Makapuku Forum

Makapuku Forum

MMESIKIA? BRAZIL WANAMTAKA PEP
.
Pep Guardiola ameripotiwa kupokea ofa ya kutimiza ndoto zake za kuhamia kwenye soka la kimataifa baada ya Brazil kuwa tayari kumlipa mshahara wa Pauni 10 milioni (Sh 30 Bilioni) kwa mwaka ili awe kocha wao.
.
Kocha huyo wa Manchester City aliwahi kuweka wazi mipango yake ya kuingia kwenye soka la kimataifa na sasa mabosi wa Selecao wanaripotiwa kwamba wanamweka kwenye mpango wao.
.
Baada ya kocha wa sasa wa Brazil, Tite kuthibitisha kwamba ataachana na timu hiyo baada ya fainali za Kombe la Dunia 2022 huko Qatar, Marca linaripoti kwamba chama cha soka cha Brazil kinamfuatilia Guardiola akarithi mikoba yake.
Screenshot_20220410-125739_Instagram.jpg
 
Ni POLISI dhidi ya MNYAMA leo kwenye NBC Premier League, Malengo ya Polisi Tanzania kwa mujibu wa Kocha Msaidizi George Mketo ni kumaliza Ligi wakiwa kwenye nafasi tatu za juu lakini hadi sasa wapo nje ya malengo, Simba malengo yao ni kutetea taji lao la Ligi lakini hadi sasa wapo nyuma ya vinara wa Ligi kwa alama 11 kabla ya mchezo wa leo. Simba ipo nyuma ya Yanga kwa mchezo mmoja!
Screenshot_20220410-125942_Instagram.jpg
 
Uwanja wa West Ham unatambulika kama London Stadium au Queen Elizabeth Olympic Park, ni moja kati viwanja viliyotumika kwenye Olympic 2012 jijini London

Lakini maswali yanaweza kuwa ni mengi, kwanini kabla ya mechi au bao likifungwa basi kunakuwa na vitu kama mapovu uwanja mzima?

Yes huo ni utambulisho wa West Ham tangu miaka ya 1900, kama ambavyo Liverpool wametumia wimbo wa You’ll never walk alone wa Gerry na Pacemakers uliotungwa 1960 kutokana na kuwakilisha utamaduni wao

Kama ambavyo Newcastle wanatumia wimbo wa The Blaydon races unaoelezea utamaduni wa Magpies huko Kaskazini Mashariki mwa Uingereza, ndivyo ilivyo kwa West Ham

West Ham wana wimbo uitwao “ I’m forever blowing bubles” ambao ulitungwa na James Brockman, wimbo huu ukapendwa sana na Hammers wakautumia rasmi kama anthem

Maana ya wimbo huo ni kuwa “Nitapuliza mapovu daima” hivyo wakati wanaimba ndipo hayo mapovu yanatoka kupitia mashine maalum zilizofungwa uwanjani hapo

Ni utamaduni wao
Screenshot_20220410-130104_Instagram.jpg
 
Shaffih Dauda

MSIMU WA 2021/22, SIMBA NA YANGA WOTE MABINGWA

Well ni msimu ambao inaonekana wazi Yanga ana uwezekano mkubwa wa kutwaa ubingwa baada ya misimu minne, baada ya muda mrefu wa kujaribu na kufeli ni sasa kama hesabu zao zinaenda sahihi

Kwa mechi zilizosalia na utofauti wa alama basi uwezekano ni mkubwa kwa Jangwani labda maajabu ya mpira wa miguu yatokee, timu haijapoteza mchezo mpaka sasa, inakosa baadhi ya wachezaji ila bado iko imara

Katika hatua ya kwanza nasema Yanga ni bingwa apewe taji lake msimu huu, utofauti wa alama ni mkubwa, tayari timu vigogo kama Azam wameachia alama, timu pekee iliyosalia ni Simba ila nyingi Yanga anapewa nafasi akicheza nazo

Lakini kwanini Simba nae apewe ubingwa msimu huu?? Apewe ubingwa upi??

To me naona wanastahili ubingwa kwa heshima kubwa ya TRANSITION wanayofanya kwenye mipango mikakati ya klabu yao, kuna kitu ambacho wengine wote wanastahili kukiiga kutoka kwao

Wapo nafasi ya pili kwenye ligi nyuma ya Yanga ila hawana presha kubwa wanaendelea kucheza mechi zao huku wakipiga hesabu zao kwa usahihi, wapo kwenye FA, wapo Ligi kuu bara na wapo Shirikisho Afrika, kote wapo hatua nzuri

Inakupa tafsiri kubwa juu ya Management yao, sio rahisi kuwa na malengo matatu na yote yakaendana, yote ukawa kwenye hatua kubwa, huwa tunaona kuna baadhi ya timu huamua kupigania kikombe kimoja na kuipa nguvu yote

Huenda Simba wanaweza wasitwae kikombe cha Ligi kuu ila wanatwaa ubingwa wa darasa la bure kwa klabu nyingi, bado kupitia ushiriki wao kimataifa umesaidia kupeleka timu nne kwa mara ya pili mfululizo

Nafasi nne zilizopatikana zinaongeza chachu kwenye ligi, kwenye vita ya kupata hizo timu! Bado inaongeza thamani ya ligi, inatangaza nchi kimataifa, nje ya ubingwa wa Yanga pia kuna ubingwa wa Simba

Anapopewa taji Yanga msimu huu, kuna taji ambalo pia Simba analibeba tena na tena kwa heshima ya mpira wa miguu, IKITOKEA
Screenshot_20220410-131406_Instagram.jpg
 
Nyota wa Ureno na Manchester United, Cristiano Ronaldo ameomba radhi kwa kitendo chake cha kupiga chini simu ya Shabiki aliekuwepo uwanjani kutazama mchezo wa United dhidi ya Everton pale Goodson Park

Baada ya video kuchapishwa mtandaoni juu ya tukio hilo huku United wakianza uchunguzi, Ronaldo amepost akiomba radhi na kumualika Shabiki huyo Old Trafford kutazama mechi kama sehemu ya kuonesha uungwana
Screenshot_20220410-131533_Instagram.jpg
 
| NATHAN FASIKA SIMBA SC
.
Kwa mujibu wa GoalAfrika, Mabingwa wa nchi Simba SC na klabu ya Cape Town City ya Afrika Kusini zimefikia Makubaliano ya kuuziana Beki wa Kati raia wa DR Congo Nathan Idumba Fasika Uhamisho wa Nyota huyo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa msimu huu.
Screenshot_20220410-152431_Instagram.jpg
 
Baada ya kufunga ndoa na Doreen Mrema, Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema aliahidi kuwa honeymoon yake ataitumia kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii Tanzania ambapo tayari ameanza na Tarangire.

Hizi ni picha ambazo zinamuonesha akiwa Tarangire ambayo ni hifadhi yenye mvuto wa kipekee ikiwa pia ni moja ya hifadhi maarufu katika kanda ya kaskazini.

Sifa kubwa ya Hifadhi hii ni makundi makubwa ya Tembo, mibuyu mikubwa , chatu wapanda miti na wanyama wengine wengi kama simba na inasifika kwa kuwa location sahihi kwa honeymoon (fungate) kama rest houses na sehemu zingine za malazi ya private ambazo ni nyingi sana.

Wageni wengi wamekuwa wakifanya harusi zao katika hifadhi hii kutokana na ukaribu wa hifadhi hii na Arusha.
Screenshot_20220410-152707_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amekutana na Rais Zelensky wa Ukraine katika Mji wa Kyiv nchini humo na kuahidi kuipa ushirikiano Ukraine katika mapambano dhidi ya Urusi.

Boris amempongeza Rais huyo kwa kuendelea kuongoza Wananchi kwenye mapambanao na kumuahidi kuwa Uingereza itaipa Ukraine msaada mpya wa kifedha na silaha za kivita.

"Ukraine wana ujasiri wa Simba na Rais Zelenskyy ana koromeo la Simba la kuwapazia sauti, Uingereza inasimama na Ukraine" alisema Boris.
Screenshot_20220410-152859_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema mafuta yapo ya kutosha na bado kuna meli za mafuta zinaendelea kuwasili nchini.

RC Makalla amesema hayo wakati wa mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Abdulrahman Kinana katika Mkoa wa Dar es Salaam.

"Kulitokea sintofahamu kwamba mafuta yamepanda bei, Tanzania haiwezi kuwa Kisiwa kutokana na hali inavyoendelea kule na hata soko la Dunia tunanunua kwa Dola na imebadilika”

“Nawahakikishia mafuta yapo ya kutosha na Meli nyingine zipo njiani, kazi yetu kama Serikali ni kuhakikisha tunawabana Wafanyabiashara wasio waaminifu wasifiche mafuta ili yawe adimu lakini wauze kwa bei elekezi" ———
Screenshot_20220410-153137_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom