Makapuku Forum

Makapuku Forum

Shabiki mmoja Kijana wa Uingereza amehukumiwa kifungo cha wiki sita jela baada ya kupatikana na hatia ya kumtukana na kuonyesha ubaguzi wa rangi kwa Mchezaji wa Manchester United Marcus Rashford baada ya kushindwa kufunga penati kwenye mechi ya England katika fainali ya Euro 2020.

Kijana huyo Justin Lee Price (19) kutoka Worcester, Uingereza alikiri kosa katika Mahakama ya Kidderminster ya "shitaka moja la kutuma ujumbe wa kuudhi kwa mtandao wa mawasiliano ya umma".

Kijana huyo awali alikanusha mashtaka hayo wakati wa mahojiano na polisi, pia alibadilisha jina lake kwenye account yake ya Twitter ili kuepuka kutambuliwa lakini baadae alikiri kufanya kosa hilo, muda wa kifungo chake ulipunguzwa kwasababu alikiri kosa na kukubali mashtaka yake Mahakamani.
Screenshot_20220401-092339_Instagram.jpg
 
EDO: MORRISON ANANICHEKESHA AITWE GHANA !?
.
Kuna ukweli mwingi ambao Morrison anausahau. Amekuwa akiwaponda kina Andre Ayew na mdogo wake Jordan Ayew kama vile wapo nyuma yake kisoka naye kupitia hizi mechi dhidi ya Coastal Union anaona kama anastahili kuitwa timu ya taifa ya Ghana.
.
Mpira una viwango vyake. Kuna Waghana zaidi ya 100 ambao inawezekana kiasili hawafikii kipaji cha Morrison, lakini wanacheza soka katika nchi ambazo ligi zao ni bora kuliko Tanzania. Ghana wanakuchaguaje wakati unacheza Tanzania?
.
Rafiki yangu Morrison ananichekesha. Nimepitia orodha ya Waghana wanaocheza timu ya taifa nje ya watoto wa Abeid Pele nimekutana na watu wanaocheza Ligi Kuu za Ujerumani, Ubelgiji, Ufaransa, England na kwingineko. Alitaka aitwe kwa sababu gani? Ulazima huo unatoka wapi?” - Edo Kumwembe
.
WADAU mnasemaje __!!
Screenshot_20220401-092545_Instagram.jpg
 
Giannis Antetokounmpo wa Milwaukee Bucks amevunja rekodi ya kufunga points nyingi ya' Legend' Kareem Abdul-Jabbar. Katika mchezo wa jana dhidi ya Brooklyn Nets, Giannis Antetokounmpo alifunga points 44 na kufikisha jumla ya points 14,216 na kuvuka rekodi ya Abdul-Jabbar ambaye alifunga points 14,211 akiwa na Milwaukee Buck na hivyo kuwa Mfungaji wa muda wote wa Milwaukee Bucks.
Screenshot_20220401-092918_Instagram.jpg
 
Mkufunzi raia wa Argentina Hector Cupper amevunja mkataba wake wa kuifundisha timu ya taifa DR Congo baada ya kushindwa kuisadia kufuzu katika fainali za kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Qatar.
Screenshot_20220401-093032_Instagram.jpg
 
Tanzania tumepanda nafasi mbili katika viwango vya CAF, kutoka nafasi ya 39 na sasa 37
Screenshot_20220401-093322_Instagram.jpg
 
Mataifa yaliyoshiriki fainali za kombe la dunia mara nyingi zaidi

Samba boys wanaongoza kwa ushiriki na wanaongoza kwa makombe pia
Screenshot_20220401-093834_Instagram.jpg
 
Mataifa makubwa yakayozikosa fainali za kombe la Dunia Qatar
Screenshot_20220401-094452_Instagram.jpg
Screenshot_20220401-094527_Instagram.jpg
Screenshot_20220401-094601_Instagram.jpg
Screenshot_20220401-094627_Instagram.jpg
 
Anaitwa Davide Ancelotti, mtoto wa Kocha Carlo Ancelotti ambaye ndie Kocha mkuu wa Real Madrid huku mwanae huyo akiwa msaidizi wake

Kutokana na Baba yake mzazi kukutwa na maambukizi ya COVID 19, Kijana huyo atabeba majukumu ya kukiongoza kikosi cha Real Madrid ugenini dhidi ya Celta Vigo

Ana umri wa miaka 32, amezaliwa Parma nchini Italia, ni wakati sasa wa kuona weekend hii kama kweli kitanda hakizai haramu
Screenshot_20220401-094803_Instagram.jpg
 
"Usafiri utakuwepo hadi saa 5, 6 usiku. Tutawapeleka maeneo yote wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambao watakuwepo uwanjani siku hiyo, utakuwepo pia usafiri wa kwenda Kibaha."- Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Tanzania (TADU), Jaeka Odillo Mdami. #NguvuMoja
Screenshot_20220401-095245_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom