzui ya Royal Tour umefanyika kwa mafanikio makubwa hapa New York katika jumba la makumbusho la Solomon Guggenheim na kule Los Angeles katika eneo maarufu la burudani duniani na ambalo lina umaarufu mkubwa katika uzalishaji na usambazaji wa maudhui ya sanaa la Hollywood, baada ya uzinduzi uliofanyika hapa Marekani sasa uzinduzi unakwenda kufanyika nchini Tanzania"

"Tarehe 28 Aprili, 2022 tutazindua filamu hii Jijini Arusha, tarehe 07 Mei, 2022 tutazindua Zanzibar na tarehe 08 Mei, 2022 tutazindua Jijini Dar es Salaam, baada ya hapo filamu hii itatolewa kwa vituo vyote vya TV kwa Tanzania ikiwa imetafsiriwa maudhui yake kwa Kiswahili na vitakuwa huru kuirusha ili Watanzania wote waione kupitia kwenye TV zao"
Screenshot_20220426-040635_OGInsta%2B.jpg
 
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Meya wa Jiji la Dallas nchini Marekani, Eric Johnson, anajipanga kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Dallas mpaka Tanzania, hiii ni baada ya kufanya mazungumzo na Mawaziri wa Tanzania waliomuwakilisha Rais Samia ambapo wamekubaliana kuanzisha uhusiano wa kibiashara wa utalii na mawasiliano na Tanzania.

Kwenye taarifa yake ambayo ameitoa kutoka New York Marekani Msigwa amesema "Moja ya jambo ambalo tunaenda kufanya ili kuongeza Watalii ni kuongeza ndege za moja kwa moja kutoka kwenye maeneo ambayo yana Watalii wengi, Marekani hapa ni moja ya maeneo ambayo yanachangia Watalii wengi duniani "

"Rais Samia amewakilishwa na Mawaziri Jijini Dallas ambapo wamekutana na Meya wa Jiji hilo, Eric Johnson ambapo wamekubaliana kuanzisha uhusiano wa kibiashara wa utalii na mawasiliano na Tanzania "

"Meya huyo wa Jiji hilo anajipanga kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Dallas mpaka Tanzania"
Screenshot_20220426-040755_OGInsta%2B.jpg
 
Kundi la Taliban limepiga marufuku utumiaji wa application ya TikTok na mchezo wa mtandaoni wa PUBG, wakisisitiza kuwa inawapoteza vijana wa Afghanistan, Kundi hilo la Taliban kutokea nchini Afghanistan limesema pia litapiga marufuku vituo vya televisheni kurusha hewani kile walichokiona kuwa vitu visivyo vya maadili.

Hii inakuja baada ya kupigwa marufuku kwa muziki, sinema na michezo ya kuigiza ya televisheni, Kundi la Taliban liliahidi mbinu nyepesi za kuongoza Serikali pindi likishika madaraka lakini limezidi kukandamiza uhuru hasa kwa Wanawake nchini humo.

Msemaji wa Taliban Inamullah Samangani amesema marufuku hiyo ya kutumia Tiktok ni muhimu ili kuzuia upotoshaji wa kizazi kipya, mpaka sasa haijulikani ni lini marufuku hiyo itaanza kutumika na kwa muda gani.

Hii ni mara ya kwanza kwa kikundi hicho kupiga marufuku application ya simu tangia waingie madarakani, TikTok na game ya PUBG zimekuwa zikitumika zaidi na vijana wa Afghanistan katika miezi ya hivi karibuni kwa sababu aina nyingi za burudani zimepigwa marufuku nchini humo.
Screenshot_20220426-040907_OGInsta%2B.jpg
 
Watu wanane wamefariki dunia na wengine 19 wamejeruhiwa katika ajali ya gari (Coaster T 287 CCY) mali ya Kanisa Katoliki Njombe iliyogongana na lori la makaa ya mawe, RPC Njombe, Hamis Issah amethibitisha.

Watu hao ni miongoni mwa Vijana wanaounda Umoja wa Vijana Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe (UVIKANJO) ambao walikwenda kuwatembelea Watoto yatima katika kituo cha Ibumila Wilayani Njombe.

Ajali hiyo imetokea jana jioni katika eneo la Igima Wilayani Wanging'ombe Barabara kuu inayoelekea Mkoa wa Ruvuma.

RPC Issah amesema majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Mji wa Njombe Kibena pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.
Screenshot_20220426-041018_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Rwanda Paul Kagame amesafiri hadi nchi jirani ya Uganda kushiriki sherehe ya kuzaliwa ya Mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba ambayo imefanyika usiku wa kuamkia leo.

Safari hii nchini Uganda ambayo ni ya kwanza kwa Kagame katika kipindi cha miaka minn inaonekana kama ishara ya kupunguza hali ya wasiwasi kati ya nchi hizo mbili ambazo mara kadhaa zimetajwa kuwa na mzozo wa chini kwa chini.

Shirika la Utangazaji la Taifa la Rwanda limesema Kagame pia atafanya mazungumzo na Mtoto wa huyo wa Museveni, Luteni Jenerali Kainerugaba, ambaye anasimamia vikosi vya jeshi la nchi kavu vya Uganda ambaye ameonekana kuwa na mchango mkubwa katika kurahisisha uhusiano kati ya Rwanda na Uganda.

Kuingilia kati kwa Mtoto huyo wa Museveni kwenye mgogoro wa nchi hizo, kuliaminika kuwa sababu kuu ya kufunguliwa tena kwa mpaka wa pamoja wa nchi hizo mapema mwaka huu, mipaka hiyo ilikuwa imefungwa tangu mwaka 2019, nchi zote mbili zilikuwa zinashutumiana kuingilia mambo ya kila mmoja.

Muhoozi alizaliwa April 24,1974 na jana ametimiza umri wa miaka 48, Muhoozi anatajwa kuwa ndiye anaandaliwa kuwa mrithi wa kiti cha Urais ambacho kinashikiliwa na Baba yake (Museveni) kwa sasa.
Screenshot_20220426-041124_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Emmanuel Macron (44) anaanza sasa juhudi za kuliunganisha Taifa lililogawika pakubwa la Ufaransa baada ya kuchaguliwa tena kuongoza kwa muhula wa pili katika duru ya pili ya uchaguzi dhidi ya mpinzani wake Marine Le Pen.

Macron, wa siasa za mrengo wa wastani ameshinda kwa asilimia 58.6 ya kura dhidi ya Le Pen aliyepata asilimia 41.45, kwa mujibu wa matokeo rasmi yaliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Macron ndiye Rais wa kwanza wa Ufaransa katika miongo miwili kushinda muhula wa pili lakini ushindi wake huu dhidi ya mpinzani wake wa siasa kali za mrengo wa kulia umekuwa mdogo zaidi kuliko kinyang'anyiro cha mwaka mwaka wa 2017 baina yao wakati ambspo alishinda kwa asilimia 66.1 dhidi ya asilimia 33.9.

Akiwahutubia Wafuasi wake mbele ya mnara wa Eiffel, Macron ameapa kuziba mipasuko katika taifa hilo lililogawanyika pakubwa "Enzi hii mpya haitakuwa mwendelezo wa miaka mitano iliyopita lakini uvumbuzi wa pamoja wa mbinu iliyorekebishwa kwa ajili ya miaka mitano bora ya huduma kwa nchi yetu na kwa vijana wetu"
Screenshot_20220426-041223_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu amempongeza Rais Emmanuel Macron na Chama chake kwa ushindi walioupata baada ya Macron kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Ufaransa.

Rais Samia ameihakikishia Ufaransa kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Nchi hiyo kwa ukaribu katika kukuza masuala ha kiuchumi na Kijamii.

Macron, wa siasa za mrengo wa wastani ameshinda kwa asilimia 58.6 ya kura dhidi ya Le Pen aliyepata asilimia 41.45, kwa mujibu wa matokeo rasmi yaliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Screenshot_20220426-041313_OGInsta%2B.jpg
 
“Niliamua kuanzisha studio ya kurekodi muziki kwa ajili ya kuwasaidia wasaniii wa Dodoma Mjini,na hivyo ni fursa ya kipekee ya kwaya zote zilizopo Jimbo la Dodoma Mjini kwenda kurekodi hapo kwa kuwa hiyo ni huduma yangu kwenu na ni bure kabisa kwasababu hiyo studio nimeianzisha kwa ajili yenu.

Ningependa pia tuwe na matamasha makubwa ya kumsifu Mungu kupitia Kwaya mbalimbali kama ambavyo imekuwa leo na nipo tayari kusaidiana nanyi kuandaa haya matamasha makubwa na kuwatafutia wadhamini” Naibu Waziri wa Kilimo, Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde
Screenshot_20220426-041417_OGInsta%2B.jpg
 
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Wilbroad Mutafungwa ametoa onyo kwa wamiliki na madereva wa coaster zinazofanya safari usiku kinyume na utaratibu kuacha mtindo huo kwani vitendo hivyo vinachangia ongezeko la ajali.
Screenshot_20220426-041522_OGInsta%2B.jpg
 
Tume ya Uchaguzi ya Kenya imewapa siku tatu Naibu Rais wa Kenya, William Ruto na Kiongozi wa Muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga kuwa wametaja wagombea wenza kuelekea uchaguzi mkuu wa Agosti 9, 2022

Screenshot_20220426-041622_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom