Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Vladmir Putin wa Urusi ameziambia Nchi mbalimbali zinazonunua gesi ya Urusi ikiwemo Ujerumani na Italia kwamba ni lazima zianze kulipia gesi hiyo kwa kutumia pesa ya Urusi (ruble) na kama sio hivyo basi hazitoipata hiyo gesi.

Vladimir Putin ametia saini kwenye amri mpya inayosema Wanunuzi wotelazima wafungue akaunti za ruble kwenye benki za Urusi kuanzia Ijumaa "Hakuna mtu anayetuuzia chochote bure na hatutafanya hisani pia".

Agizo hilo jipya la Putin kutaka kulipwa kwa fedha ya Russia ni jaribio la kuongeza sarafu hiyo ambayo imeathiriwa sana na vikwazo vilivyowekwa na Nchi mbalimbali za Ulaya na America.
Screenshot_20220401-081145_Instagram.jpg
 
Tariq Awaz Kipemba ambaye ni Mkazi wa Shanti town mkoani Kilimanjaro ameongea kwa mara ya kwanza toka tukio lake la kumwagiwa kitu kinachoaminika kuwa ni tindikali ambacho kimemuumiza kwenye maeneo ya usoni na mikononi.

Tariq ambaye sasa ametimiza mwezi mmoja akiwa kalazwa Hospitalini KCMC amesema anahisi Mtu aliyehusika na kitendo hicho ni rafiki yake ambaye wamekua na ugomvi kwa muda mrefu ambapo siku ya tukio alifuatwa na Vijana wawili wakiwa na pikipiki na kumwagia kimiminika akiwa maeneo ya Shanti town, Moshi Kilimanjaro.

Video nzima ya Tariq akisimulia ipo kwenye Youtube ya millardayo na unaweza kuitazama moja kwa moja kwa kubonyeza link kwenye bio yangu hapa Instagram.
Screenshot_20220401-081325_Instagram.jpg
 
Rais Samia amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri ambapo George Simbachawene, Waziri wa Katiba na Sheria amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.

Damas Ndumbaro, Waziri wa Maliasili na Utalii amehamishiwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria na Pindi Chana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Sera na Uratibu) amehamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.
Screenshot_20220401-081449_Instagram.jpg
 
Kijukuu cha mtume. Imagine watu wakuseme WhatsApp na pm na bado ukapata screen shot, bado tena mwingine ascreen shot azirudishe humu humu. Hao wamama na mubaba wao mbabaifu wangejua tu upupu wanaodanganyana ni uongo. Mungu hawezi kuumbua watesi wako hadharani hivi ujue.

Nyie wamama huo muda mnakuja na matusi sijui kuliwa (hakuna ajabu kabisa kwenye kukulana washamba tu ndo wanaonaga big deal) mshauri mubaba wenu aache kujipa umuhimu na kujiongelesha uongo. Na mtumie akili huyo mubaba anatumia mvinu ya divide and rule ila kwa kuwa kikundi chote hamna akili mnatumia infos za uongo mnazopewa kumuattack mwingine
Akili ni mali my dear.
 
Doooh. Ukute ndo wale wanaojifanyaga hawanaga muda na watu . Naomba huu ubuyu vizuri WhatsApp my ndugu
unaafiki mbaya sana!mi nshashindwa kupretend kwa kua najijua ni mwanadamu i have strength and weaknesses zangu kama mtu atanihukumu tu kwa mabaya yangu sawa ntashukuru pia

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limepiga kura ya kumuondoa Waziri wa Uchumi Jean-Marie Kalumba kutoka kwenye nafasi hiyo likimlaumu kwa kupanda kwa bei ya bidhaa za kimsingi na usimamizi mbovu wa sekta ya uvuvi.

Waziri huyo ana saa 48 za kuwasilisha barua yake ya kujiuzulu kufuatia kura ya kutokuwa na imani naye ambayo imepigwa mwaka mmoja tu toka alipoteuliwa na Rais Felix Tshisekedi.

Hoja iliyotiwa saini na Wabunge ilitoa malalamiko mengi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa sera ya kusaidia wavuvi wa ndani na uhaba wa gesi mara kwa mara unaosababisha bei ya usafiri kupanda.

Congo ni nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa shaba barani Afrika na mchimbaji mkuu duniani wa madini ya betri ya cobalt lakini inasalia kuwa mojawapo ya nchi maskini zaidi duniani.
Screenshot_20220401-091725_Instagram.jpg
 
Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kinachoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Samia Suluhu Hassan leo kimetangaza kumsamehe na kumrudishia uanachama Bernard Membe baada ya kuandika barua ya kuomba msamaha.
Screenshot_20220401-091900_Instagram.jpg
 
Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amepitishwa na Halmashauri Kuu ya CCM leo kuwa Mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara wa Chama hicho.

Dakika chache zilizopita Philiph Mangula ambae alikua akiishikilia nafasi hiyo aliwasilisha barua ya kung’atuka katika nafasi hiyo.
Screenshot_20220401-092012_Instagram.jpg
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Tanzania Bara, Philip Mangula leo amewasilisha katika Halmashauri Kuu ya CCM barua ya kung’atuka katika nafasi hiyo.

Mwenyekiti wa CCM Samia Suluhu Hassan leo anaongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Dodoma, taarifa zaidi kukujia.
Screenshot_20220401-092115_Instagram.jpg
 
Mwanamke mmoja wa Afrika Kusini ambaye alitumia pesa aliyotumiwa kimakosa karibu $ milioni 1 katika akaunti yake ya benki amefungwa jela miaka mitano.

Sibongile Mani alipokea randi 14m badala ya 1,400 alizostahili kupata mwaka 2017 akiwa Mwanachuo na kuanza kuzitumia mara moja, pesa hizo zilitoka kwenye Mpango wa Kitaifa wa Msaada wa Kifedha kwa Wanafunzi (NSFAS) ambapo hakuripoti kosa hilo na badala yake akaanza kuzitumbua ndani ya dakika 120 tu baada ya kuzipokea.

Mpaka Mamlaka zinafanikiwa kuizuia account yake tayari alikuwa ametumia karibu $ 70,000 (Tsh. milioni 160+) katika maeneo 48 kote nchini kwa siku 73 na alitumia pesa hizo kununua nywele bandia, smartphone, pombe, godoro, kadi za zawadi na bidhaa nyingine za kifahari.

Mahakama imesema ni jambo la kushangaza kwamba alikuwa ameweza kutumia pesa nyingi kwa siku chache kote nchini huku Jaji akisema kuwa matumizi yake yalichochewa na uchoyo akitupilia mbali hoja kwamba alitumia hivyo kutokana na kuwa na maisha duni.
Screenshot_20220401-092219_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom