Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220410-063146_Opera%20Mini.jpg
 
MGOSI: PABLO ATAVUNJA REKODI SIMBA
.
Nyota wa zamani wa Simba, Mussa Mgosi amesema anaamini kocha, Pablo Franco atavunja rekodi za makocha wageni waliowahi kupita hapa nchini kutokana na mwenendo wake pamoja na matokeo wanayowapata Simba.
.
“Ni kocha anayetumia akili nyingi kufanya kazi zake na kuyatekeleza kwa umakini mkubwa ukilinganisha na makocha wengine, pia anasimamia misimamo yake ambao imekuwa ikimpa matokeo mazuri bila ya wengi kutarajia,” amesema.
.
“Tangu atue na kuiongoza Simba, nimegundua hilo na pia natarajia kuona Simba ikifanya makubwa zaidi ikiwa chini ya Kocha huyo ila jambo kubwa ni kumpatia muda na kumuamini pasipoingilia kazi atazidi kuipasha timu,” aliongeza Mgosi.
.
Screenshot_20220410-124456_Instagram.jpg
 
DJUMA: PENATI SIBAHATISHI
.
“Suala la kupiga penalti sijaanza Yanga ni jukumu maalum nililopewa tangu nikiwa Vita, hivyo nilikuwa nalifanyia mazoezi kabisa na sasa nimelizoea sikumbuki nilikosa lini mara nyingi nimekuwa nikipata,” amesema Djuma na kuongeza:
.
“Penalti haina mwenyewe ni kujiamini na kupiga ukiwa na akili kwamba timu nzima wewe ndio umeibeba ukikosa umewaangusha wachezaji na benchi la ufundi.”
Screenshot_20220410-125035_Instagram.jpg
 
KADUGUDA: NIPO TAYARI KUFA SIMBA IFANIKIWE !!
.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya wa Simba, Mwina Kaduguda amesema kuwa wapo tayari kufa ila Simba ifanikiwe na kufikia malengo yao kwa msimu huu.
.
“Tunaziona timu zilizofanikiwa Afrika kuwa na uwekezaji mkubwa. Simba pia tupo kwenye njia hiyo kwa msimu wa tano sasa kwanini tusifanikiwe kubeba mataji makubwa Afrika?” amesema mwenyekiti huyo wa zamani wa Simba na kuongeza:
.
“Tunaamini tunaweza kumfunga yeyote na kutwaa mataji kama ilivyo lengo letu na nipo tayari KUFA ili kuhakikisha Simba inafikia malengo na kutwa mataji makubwa makubwa Afrika.” amesema Kaduguda [via Mwanaspoti]
Screenshot_20220410-125340_Instagram.jpg
 
NABI: NAAMINI TUTASHINDA DABI NA KUTWAA UBINGWA
.
“Hadi ikifika siku ya mechi naamini kuna baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza waliokuwa majeruhi watakuwa wamerejea na kuongeza ubora wa timu yetu kwenye mechi hiyo kubwa nchini.
.
“Hakuna mechi ya dabi iliyokuwa rahisi, ushindani mkubwa kwenye mechi utakuwepo ila naimani wachezaji wangu watafanya vizuri na kushinda kwani ikiwa hivyo tutakuwa kwenye eneo zuri la kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa ligi baada ya kushindwa kufanya hivyo misimu minne iliyopita.” amesema Kocha Nasreddine Nabi.
Screenshot_20220410-125600_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom