SIMBA KIMATAIFA HANA MPINZANI[emoji91][emoji91]
Na @emanuelmwayombojr
Huwezi tumia nguvu nyingi kuelezea ubora wa @simbasctanzania katika michuano ya Kimataifa kwa sababu katika Nchi yetu wamejitengenezea daraja la peke yao wakifika katika hatua ya kushiriki michuano hii.
Kizuri zaidi kwa sasa Simba wanajua wao ni washindani katika michuano hii iliyo chini ya CAF ndiyo maana hata mashabiki wao wanaamini wao ni moja ya timu bora Afrika hivyo hawapendi kabisa kusikia habari ya kuondoshwa mapema katika michuano hii kwa sababu hivi sasa Simba kung'olewa katika hatua ya awali katika michuano hii ni stori kubwa kwa kuwa kila mdau wa Kandanda ana amini Simba wanaweza kufanya makubwa katika ngazi hii ya mashindano ya Vilabu bora barani Afrika.
Simba tangu miaka ya nyuma kabla @moodewji hajatia maguu kuwekeza fedha zake walishaonyesha mwanga linapokuja swala la International competition wao ni mwamba wakiwa na bajeti finyu lakini vigogo wengi wa Afrika ilikuwa ni vigumu kutoka salama katika ardhi ya Mkapa hivyo kwa sasa baada ya uwekezaji mkubwa wameonyesha makucha yao kwamba wao ni wa Kimataifa.
Vilabu vingine Tanzania vinatakiwa kujifunza kutoka kwa Simba, kwa sababu Simba siku zote wanaamini wakiwa katika ardhi tukufu ya Tanzania hatoki Mtu hii imewajenga hata wachezaji wao kupambana kwa Nguvu zao zote kwa sababu wana amini wakiwa nyumbani wamebeba imani ya mashabiki lukuki.
Alfred the great (King of wessex) aliwahi kusema Huwezi kushinda vita kama bado hujajiamini kama unaweza Simba SC kwa sasa wanaamini michuano ya Kimataifa ni jukwaa Lao la kutamba ndiyo maana wanafanya vema kwa sasa na kuipaisha ligi ya Tanzania.
Bila ubora wa Simba katika michuano hii ligi ya Tanzania bado ingekuwa mafichoni ubora wa Klabu hii Kimataifa umesabibisha ligi yetu kuwa moja ya ligi inayotupiwa macho zaidi hapa Afrika kwa sasa hakuna Mchezaji yoyote atakaye kataa kucheza ligi ya Tanzania kwa sababu anajua ligi hii inafatiliwa.
Bila ubora Simba Kimataifa nani angetambua Tanzania ni moja ya ligi yenye ushindani mkubwa ndani ya kiwanja na soka la kuvutia?Basi Nguvu yetu kubwa iwe kuinua Vilabu vingine vitishe Kimataifa.